Mchina jela miezi mitano kwa kuua tembo 511, Mtanzania jela miaka 60 kwa kukutwa na meno ya tembo na kiboko

Kuua tembo 511 kama ni kweli, ni uhalifu wa kutisha. Ni kama mauaji ya kimbari (genocide). Wachina ni hatari!
CCM wanataka kuwapa Bandari ya Bagamoyo wangechota wanyama wetu wote na ndege na Samaki.
 
Umesahau maneno ya Mama Samia kwa Mr Peter alivyompeleka kwenye lile Godown la hayo mapembe? Serikali haipendi kuyakamata maana haitaweza kuyauza.

Mchina anajua soko kuliko huyo mmatumbi. Mchina ana Yuen na dolari wakati mmatumbi ana msimbazi. Inshort aliyehukumu na waliohukumiwa wamekula kwa urefu wa kamba zao
 
CCM wanataka kuwapa Bandari ya Bagamoyo wangechota wanyama wetu wote na ndege na Samaki.
Na unaambiwa wakishapewa utakiwi kutia mguu pale wala jicho aisee sio poa hii nchi ni ngumu sana
 
Huyu DDP kawekwa pale ili kuwaachia huru watuhumiwa wa ufisadi na uhujumu uchumi na majangiri tu, lakini chakushangaza wanyoge hawajawi kuwafutia kesi ata mara moja, kuna Mwalimu kafungwa jela kwa kosa la rushwa ya elf 50, Huyu Mama Samia anajifanya ana huruma kwa matajiri tu, yeye kama ana roho ya huruma basi amwambie DDP awafutie kesi na masiki na siyo kuwafutia kesi Matajiri tu, hii Zambi ya kuonea masikini itamtafuna tu ipo siku, anajifanya ana huruma kumbe uongo, kama kweli ameamua kumsamehe watuhumiwa basi na watanzania wa kipato chanini amwambie huyo DDP fisadi waachie Watanzania wakawaida kama anavyo waachia wafanyabishara kubwa wenye makosa makubwa.
 

Imenipa uchungu na hasira.
 
Hakuna haki kama huna pesa mkuu
 
Reactions: K11
Mama mjane afungwa miaka 22 kwa kukutwa na nyama ya swala
 
Sheria zinasemaje ?

Mara nyingine kuna technicalities nyingi ambazo zinatengeneza loopholes za wenye rupia kuweza kupenyeza kwenye udhia...

Huenda kukutwa na nyara ni kosa kubwa kuliko kuua nyara...
Mchina kwenyw Uhujumu Uchumia kaomba PLEA BARGAIN mzee.

Katokea hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…