Mchezo huu wa Yanga na Al Hilal ni ngumu kutabirika

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Kuna wakati sisi mashabiki wa Yanga tunatabiri sijui hawa watakufa 1 au mbili huko kwao, ila ukiangalia vizuri hawa Al Hilal japo siyo bora zaidi yetu, wao wana viongozi wazoefu kwenye mashindano haya.

Tutoke uko twende kwenye ufundi, hawa Al Hilal wakituchezea mipira ya juu kwa beki zetu zile na vimo vyao ni Mungu na maombi. Nilikuwa naona walivyokuwa wanapata shida ya kushinda mipira ya juu.

Pia Al Hilal mashambulizi yao mengi yanatoka pembeni sana, kwa hiyo naomba beki zetu wa pembeni wawe makini sana. Ikiwezekana wakabe "Batle kwa batle" yaani mtu kwa mtu siyo wampe nafasi ya kukimbia. Mawinga wa Al Hilal wana mbio sana kuzidi mabeki wetu.

Kwahiyo tukiwazuia huku tutakuwa tumeshinda mchezo. Kuhusu washambuliaji wetu sina mashaka, naona sura ya Fiston inaonesha hawa Al Hilal watafungwa tu, tatizo ni ulinzi wetu.
 
Wala hamna cha kutabiri hapo. Labda useme unatabiri atafungwa over ama la?
 
Hili hata Shetani analijua, yanga ameshahamia shirikisho. Tukutane mwakani kilabu bingwa ila mwaka huu imeisha hiyo.
Al hilal wameshafuzu, mpira unachezwa uwanjani na kila mtu ashinde nyumbani kwake
 
Wachambuzi wanasema yanga ni bora kuliko al hilal uwanjani, je hukuona ibenge alipoamua kuingiza watu wa kazi kipindi cha pili ulivokua unataman mpira uishe? Sasa kama unasema ubora wa al hilal upo kwa viongoz unamaanisha hamuamini tena injinia na wenzie? Eti semeni wa2achie timu yetu sawa?
 
Pambaneni watani zangu, mechi iko wazi hii, mnaweza mkatoboa pia
 
Kwani TFF hawajawapa kiloba cha mbinu kama walivyoagizwa na waziri?
 
Tatizo la Utopolo mechi wanachezea maneno,na wachambuzi uchwara wako busy kuwasifia ujinga
 
Ni mgumu kweli ila Yanga lazima ifungwe
 
Je?Yanga ataweza kushikilia bomba dakika 90?,maana gemu ya kwanza tu wasudani walishikilia bomba na bado waliongoza kwa short on target nyingi,imagine akifungua turbo [emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…