Mchina kortini kwa meno ya fisi

mahakama ya kazi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2013
Posts
1,520
Reaction score
241
Raia wa China,Xu Wenze (29) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Wilaya ya Mpanda akikabiliwa na tuhuma za kukamatwa na meno matatu ya fisi.Mwendesha mashitaka wa hifadhi ya wanyamapori ya mbuga ya Taifa ya Katavi,Pele Malima,alidai mbele ya hakimu mkazi Mfawidhi Chiganga Tengwa kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo januari 3 mwaka huu,majira ya saa 6 mchana.Alidai raia huyo wa China ambaye anatengeneza barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda kuelekea Sitalike,alikamatwa na meno hayo matatu wakati akiwa kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda muda mfupi kabda ya kupanda ndege kuelekea mjini Mwanza.Mtuhumiwa alikana mashitaka na yuko nje kwa dhamana ya shilingi milioni tano.Kesi itatajwa Aprili mwaka huu.
source;gazeti la tanzania daima.

ILA WADAU HIZI KAMPUNI ZA BARABARA ZINAIBA SANA MALIASILI ZA TANZANIA.
 

tuambiane kama meno ya fisi nayo dili watu tujipe ajira binafsi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…