Mchujo TFF:Ali Mayai apeta,Malinzi afungaishe

Mchujo TFF:Ali Mayai apeta,Malinzi afungaishe

MCHUJO UCHAGUZI MKUU TFF

Wakati majina 73 yakipita katika hatua ya awali,mgombea tishio Ali Mayai amepita kihunzi hicho. Mwanasoka Ali Mayai wamekuwa akiiundiwa mazengwe na timu ya fitna ya Malinzi ambayo imekosa sababu za kuendelea uongozini.

Kamati ya Uchaguzi ya TFF imechuja jina la Abdallah Mussa katika orodha ya wagombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao wa shirikisho. Sababu za kukata jina la Mussa ambaye alikuwa anawania nafasi ya Ujumbe kutoka Kanda Na. 1 ya mikoa ya Kagera na Geita ni kutoambatanisha kivuli cha cheti cha kidato cha nne kwa mujibu wa kanuni ya 9 inayozungumzia sifa nane za kuwania uongozi TFF. Katika majina hayo 73, majina 10 ni wale wanaowania urais, makamu rais sita na wajumbe wa kamati ya utendaji 57.

Wagombea wote hapo juu wanatakiwa kufika kwenye usaili utakaofanyika kuanzia Juni 29, 2017 hadi Julai 1, mwaka huu katika ofisi za TFF Karume, Dar es Salaam kuanzia saa 4.00 asubuhi wakiwa na nyaraka halisi za viambatisho vyote walivyoweka kwenye fomu za maombi. Vyeti vya elimu ya Sekondari viwe vya Baraza la Mitihani (NECTA


SUMU YA MALINZI HAIWEZI MWACHA MTU SALAMA HATA MAYAI ANAJUA ANASINDIKIZA
 
Malinzi hana sifa zakuendelea kuwa rais wa tff.apishe wengine tuu.
 
Ningependa Mayay awe rais...ila naogopa sana akishindwa leta maendeleo maana ninamuelewa sana jamaa.Asije tu kuwa nae anaongozwa na njaa
 
Ningependa Mayay awe rais...ila naogopa sana akishindwa leta maendeleo maana ninamuelewa sana jamaa.Asije tu kuwa nae anaongozwa na njaa
Akishindwa kuleta maendeleo tunamtupilia mbali.

Tanzania tunavichwa karibia 50 millions.
 
Ningependa Mayay awe rais...ila naogopa sana akishindwa leta maendeleo maana ninamuelewa sana jamaa.Asije tu kuwa nae anaongozwa na njaa
Anashinda asubuhi kweupe. Msiwasikilize hawa watu humu ambao njaa zimehamia kichwani. Yaani kweli mpenda soka unamtetea malinzi!!!!!!!
 
Anashinda asubuhi kweupe. Msiwasikilize hawa watu humu ambao njaa zimehamia kichwani. Yaani kweli mpenda soka unamtetea malinzi!!!!!!!
Nyie ndio mna njaa mpaka imewatia upofu na unafiki kwa kutokuona mambo mazuri ya Malinzi.

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom