Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
Cartoonist Oppter John Fwema anashikiliwa na polisi kituo cha Oysterbay. Nimeongea na mdogo wake na amenambia kuwa Oppter alikamatwa nyumbani kwake Bunju siku ya Ijumaa tarehe 3 September 2021kwa makosa ya mtandao. Taarifa zaidi zinaendelea kupatikana Polisi na kwa familia na tutajuzana zaidi.
Oppter anafahamika kwa katuni zake zenye ujumbe wa kukosoa serikali.
Mchoro wa Katuni uliomuingiza matatani
Ukurasa wake wa Instagram
=≈========UPDATE==========
Polisi wamezuia dhamana yake. Kwa mujibu wa ndugu na jamaa wanaofuatilia wamenijuza kuwa
Wanasheria nguli wamejitokeza kufuatilia sakata la msanii huyu.
Inawezekana uwepo wa wanasheria ukapelekea haki kutendeka bila kukiuka haki za mtuhumiwa.
Nitaendelea kuwajuza zaidi kadiri taarifa sahihi zinavyopatikana
===≈====== UPDATE ==========
02/10/2021
Mpaka naandika ujumbe huu, ndugu wanasema kesi imeshikiliwa na RCO, tangu amekamatwa hakuchukuliwa maelezo ambapo amehojiwa Alhamisi wiki hii.
Wanasheria wameshajitokeza kufuatilia haki za mchoraji huyu wa vibonzo.
===≈====== UPDATE ==========
04/10/2021
Wakili Msomi Jebra Kambole amejitolea kushughulikia suala la Mchoraji Optter Fwema.
Ameshawasiliana na ndugu wa mshikiliwa kwa ajili ya taratibu za kisheria.
Mashirika na majukwaa ya kimataifa wameanza kufuatilia na kuanzia leo sauti zitapazwa.
Wakili kutoka THRDC alikuwepo kituo cha polisi akaonana na mpelelezi wa kesi na Msanii Optter.
Polisi wamesita kumpa dhamana leo, wanasema faili limepelekwa kwa state attonery kisha kesho watampeleka mahakamani.
Msukumo wa kijamii umesaidia kiasi kikubwa kwenye hili kwa sababu hapo awali polisi waligoma kutoa ushirikiano na kingine hawakutaka jamii ijue anashikiliwa.
-------------SAHIHISHO------------
Watu wengi wanamfananisha mchoraji Optter na mwanavibonzo mwingine aitwaye Fredy ambaye alitumia sana kalamu yake kuwachora upinzani wakati wa uchaguzi
PIA, SOMA:
- Mchora katuni Oppter afutiwa kesi, akamatwa tena na polisi
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
Oppter anafahamika kwa katuni zake zenye ujumbe wa kukosoa serikali.
Mchoro wa Katuni uliomuingiza matatani
Ukurasa wake wa Instagram
=≈========UPDATE==========
Polisi wamezuia dhamana yake. Kwa mujibu wa ndugu na jamaa wanaofuatilia wamenijuza kuwa
Wanasheria nguli wamejitokeza kufuatilia sakata la msanii huyu.
Inawezekana uwepo wa wanasheria ukapelekea haki kutendeka bila kukiuka haki za mtuhumiwa.
Nitaendelea kuwajuza zaidi kadiri taarifa sahihi zinavyopatikana
===≈====== UPDATE ==========
02/10/2021
Mpaka naandika ujumbe huu, ndugu wanasema kesi imeshikiliwa na RCO, tangu amekamatwa hakuchukuliwa maelezo ambapo amehojiwa Alhamisi wiki hii.
Wanasheria wameshajitokeza kufuatilia haki za mchoraji huyu wa vibonzo.
===≈====== UPDATE ==========
04/10/2021
Wakili Msomi Jebra Kambole amejitolea kushughulikia suala la Mchoraji Optter Fwema.
Ameshawasiliana na ndugu wa mshikiliwa kwa ajili ya taratibu za kisheria.
Mashirika na majukwaa ya kimataifa wameanza kufuatilia na kuanzia leo sauti zitapazwa.
Wakili kutoka THRDC alikuwepo kituo cha polisi akaonana na mpelelezi wa kesi na Msanii Optter.
Polisi wamesita kumpa dhamana leo, wanasema faili limepelekwa kwa state attonery kisha kesho watampeleka mahakamani.
Msukumo wa kijamii umesaidia kiasi kikubwa kwenye hili kwa sababu hapo awali polisi waligoma kutoa ushirikiano na kingine hawakutaka jamii ijue anashikiliwa.
-------------SAHIHISHO------------
Watu wengi wanamfananisha mchoraji Optter na mwanavibonzo mwingine aitwaye Fredy ambaye alitumia sana kalamu yake kuwachora upinzani wakati wa uchaguzi
PIA, SOMA:
- Mchora katuni Oppter afutiwa kesi, akamatwa tena na polisi
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
- Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea siku 10 na hajulikani alipo
- Mhariri Mtendaji wa Gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea avamiwa na kumwagiwa tindikali akiwa ofisini kwake
- Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
- Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa
- Mwanahabari Erick Kabendera akamatwa na Polisi nyumbani kwake; yadaiwa anaendelea na Mahojiano
- Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi
- Mwandishi wa Mwananchi Jesse Mikofu ashambuliwa na askari akitekeleza majukumu yake
- Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma