Mchezo (mwingine ) mchafu kumchagua DG mpya DAWASCO

Kwani sheria inasemaje kuhusu uteuzi wa CEO wa DAWASCO? Ni bodi au waziri mwenye dhamana ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kwenye teuzi?
 
Kama kuna sheria na taratibu, migongano inatokea wapi?nani hafuati taratibu? na kwa nini?
 
Nilikuwa namuamini sana Mwandosya,kumbe na yeye ni hopeless.Kazi ipo sasa amebaki nani kati ya hawa washika dau wa nchi hii
 
Siku zote kukitokea changes kuna watu wanachukua muda kuelewa!

I doubt, they may not be wrong only that we do not have full information. We only have one sided information and probably coming from loosers....
Yes indeed! Sometimes it is good to seek to understand before being understood
 
Sikumbuki jina la wimbo huu wa Dr Remmy Ongala kabla hajaanza kuimba gospel nakumbuka maneno yake kama ifuatavyo: "Walipewa madaraka wakayatumia vibaya, walipewa madaraka wakalala usingizi tembo wanateketeaaa..... uchumi wa taifa unatoweka..... saa tatu asubuhi walevi kwenye supu......" (mwisho wa wimbo)
Kuhusu tembo ofcourse alikuwa anaponda kumilikishwa waarabu vitalu vya uwindaji pale ngorongoro. Kuhusu kulala usingizi alikuwa anazungumzia serikali kuu kutokuwa makini na mambo mengi yaliyokuwa hayaendi sawa wakati huo, nadhani ilikuwa miaka ya mwanzo ya tisini.
Mwenye huo wimbo atuletee unafaa kutukumbusha kwamba hii nchi wameibinafsisha zamani hivi sasa wanahitimisha tuu nasi tuendelee kulala usingizi mwisho wetu kama taifa hauko mbali.
 
Matatizo Dawasco yasimsubiri Waziri Mkuu


Mwandishi wetu
Daily News; Saturday,March 22, 2008 @21:01

SIKUUSHANGAA msimamo wa Wafanyakazi wa Kampuni ya Maji Safi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasco) kumkataa Mkurugenzi Mkuu wao, Alex Kaaya, wao si wa kwanza kufanya hivyo kwa sababu zinazofanana na walizozisema Ijumaa wiki hii.

Madai ya wafanyakazi kuhusu maslahi ni jambo la kawaida, lakini si kawaida kwa Mkurugenzi Mkuu kutakiwa kujiuzulu, Mhandisi Kaaya kajikuta katika wakati mgumu kwa kuwa kaambiwa apime uzito wa hoja za wafanyakazi!

Malalamiko ya wafanyakazi Dawasco yamenikumbusha yaliyotokea hivi karibuni katika Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), waligoma kushinikiza kuongezewa mishahara, wakaongezewa na wameahidiwa nyongeza nyingine Agosti mwaka huu.

Kwa mtazamo wangu, yanayotokea Dawasco yanaweza kufikia huko, kuna madai matatu ya msingi, uongozi, mishahara midogo kwa wafanyakazi wakongwe na tofauti kubwa ya mishahara baina ya wafanyakazi.

Hata kama Kaaya ataachia ngazi mengine yasipotafutiwa ufumbuzi moto utaendelea kuwaka Dawasco kwa kuwa kuna kila dalili kuwa kampuni hiyo imegawanyika kimatabaka na hakuna amani.

Kwa mtazamo wangu jambo la msingi nani anaiongoza Dawasco bali anafanya nini na Dawasco inatekeleza vipi wajibu wake kwa wananchi. Kwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Tanzania (TUICO), Boniface Nkakatisi ameahidi kuwa Kaaya atazifanyia kazi hoja za wafanyakazi, naamini kipaumbele kitakuwa ni kutatua matatizo yaliyopo katika kampuni hiyo kwa uongozi mpya au wa sasa, na si visasi.

Wafanyakazi wametoa kero zao hadharani katika Ukumbi wa Almuntazir, Dar es Salaam, bila shaka hawatafukuzwa kazi, naamini walisema waliyoyasema kwa nia njema, kwa faida yao na Dawasco hususan uhusiano baina yao na viongozi wao.

Kama waliyoyasema ndiyo ukweli, Dawasco inakwenda kubaya, malengo ya kuianzisha kampuni hiyo hayatatimia hivyo huduma bora za maji safi na maji taka kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani zitaendelea kuwa ndoto.

Kama Dawasco hawatachukua hatua, serikali itimize wajibu wake, kampuni hiyo ipo kwa faida ya wananchi, maslahi ya umma yazingatiwe kwanza, kila mtu atimize wajibu wake kwa nafasi aliyonayo.

Jambo la msingi ni huduma bora za maji kwa wananchi, kama viongozi waliopo Dawasco ni tatizo waondolewe ili waje wengine watakaoiwezesha kujiendesha kwa faida, na kumaliza kero nyingine katika kampuni hiyo.

Yaliyosemwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo yanaonyesha kuwa wamekata tamaa, wanahitaji matumaini, kwa kuwa hawamtaki Mkurugenzi wao Mkuu ni wazi kuwa mkono wa serikali ni muhimu katika suala hilo.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya na mamlaka nyingine wasisubiri hadi wafanyakazi wa Dawasco wagome, wameyasikia madai ya wafanyakazi, yafanyiwe kazi haraka bila kuupendelea upande wowote.

Wakati Kaaya anaendelea kupima uzito wa hoja za wafanyakazi, serikali nayo ifanye hivyo hivyo, hakuna njia ya mkato katika hili, kuna matatizo mengi Dawasco ukiwamo udhaifu wa kukusanya fedha za malipo ya huduma za maji.

Mhandisi Kaaya na wasaidizi wake wakuu wajifanyie tathmini kama wanafaa kuendelea na madaraka waliyonayo Dawasco, malalamiko ya wanaowaongoza iwe ni msingi wa maswali ya kujiuliza ikiwa ni pamoja na, je moja ya sifa ya uongozi wao ni kuwa na makundi Dawasco?
 
Date::1/23/2009Ukosefu wa maji : Kero iliyokosa ufumbuzi wa kudumu Dar
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Professa Mark MwandosyaNa Jonas Songora

MALALAMIKO juu ya ukosefu wa maji safi na salama kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam, yamezidi kuwa mengi huku lawama lukuki zikipelekwa kwa Kmpuni ya Maji Safi na Maji Taka jijini Dar es Salaam (Dawasco).

Wakazi wa jiji hili wanaokadiriwa kufikia milioni nne, wamekuwa wakiishi kwa taabu kutokana na ukosefu wa maji safi kuwa tatizo la kawaida kwa kipindi kirefu sasa, huku hatua zinazochukuliwa kumaliza tatizo hilo zikisua sua.

Mara kadhaa Mkurugenzi Mtendaji wa Dawasco, Alex Kaaya, amekuwa akikaririwa akisema kuwa, ukosefu wa maji safi na salama kwa wakazi wa jiji hilo, unachangiwa zaidi na miundo mbinu isiyotosheleza iliyopo sasa.

Anadai kuwa miundo mbinu hiyo imekuwapo kwa miaka takriban ishirini na tano ilioyopita wakati jiji hili likiwa na idadi ndogo ya watu tofauti na sasa ambapo pamoja na kuongezeka kwa idadi ya watu, jiji hilo linapanuka kwa kasi.

Hali hiyo inachangia baadhi ya watu kujikuta katika maeneo ambayo hakuna kabisa miundo mbinu ya kufikisha maji safi na salama na wakati mwingine bado kunakuwepo na shida ya vyanzo vya maji kuhudumia wakazi wote wa jiji.

Ukweli huu wa mambo unaungwa mkono na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Professa Mark Mwandosya, ambaye anakiri kuwa huduma ya utoaji maji safi kwa wakazi wa mikoa ya Kanda ya Pwani, hairidhishi na inatakiwa kuboreshwa.

Prof. Mwandosya anasema kuwa, takribani watu milioni tano wanaoishi katika jiji la Dar es Salaam, Bagamoyo na Kibaha mkoani Pwani, hawafikiwi na huduma ya maji safi na salama.

Hili ni tatizo kubwa, kwani kutokana na tatizo hili idadi kubwa ya watu huathirika kiafya kutokana na maradhi yanayosababishwa na utumiaji wa maji yasiyo safi na salama. Miongoni mwa maradhi hayo ni ugonjwa wa kipindupindu ambao umekuwa wa kawaida masikioni mwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.

"Watu hawa milioni tano ambao ni sehemu ya watu milioni saba wanaoishi katika mikoa hiyo miwili, hawafikiwi na huduma ya maji safi na salama kutokana na miundo mbinu mibovu na isiyoendana na hali halisi ya ukuaji wa idadi ya watu," anasema Prof.Mwandosya.

Anaongeza kuwa, ili kuhakikisha kuwa wananchi walio wengi wanapata huduma nzuri ya maji, Dawasco hawana budi kupanua wigo wake wa miundo mbinu.Kwa kufanya hivyo, watatoa huduma ipasayo kwa wananchi wa mikoa hiyo.

Akionyesha kuwa bado hajaridhishwa na utendaji wa Bodi ya Dawasco, Prof. Mwandosya anasema kuwa muda uliosalia hadi kufanyika uchaguzi mkuu nchini ni mchache, hivyo Bodi ya Dawasco inalo jukumu kubwa kuhakikisha kuwa inatekeleza majukumu yake katika kipindi hiki kifupi.

"Tuna mwaka mmoja na miezi michache tu ili kufikia lengo hilo, hivyo bodi inatakiwa kusoma na kuelewa kwa makini malengo na viashiria vilivyowekwa kwenye mkataba wao, ili waweze kupima utekelezaji wake mara kwa mara," anasema Mwandosya.

Lakini tatizo ni kubwa zaidi ya hapo, kwani imebainika kuwa ukosefu wa maji pia unachangiwa na wafanyakazi wenyewe wa Dawasco ambao wamekuwa mstari wa mbele kufanya vitendo vichafu vilivyo nje ya maadili yao ya kikazi hivyo kudhoofisha utoaji wa huduma bora.

'"Wafanyakazi wanashirikiana na baadhi ya wateja wasio waaminifu katika kuchepusha dira ya maji, wizi wa maji, vitendo kama hivi haviwezi kuwa vinafanywa na wananchi wasiokuwa na utaalamu bali ni wafanyakazi wetu wenyewe kwani wao ndio wenye utaalamu katika sekta hiyo," anaeleza Prof Mwandosya.

Anaongeza kuwa kutokana na hali hii ya uhujumu inayofanywa na wataalamu, athari zake ni kubwa kwani miundo mbinu iliyopo huhujumiwa. Hali hii inasababisha kutolipwa kwa ankara sahihi hivyo kuikosesha Dawasco mapato stahili.

Pia kuna changamoto nyingine ambazo ni kikwazo katika utoaji wa huduma nzuri ya maji kama vile uwezo mdogo wa mitambo ya Ruvu Juu, Chini na Mtoni, huku kukiwepo na uvujaji wa maji kwa asilimia hamsini ya maji yote yanayopatikana.

"Matatizo hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kutofikiwa kwa malengo ya ukusanyaji wa mapato ambacho ni kiasi cha Sh 2.5 bilioni kwa mwezi,"anaeleza.

Mwenyekiti wa Bodi ya Dawasco, Mhandisi Suleiman Suleiman, anasema kuwa vitendo vya kihalifu vinavyofanywa na wafanyakazi wa Dawasco hadi kufikia kufifisha juhudi za kusambaza huduma za maji ipasavyo kwa wateja wake,vinatokana na wafanyakazi hao kutopewa maslahi mazuri.

"Kampuni imejipanga kutoa maslahi mazuri kwa wafanyakazi wake ili hatimaye wajiepushe na vitendo vya kihalifu. Kwa kufanya hivyo, huduma zetu kwa wateja zitakuwa bora zaidi," anasema Suleiman.
Anasema kuwa mipango mingine iliyopo ni kuhakikisha kuwa wanakabiliana na changamoto zinazochangia ukosefu wa maji kwenye baadji ya maeneo na kudhibiti uvujaji wa maji, wizi wa miundo mbinu na kuongeza upatikanaji wa maji anagalau katika maeneo yote.
 
tatizo la 'dawasco na mashirika mengi ya bongo ni mfumo tuliowekewa na watawala ambao unawapa nafasi wanasiasa kutuchagulia viongozi wa siasa mpaka viongozi wa kitaaluma.
hivyo ni vizuri kazi kama hizi zikaachiwa civil service commmission kufanya kazi yake.
badala ya waziri au bodi.
katika suala hili bila kuficha nk tuangalie Kaaya ni Zao la Nani? hata kama ana qualications (uhandisi) etc aliteuliwa Vipi? Bodi ilikuwaje au ipoje? utakuta zote ni zao la EL-fiasadi alipokuwa waziri wa Maji na kuongezea madaraka aliyo shika baada ya hapo.
Sasa waziri ni mwingine lakini Bodi ni hiyo hiyo? je bodi inamsaidia waziri au imekuwa kama daraja lililobonmoka?
kuna watu wameuliza nani mwenye mamlaka kati ya waziri au bodi lakini ukifuatilia uchangiaji hapa utaona ni waziri kisiasa na techincally ni bodi, maana tunaambiwa bodi iliomba kibali toka kwa waziri, halafu bodi ikaona masuala yake ndio haya watetezi
 
Sasa ni lazima haya makampuni yaachwe kujiendesha bila mkono wa moja kwa moja na watawala. Wakiwa wameoza basi yooote nayo yanaoza
 
Utaratibu wa kuwapata hawa maDG kama wa DAWASCO na pia wajumbe wa Board kama vile EWURA una walakini mkubwa ingawa on the surface inaonekana kuna some semblance of TRANSPARENCY katika kuwapata wahusika!! Wizara ya Maji inacontract anindependent consulting firm kutangaza nafasi hizo na watu huomba kufuatana na qualifications zinazohitajiwa kwa nafsi husika; baada ya hapo majina ya walioomba yanachambuliwa na waliotimiza masharti wanakuwa shortlisted na kuitwa kwenye usaili. Kitu chakushangaza badala ya usaili huu kufanywa na hiyo independent firm , unafanywa chini ya uenyekiti wa katibu Mkuu wa wizara ya Maji na wajumbe wanaowateuwa wao toka kwa so called stakeholders ambao mara nyingi wanakuwa watu wasiokuwa na uelewa na mambo kama ya EWURA!! Sasa kwa mfumo kama huo unataegemea waziri husika na katibu wake Mkuu wasiwateue cronnies wao?? Utaratibu unaofaa ni ule wa independent consultans kufanya kazi yote toka kutangaza mpaka usaili na wizara kupelekewa majina ya walioshinda na wizara kufanya uteuzi bila kupendelea on the basis ya mapendekezo ya consultants. Lakini haifanyiki hivyo kwa sabababu mfumo tulionao unaendekeza Patronage!!
 
Waziri na bodi kama paka na panya vile sasa hivi hata barua hazijibiwi
 
Nadhani kuna moto mkali sana kati ya CEO,wafanyakazi,DAWASA na Wizara ya maji.Na tatizo ni mfumo mzima ni mbovu sana ndio unaoleta matatizo.
 
Nadhani kuna moto mkali sana kati ya CEO,wafanyakazi,DAWASA na Wizara ya maji.Na tatizo ni mfumo mzima ni mbovu sana ndio unaoleta matatizo.

Umefika wakati sasa utaratibu unahitaji kubadilishwa, hata kama nafasi za bodi zinatangazwa na watu kuomba kuna uhakika gani kuwa wanaoomba ndio wanaopata?. Na hii sheria inayompa nguvu waziri kuteua wajumbe wa Bodi , mwenyekiti na CEO , Wa taasisi husika imefutwa? Pamoja na kuwa Kwenye taasisi ya Elimu ya juu kunahundwa search Commitees lakini ni kweli kwamba hizi commitees ziko independent? na nani anaziunda?
 

Kwani mkataba wake ulikuwa wa muda gani?hivi wananchi watakuwa wamekosa vya kufanya mpaka kuandamana kwa ajili ya mtu ambaye ameshindwa kuwaweka sawa wafanyakazi waliochini yake?

Suala ni je utaratibu wa mchakato wa kumpata CEO mpya ulifuatwa na bodi?wizara?
 
Game Theory na Mzee Mwanakijiji, hebu fanyieni kazi ajira ya MD/CEO wa Benki ya Posta baada ya kutangazwa nafasi hiyo, maana huyu mnyalu anayeondoka tayari kamtayarisha kijana wake anaitwa Mkuba ili aendeleze ufidhuli na ufisadi na kumlindia maslahi yake. Huyu kijana kabebwabebwa kwa kuwa ndiye wakili wake katika kesi zake za viwanja na majumba anayonunua kwa aliowapa mikopo feki wakashindwa kurejesha, basi yeye Mnyalu ananunua nyumba zao zinapopigwa mnada. Wenye nyumba hizo wamekwenda mahakamani na Mkuba ndiye wakili wa kumtetea. Tunajiuliza ni kwa nini yeye ndiye anunue nyumba hizo ????????

Huyu dogo sasa hivi ni jeuri na anadharau kila mtu hata wakuu wa idara wenzake anajiona kama deputy/asst CEO. Kwa mtindo huu kweli waTZ tutafika na haya mashirika yetu ya umma !!!
 
Uanzishwaji wa DAWASCO, uteuzi wa Kaaya kuwa CEO tangu 2005 vyote vilifanyika kienyeji na Lowassa wakati huo akiwa Waziri wa Maji na Mifugo. Kasoro hiyo haikuwahi kurekebishwa hadi Lowasa anaondoka serikalini. Kwa namna Kaaya alivyopewa nafasi ile akawa na kiburi na jeuri ya hali juu. Akaliendesha shirika lile anavyotaka, akafukuza wafanyakazi wengi tu kwa visingizio kuwa ni wezi, hatimaye akaomba fedha nyingi serikalini akawapunguza wengi tu (zaidi ya 400). Akaanza kuajiri upya kwa mishahara mikubwa isiyoendana na hali ya shirika.
Sasa ameajiri karibu idadi sawa na wale aliowapunguza! Wizi uko palepale tena sasa unafanyika kisomi zaidi; amewagawa wafanyakazi kimatabaka. Wapya amewapa mishahara na maslahi bora zaidi kwa kuwa ni "watiifu" kwake. Kampuni ina hali mbaya sana kifedha na pengine isingekuwa ya serikali ingeshakabidhiwa kwa mfilisi.
Kwa kuwa usaili wa CEO mpya ulishafanyika watoe tu jina wanalolitaka.
 
Usilolijua ni kama usiku wa giza.Unaweza kuwa 50% right and 50% wrong!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…