Mchungaji amuua mkewe naye kujiua wakati Ibada ikiendelea

Mchungaji amuua mkewe naye kujiua wakati Ibada ikiendelea

Naona watu hapa kwenye huu uzi wanafanya utani na kebehi tu kisa muonekano wa kanisa au jambo lilivyotokea, nadhani baada ya hayo tuzidi kujikita ndani katika kujiimarisha kwenye afya ya akili zetu. Kwanza fikra madhubuti, mawazo ya msingi na kujenga uhusiano mwema na jamii husika. Yaliyowakuta hawa wanandoa hatujui bado ila binadamu tunapitia mambo mengi mno na tunapaswa kuwa na nguvu ya kuyatatua bila kujenga majeraha au madhara makubwa kama haya ya kifo. Mchungaji hakuwa mwendawazimu mpaka kuyaandika wazi kitakacho mfikisha kufanya alichofanya kwa mkewe na kwake binafsi, sio jambo jema kabisa alilotenda ila liwe somo na onyo kwetu tunaoendelea kupata pumzi ya bure ya Mwenyezi Mungu.

NB: Dunia ya sasa ni chafu sana, utacheka hapa ila kesho jambo la aibu na ajabu linaweza kukukaribia. Chukua hatua!
 
Lakini si ni mfuasi wa yesu?

Waumini wake watajibu
Mimi sio upande huo [emoji3064]
Nilijibu hivyo kwa sababu najua wanavyotetea ujinga na kuhamisha mjadala ukiwa upande huo

Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Huyo hakuwa mchungaji bali makamata fursa. Inawezekana walitofautiana jinsi ya kutumia sadaka na mafungu ya kumi.
La hasha. Nadhani mke wake ndiye alikuwa mkarimu sana. Anagawa mali ya mchungaji kwa kijiji kizima.
 
Mhubiri amuua mkewe wakati wa ibada

JUMAPILI, 5TH JAN , 2020

Mhubiri Elisha Misiko wa kanisa la Ground for Jesus, lililoko mjini Mombasa nchini Kenya, amemuua mke wake kwa kumchoma na kisu na kisha yeye kujikata koo lake na kufariki papo hapo, wakati wa ibada ya Jumapili ikiendelea kanisani hapo.

Tukio hilo lilitokea Januari 5, 2020, ambapo kwa mujibu wa waumini wa kanisa hilo wamesema kuwa mhubiri huyo alitekeleza unyama huo kwa haraka sana na kwamba juhudi za kuwanusuru wawili hao hazikuzaa matunda.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa eneo la Kisauni, Julius Kiragu, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea majira ya saa 4:00 asubuhi ya leo na kwamba Jeshi la Polisi mjini Mombasa, limekwishaanza kufanya uchunguzi ili kubaini nini chanzo kilichopelekea mume kumuua mkewe na kisha yeye naye kujikata koromeo.

Aidha Kamanda Kiragu amesema kuwa ndani ya mfuko wa suruali wa mhubiri huyo wakati wakiondoa mwili wake na kuupeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti, wamekuta barua yenye kurasa 17, iliyokuwa ikieleza chanzo cha mauaji hayo kuwa ni migogoro ya kifamilia.
 
Back
Top Bottom