Mchungaji azomewa kwa kuwapendelea warembo

Mchungaji azomewa kwa kuwapendelea warembo

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564
Kisanga kilitokea katika kanisa moja eneo la Buchinga baada ya majamaa kufokea vikali mtumishi wa Mungu kwa madai alikuwa akiwapendelea akina dada katika mahubiri yake.

Mdakuzi alisema kwamba, mara kwa mara, mchungaji alikuwa akiwapendelea sana wanawake wakati akitoa mafunzo yake kanisani jambo ambalo liliwaudhi wanaume.



Kwa mujiibu wa Taifa leo, mabarobaro hao waliamua kumkabili pasta kudhihirisha gadhabu yao.

Siku ya kisanga, mtumishi alisimama kwenye madhabahu kama ilivyokuwa ada na kuanza kuwalisha kondoo wake neno.

Inaarifiwa kuwa baada ya kunukuu kifungu cha Bibilia, mchngaji huyo alianza moja kwa moja kuwadhalalisha majamaa.

“Wasichana ninataka kuzungumza nanyi. Mungu anawapenda sana. Endeleeni kumheshimu Mungu naye atawatimizia matamanio ya mioyo yenu,” pasta alihubiri.


Baada ya kuwapa himizo hilo na kuwatia moyo warembo aliwageukia wanaume.

“Ninataka wanaume wote ambao hawajapata jiko wanisikilize kwa makini. Kila siku mnakuja hapa kunitazama tu. Mungu amekataa kuwabariki kwa sababu hamjui kuomba,” pasta aliwafokea.

Semasema zinaarifu kwamba mabarobaro waliangaliana kisha wakasimama wote kwa pamoja na kuwaka moto.

“Kama hatujui kuomba mbona hutaki kutufunza,” sauti ya lofa mmoja ilisikika ikisema.

Vicheko vilisikika kote kanisani lakini pasta alishikilia neno kwamba mwaka huu ni mwaka wa urejesho kwa akina dada,” pasta aliendelea kusema.

Penyenye zinasema kwamba mapolo walipandwa na hasira na kuanza kumfokea pasta.

“Kwenda huko. Umetudharau sana kwa muda mrefu. Tumechoka na hizo kejeli zako,” walisema huku pasta akitokwa na kijasho jembamba.

“Mahubiri yako yamejaa mapendeleo na madharau mengi sana. Unawapendelea warembo sana sijui wana nini ambacho sisi hatuwezi kukupa,” polo mmoja alimzomea pasta.

Mdaku alisea pasta aliingia baridi na kutamani ardhi ipasuke immeze mzima mzima.

“Koma hiyo tabia ama tuhame kanisa,” makalameni walionya na kuketi chini huku pasta akibadilisha mahubiri.

Inasemekana baada ya ibada aliwaita makalameni kwa mkutano na kuwaomba msamaha akisema hakuwa na nia mbaya kwao.






[emoji2398]TaifaLeo
 
Back
Top Bottom