Mchimbaji aula kwa kupata mawe ya Tanzanite ya thamani ya Tsh. Bilioni 7.8

Mchimbaji aula kwa kupata mawe ya Tanzanite ya thamani ya Tsh. Bilioni 7.8

Kama ni propaganda za kuita wawkezaji sioni tatizo
 
Habari wakuu,

Ninaona hili suala la Mmasai Leizer kupata madini 2 ya Tanzanite yenye thamani kubwa ya 7.8 billions ni kama propaganda fulani hivi.

Huenda ikawa ni white propaganda ya kuwaita wawekezaji wa nje au wa ndani kwenda kuwekeza kule Mererani.

Au ni propaganda yenye lengo fulani ambalo sisi hatulifahamu.

Anayemfahamu au kumjua vizuri Mr. Laizer atupe short of his life, maana isije ikawa ni mtu wa kitengo.
Usijifanye mjuzi kumbe Zero tu
Kila kitu wajuaji hata vitu vilivyo nje ya uwezo wenu kwenu sifa tu humu
 
Habari wakuu,

Ninaona hili suala la Mmasai Leizer kupata madini 2 ya Tanzanite yenye thamani kubwa ya 7.8 billions ni kama propaganda fulani hivi.

Huenda ikawa ni white propaganda ya kuwaita wawekezaji wa nje au wa ndani kwenda kuwekeza kule Mererani.

Au ni propaganda yenye lengo fulani ambalo sisi hatulifahamu.

Anayemfahamu au kumjua vizuri Mr. Laizer atupe short of his life, maana isije ikawa ni mtu wa kitengo.
Harufi ya propaganda kwa maana kwamba Leizer kaandaliwa na hayo mawe mawili yameandaliwa kwa ajili ya show off? kwa maana nyigne unamaanisha hayo mawe hayapo??

Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
 
Watu wakisikia mchimbaji mdogo wanafikiri ni masikini wakutupwa!

Kakuambia hajui cha kufanya na hizo pesa?
 

Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila amesema kuwa leo wizara inamtabua mchimbaji mdogo wa madini ya Tanzanite, Saninniu Laizer kuwa bilionea baada ya kupata mawe makubwa mawili yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8.

Mchimbaji huyo amepata mawe hayo mawili ambapo moja lina kilo 9.2 ambalo thamani yake ni shilingi bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.

“Na utofauti wake ni kwamba mawe ya uzito huo hayajawahi kupatikana kwenye machimbo ya Tanzanite tangu machimbo yaanze na yamepatikana ndani ya ukuta wa Mirereni kwahiyo hii ni rekodi mpya ya kupata mawe yenye uzito huo,” amesema Prof. Msanjila.

Profesa Msanjila amesema kuwa sekta ya madini inauwezo wa kumfanya mtu kuwa bilionea kwa haraka, ameongeza kuwa kunahitaji kuwa uwekezaji wa dhati katika sekta hiyo.

Serikali imenunua mawe hayo kutoka kwa mchimbaji huyo na yatawekwa katika makumbusho ya taifa
Ole Laizer, ubarikiwe sana na Bwana, na azidi kukuzidishia!
 
Kuna mwana yupo kule anasema kwenye huo mgodi kuna raia wamekula mil 200 wengine mil 70- mil 150 yaani waliokuwepo huko chini hakuna aliyetoka mtupu kila mmoja kapiga pande yake.
dah..hongera kwao
 
Hivi askari wakigundua una mzigo wa namna hiyo wanakuacha kweli?
Akiwa Shimoni alipiga Simu kwa Maofisa wa Wizara ya Madini wakaja kuliona wakalibeba na kwenda nae kwenye office zao....

Kama ingekua Askari ingekuwa HABARI ingine...
 
Akiwa Shimoni alipiga Simu kwa Maofisa wa Wizara ya Madini wakaja kuliona wakalibeba na kwenda nae kwenye office zao....

Kama ingekua Askari ingekuwa HABARI ingine...
Kumbe yuko smart, maaskari hawakawii kukumwagia njugu na kusema ni jambazi
 
Dhana ya kuweka mawe hayo makumbusho yanaleta faida gani?
 
Dhana ya kuweka mawe hayo makumbusho yanaleta faida gani?
 
Serikali ilimsaidia kulisha wale wana apollo sio?
Mng'ato, hebu fuatilia sualala huyu mchimbaji mdogo na namna alivyo - hustle for nine years hadi alipotoboa juzi! Huna haja ya kusaidiwa na Serikali pale unapoweza, ila pale parefu then kuna haja ya mkono wa Serikali. Hilo la kulisha wana Apolo wake ameliweza ndio chanzo cha hayo mafanikio. Ila itakapokuja kwenye uwekezaji MZITO wa huyu mchimbaji mdogo, nashauri yeye aihusishe Serikali ili imusaidie.
 
hongera kubwa kwake...sasa walio karibu naye wamshauri aajiri wataalamu wabobezi wa maswala ya biashara na uchumi ili wamshauri na kumsimamia namna sahihi ya kuwekeza ili abaki kuwa juu yeye na kizazi chake forever.
 
Back
Top Bottom