Mchungaji atishia kuwafukuza waumini wake watakaokataa kutuma sadaka kwa Mpesa kila Jumapili

Zero Hours

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
12,942
Reaction score
18,669
Mchungaji James Ng'ang'a wa nchini Kenya, anetishia kuwafukuza waumini wake watakaokataa kutuma sadaka kila jumapili kwa njia ya Mpesa.

Mchungaji aliamua kuanzisha ibada zake zinazooneshwa live kupitia Facebook baada ya Nchi kuwa katika lockdown.

Aliwataka waumini kuwa wawe wanatua kiwango kinachoanzia 1,000Ksh, ambayo ni sawa na 20,000Tsh kila jumapili wanapokuwa wakifanya ibada live kutumia mtandao wa facebook.

Mchungaji aliwaambia waumini wake kuwa Janga la corona lisiwe sababu ya kushindwa kutoa sadaka. Atakayekaidi asikanyage tena kanisani kwake.
 
Na wanao sali hapo akili wanazo mhh[emoji848]
Sent using Jamii Forums mobile app
 
'General Commander Pastor James Ng'ang'a' safi sana hii nimeipenda ila hata hapa bongo kuna baadhi ya madhehebu japo hayasemi wazi au kulazimisha watu but mfumo ndiyo huohuo, kama hutoi -hupewi huduma yoyote.
 
😁😁😁walokole wanavituko jaman
 
Mchungaji vyuma vya Korona vinazidi kukaza pamoja na kutumia mitandao kuwakamua kondoo wake. Hela ya kula kwa sasa ni shida, hiyo ya sadaka wataitoa wapi?
 
Naapa, wachungaji hawa ndio kichocheo kikubwa cha korona.

Hawakujali roho za waamini wao, hawakuweza kumshauri Mheshimiwa kuhusu huu ugonjwa.

Wanataka sadaka tu.

Sitaaenda huko kanisani mpaka kiieleweke.

Mungu atete na hao wachungaji wa kundi lake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulokole ni ulevi mmoja mbaya sana, hapo utashangaa waumini wanavyohangaika kutuma hiyo sadaka ili wasifukuzwe kanisani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…