Mchungaji Gwajima amejibu tuhuma za mume wa Flora Mbasha?

Mchungaji Gwajima amejibu tuhuma za mume wa Flora Mbasha?

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
Mume wa Flora Mbasha katikat ya mwaka huu baada ya kutifuana na mkewe alimnyoshea kidole Mchungaji Gwajima kuhusika na mkasa katika ndoa yake na mkewe Flora. Tuhuma nzito zilielekezwa kwa Mchungaji huyo anayejulikana Tanzania kwa kukusanya umati mkubwa wa watu katika mikutano yake.

Tuhuma nzito zaidi zilizoelekezwa kwake kama nukuru ya barua hiyo hapo chini zinazoonekana kuwa na uzito wa juu ni:

  1. Mchungaji Gwajima kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Flora Mbasha (mke wa mtu).
  2. Mchangaji huyo kuhusishwa tuhuma za biashara ya kuuza unga.
  3. Kumkingia kifua Flora na kutaka kumfungulia mashtaka mume wake anayelalamika kuibiwa mke wake.
Kwa vile mchungaji ni public figure, na kadiri ya maadili ya utume wake alipaswa kutolea ufafanuzi na kujenga utetezi kuwaondolea dukuduku waumini (kondoo) wake na ulimwengu.

Je hilo mchungaji Gwajima amelifanya?


images
603607_893381404009686_3101986341740654157_n.jpg
images



Hii barua ya Mume wa Mwimbaji wa Nyimbo za injili nchini - Flora Mbasha kwenda kwa mchungaji maarufu nchini, Mchungaji Gwajima inakuhusu....
"Mchungaji ...yapata kama wiki mbili zilizopita nilihoji kupitia vyombo vya habari juu ya ‘utajiri' wa ghafla wa mkewangu Mara baada ya mgogoro kutokea kati yangu na yeye, bila kupoteza muda mkewangu akanijibu kupitia gazeti moja la udaku kuwa amechangiwa fedha kiasi cha milioni 9 na waumini kanisani kwakoMchungaji, naomba uelewe kuwa nafahamu juu ya mipango yote mnayoipanga kuliko unavyodhani!!

Kwanza ni kweli kuwa mlipitisha harambee ya kumchangia mkewangu, lakini kiwango kilichopatikana kilikuwa ni milioni 2 na laki tatu na si milioni tisa kama mlivyotangaza!! Lakini mlitangaza uongo huo makusudi iwe rahisi kutimiza malengo yenu ya kidhalimu mliyoyapanga juu yangu!!Mnamo tarehe 3 mwezi juni mwaka huu, mlifungua akaunti mpya kwa jina la mkewangu katika benki ya crdb morogoro, na siku nne baadae mkewangu aliingiziwa fedha kiasi cha milioni 18 kutoka akaunti ya MWANAMAPINDUZI FOUNDATION ambayo hyo accnt ipo nmb mwanza! Ambapo asasi hii inamilikiwa na mchungaji wako msaidizi Maximilian Machumu pamoja na mbunge wa viti maalumu kutoka mikoa ya kaskazini!


Nashukuru kama ulimpa fedha hizi kwa nia ya kumsaidia, lakini hofu yangu ni kuwa kwanini kitendo hiki kifanyike kwa kificho?? Kwanini mtumie njia za siri ambazo si rahisi watu kujua kama mmempa fedha??


Pia napatwa na mashaka zaidi kwani siku moja baada ya fedha hizi kuingizwa taarifa ya benki inaonyesha kuwa kiasi cha milioni sita cash zilitolewa na siku hiyo hiyo wapo waandishi watatu wa magazeti ya udaku ambao wanaonekana waliingiziwa fedha kiasi cha milioni moja kila mtu na aliyedeposit hizo fedha ni moja ya viongozi wako hapo kanisani!! Kuna nini hapo??

Mchungaji, naomba tusizunguke mbuyu! Ni dhahiri shahiri kuwa umekuwa na uhusiano wenye utata na mkewangu kwa muda mrefu sasa!

Binafsi nilianza kupata wasiwasi mwaka jana mwezi desemba tulipoenda katika mkutano wako wa injili pale morogoro! Mimi na mkewangu tulifikia hoteli ya kingsway msamvu na wewe ulifikia Nashera Hotel maeneo ya forest hill!!

Baada ya siku tatu za mahubiri mkutano wako ulipigwa marufuku na serikali kwasababu ya maneno yakichochezi uliyokuwa unahubiri, hvyo ikatulazimu waimbaji wote turejee dar es salaam!!

Lakini uliniomba mkewangu abaki na wewe kwani ulipanga uwe unawafanyia watu maombi pale kanisani kwako kihonda kwa muda wa siku nne!! Nilikubali na nikamuacha mkewangu nyumbani kwa dada yako pale mazimbu!! Lakini kesho yake dada yako alisafiri kwenda mwanza na ikabidi mkewangu arudi hotelini kingsway!!


Kwaa taarifa nilizonazo na nimezithibitisha kupitia wahudumu wa pale hotelini ni kuwa mkewangu hakuwahi kulala pale hata siku moja ingawa chumba kililipiwa kwa siku zote zile!! Unaweza kunijibu alikuwa analala wapi?? Je unaweza kunieleza kwanini mkewangu alikuwa analetwa nashera hoteli na taxi kila siku usiku!! Sibahatishi katika hili kwani hata namba ya dereva taxi ninayo!!

Yote haya nilivumilia, na hapa kati kati kuna mengi sana yametokea lakini nikajifanya mjinga nikajishusha nikavumilia kwa lengo la kulinda ndoa yangu isiharibike lakini naona wenzangu hambadiliki wala hamjishitukii sana sana mapenzi ndio yanzidi kuwa motomoto kati yenu!! Ulikuwa unategemea nivumilie mpaka lini, nijishushe kiasi gani, niwe mjinga kiasi gani Nilikuvumilia sana mchungaji lakini sasa imefika point hapana, imetosha lazima nikuondelee uvivu watanzania na dunia ikufahamu jinsi ulivyo na kitendo ulichonifanyaia na unataka kuniziba mdomo kwa kunitishia jela miaka 30!!!


Wewe ni mpuuzi na shetani anaishi ndani yako... na nataka nikuahidi kitu kimoja kuwa NITAKUSHINDA! Najua utanisumbua sana kutokana na hela zako but at the end, I will be the last man standing!! Narudia tena, nitakushinda.!!
Bila kusahau naomba niongee na wewe pia mkewangu, hivi ni nini kilichokukuta ndani ya moyo wako How did we get here?? Je ni fedha zilizokufanya ukengeuke kiasi hicho au kuna kingine??

Kama unanichukia mimi kiasi hiki je, uwahurumii hata watoto wetu?? Mbona tunawatengenezea mikosi wakiwa wadogo hivi?? Hivi unadhani watoto wanajisikiaje watakaposikia kuwa baba ameenda jela kwa kosa la kubaka lakini aliyechongesha muvi yote hiyo ni mama?? Hivi kisaikolojia hawa watoto watakuwaje Si watakuwa huku wanatuchukia sisi wote wawili kwa aibu na mikosi hii tunayowatengenezea Kwanini tunataka kuwataabisha watoto kwa dhambi ambayo hawajaitenda

Yes nafahamu nimekukosea mengi and am very sory for that, lakini basi embu kumbuka mkewangu nimekuvumilia mambo mangapi mkewangu, kumbuka makosa mazito uliyonifanyia lakini nikakusamehe ni sijamsimulia hata ndugu yako ama ndugu yangu ili kulinda heshima yako!! Kumbuka jinsi tulivyopogana na changamoto mbalimbali mpaka leo hii umefikia kuwa moja ya icons wa muziki wa injili hapa nchini?? Kumbuka shida, manyanyaso, dhuluma, kuchekwa na kudharauliwa ambako tumepitia mpaka leo hii tuko hapa!!!


Mkewangu, kwa miaka yote hii nimekubali nionekane bushoke tu huku watu hawajui kuwa mimi ndiye ninayechora ramani ya kila ishu yako!! Mimi ndiye nimekuwa nafatilia na kufanikisha kila kitu chako from scratch!!!

Lakini nimekubali jamii inione bushoke kwani nilikuwa najua nini mimi na wewe tunatengeneza kwa maisha yetu ya sasa na baadae!!! Nini kilichokubadilisha mkewangu Fedha Au huyo mchungaji mwanamazingaombwe
Hivi kweli kabisa umefikia hatua ya kulipa waandishi wa habari ili wanikandamize nionekane sifai katika jamii Ni nini kilichokuoata mkewangu??

Naomba uelewe kuwa binafsi siogopi kwenda jela kwasababu ya hiyo muvi mliyonizushia, kwani ni bora nikakae jela kuliko kuishi huru huku mkininyanyasa kiasi cha kuondoa utu wangu kama bidamu, lakini kinachoniuma ni familia yetu!! Kwanini watoto wateseke kwa sababu ya tamaa zetu binafsi!! Nikifikiria hilo naumia sana!

Najua kwa sasa inaonekana kama vile ni impossible kwa mimi na wewe kurudiana tena, lakini binafsi naamini tunaweza!! Najua haitakuwa rahisi kwani tumeharibu mno, lakini ni heri ya kujaribu kuliko kuendelea kufanya huu upuuzi tunoufanya sasa!!

Kumbuka hiki tunachokifanya sasa hatujajipaka matope sisi tu pekee, bali mziki wote wa injili Tanzania, na tusipotubu tukajirudi Mungu atatuhukumu kwa dhambi hii!!

Kumbuka kuwa hakuna kati yenu atakayeshinda katika hii vita, vyombo vya habari pekee ndivyo vitakavyo nufaika lakini mimi, wewe na mchungaji wote tuta loose!!

Mwisho nimalizie na wewe mchungaji, tulipokutana mara ya kwanza nilikuchukulia kama kaka na kama mlezi wetu wa kiroho!! Lakini umegeuka shetani mwenye pembe saba, umeparaganyisha familia yangu, umeleta maumivu makali kwenye ukoo!!


Nakuonya tena kwa mara nyingine, muache mkewangu!! Huyo ni mkewangu, nilimtolea mahali mimi mwenyewe na wazazi wake waliniamini na kunikabidhi!!! Nasema niachie mkewangu!!

Wewe ni nyoka, imefika time watanzania wakujue ukweli wako wewe mbwa mwitu mkali uliyevaa ngozi ya kondoo!!!

Umedanganya watu vya kutosha na umefarakanisha ndoa nyingi sana kwa sababu ya kiburi cha pesa zako chafu za sembe!! Umeudhalilisha ulokole kiasi cha kutosha imefika time tuwaeleze watanzania ukweli na wakufahamu kuwa wewe ni nyoka!!

Sitakubali kuona ukiendelea kuitesa familia yangu, nitapambana na nitakushinda!!! Siogopi fedha zako wala connection ulizonazo, ni bora nife nikiwa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti!

Nitapambana na wewe mpaka mwisho ili historia isomeke vizuri ili hata wanangu wakiwa wakubwa wajue kuwa baba yao sikuwa lofa kiasi cha kupiga magoti na kuelekeza shingo kibla kuruhusu mdhalimu kama wewe uichinje familia yangu, bali licha ya umasikini wangu nilisimama kiume na kupigana kutetea familia yangu!!!
Narudia tena mchungaji, nitapambana na nitakushinda.."
Kwako - Mchungaji Gwajima

 
Elimu ni ufunguo wa maisha.

Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa.

Ndoa haijengwi na wapambe, haisimami kwa nguvu wala vitisho.

Mbasha na washauri wake, including wewe muandika mada, mngekuwa na elimu ama ya duniani ama ya Mungu, msingeandika barua kama hii kwenye magazeti na kama haitoshi sasa mnaileta jamii forums. Huu ni ujinga.

Laiti kama Mbasha angelikuwa na Mungu, asingefuata ushauri wenu wapambe ambao badala ya kujenga upya mahusiano yake kwa maslahi ya familia, ndiyo mnazidi si kupanua nyufa bali kuangusha kuta kabisa.

Ninajua Ema na Flora walikotoka. Emma anaonyesha uchungu mkubwa sana na kwa barua hii, amekata tamaa na anajiona hana namna kama mfamaji. Laiti kama angelijua, asingewashirikisha ninyi mazandiki mnaozidi kumpa machungu. Ndoa haijengwi kwa shinikizo na wala haijengwi na nguvu zozote za nje ya wawili.

Huwezi kusema unampenda mke wako na unamhitaji arudi kwako kwa manipulations na ku mu embarrass. Hamwezi kujenga ndoa kwa sheria za jamii, lazima ama kuogopa aibu. Mnaanikamambo ya chumbani hadharani inabaki radha ya ndoa tena? Emma ameyakuza mwenyewe kwa kudhani ninyi mazabizabina mnamshauri vizuri!.

Kama mlitaka Mchungaji gwajima ajibu, kwa nini mlipeleka waraka huu gazetini wakati mnapafahamu anakopatikana? Huu ni wehu na ndiyo umewafanya ninyi mvunje ndoa ya Mbasha. Kwanza mnajuaje Gwajima alisoma hayo magazeti yenu au kama anasomaga hapa jamii forum?

Mnajichora ni namna gani hamna elimu ya darasani, hekima ya kurithi na maadili ya asili wala hamna hekima yaa Mungu ndani yenu. Mnaishi kwa mivumo ya kelele za upepo.

Nawapa tahadhari, huko mnakoelekea mnatafuta mauti. Shauri lenu, endeleeni na ujinga wenu.
 
Hivi ile kesi inaendeleaje au imefikia wapi kwa mlio na updates?
 
utajibu vipi mtu unayemchapia mkewe??

umaskini ni soo...
 
Elimu ni ufunguo wa maisha.

Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa.

Ndoa haijengwi na wapambe, haisimami kwa nguvu wala vitisho.

Mbasha na washauri wake, including wewe muandika mada, mngekuwa na elimu ama ya duniani ama ya Mungu, msingeandika barua kama hii kwenye magazeti na kama haitoshi sasa mnaileta jamii forums. Huu ni ujinga.

Laiti kama Mbasha angelikuwa na Mungu, asingefuata ushauri wenu wapambe ambao badala ya kujenga upya mahusiano yake kwa maslahi ya familia, ndiyo mnazidi si kupanua nyufa bali kuangusha kuta kabisa.

Ninajua Ema na Flora walikotoka. Emma anaonyesha uchungu mkubwa sana na kwa barua hii, amekata tamaa na anajiona hana namna kama mfamaji. Laiti kama angelijua, asingewashirikisha ninyi mazandiki mnaozidi kumpa machungu. Ndoa haijengwi kwa shinikizo na wala haijengwi na nguvu zozote za nje ya wawili.

Huwezi kusema unampenda mke wako na unamhitaji arudi kwako kwa manipulations na ku mu embarrass. Hamwezi kujenga ndoa kwa sheria za jamii, lazima ama kuogopa aibu. Mnaanikamambo ya chumbani hadharani inabaki radha ya ndoa tena? Emma ameyakuza mwenyewe kwa kudhani ninyi mazabizabina mnamshauri vizuri!.

Kama mlitaka Mchungaji gwajima ajibu, kwa nini mlipeleka waraka huu gazetini wakati mnapafahamu anakopatikana? Huu ni wehu na ndiyo umewafanya ninyi mvunje ndoa ya Mbasha. Kwanza mnajuaje Gwajima alisoma hayo magazeti yenu au kama anasomaga hapa jamii forum?

Mnajichora ni namna gani hamna elimu ya darasani, hekima ya kurithi na maadili ya asili wala hamna hekima yaa Mungu ndani yenu. Mnaishi kwa mivumo ya kelele za upepo.

Nawapa tahadhari, huko mnakoelekea mnatafuta mauti. Shauri lenu, endeleeni na ujinga wenu.

Makala kama hizi mnapeleka gazetini.mnatuchosha na maneno mengi point ni moja tu
 
Elimu ni ufunguo wa maisha.

Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa.

Ndoa haijengwi na wapambe, haisimami kwa nguvu wala vitisho.

Mbasha na washauri wake, including wewe muandika mada, mngekuwa na elimu ama ya duniani ama ya Mungu, msingeandika barua kama hii kwenye magazeti na kama haitoshi sasa mnaileta jamii forums. Huu ni ujinga.

Laiti kama Mbasha angelikuwa na Mungu, asingefuata ushauri wenu wapambe ambao badala ya kujenga upya mahusiano yake kwa maslahi ya familia, ndiyo mnazidi si kupanua nyufa bali kuangusha kuta kabisa.

Ninajua Ema na Flora walikotoka. Emma anaonyesha uchungu mkubwa sana na kwa barua hii, amekata tamaa na anajiona hana namna kama mfamaji. Laiti kama angelijua, asingewashirikisha ninyi mazandiki mnaozidi kumpa machungu. Ndoa haijengwi kwa shinikizo na wala haijengwi na nguvu zozote za nje ya wawili.

Huwezi kusema unampenda mke wako na unamhitaji arudi kwako kwa manipulations na ku mu embarrass. Hamwezi kujenga ndoa kwa sheria za jamii, lazima ama kuogopa aibu. Mnaanikamambo ya chumbani hadharani inabaki radha ya ndoa tena? Emma ameyakuza mwenyewe kwa kudhani ninyi mazabizabina mnamshauri vizuri!.

Kama mlitaka Mchungaji gwajima ajibu, kwa nini mlipeleka waraka huu gazetini wakati mnapafahamu anakopatikana? Huu ni wehu na ndiyo umewafanya ninyi mvunje ndoa ya Mbasha. Kwanza mnajuaje Gwajima alisoma hayo magazeti yenu au kama anasomaga hapa jamii forum?

Mnajichora ni namna gani hamna elimu ya darasani, hekima ya kurithi na maadili ya asili wala hamna hekima yaa Mungu ndani yenu. Mnaishi kwa mivumo ya kelele za upepo.

Nawapa tahadhari, huko mnakoelekea mnatafuta mauti. Shauri lenu, endeleeni na ujinga wenu.

Gwajima nimesema ni public figure, na kama amekuwa na unyofu wa moyo maungamo au kukanusha ni uanaume, lakini kunyamaza ni dalili kisaikolojia kukiri kosa bila kujutia na kuondoa wingu linazofunika ndoa ya wenyewe. Mchungaji kuhusishwa na tuhuma za matatizo ya wanandoa si jambo dogo, hawa ni kondoo wake anaowachunga.
 
Tunapata fursa ya kujifunza hapa,makanisa yanayoibuka kila kukicha ni makao ya shetani,acheni kuwaamin hawa wanaojiita manabii dhid ya wake zenu,hawa n nyoka wnye sumu kali,UKIONA MKE HAKUELEWI MPE GREEN LIGHT MAPEMA AKAOLEWE NA NABII,UBAK NA AMAM ROHONI.
 
Kunyamaza pia neno,huyo Mbasha angenyamaza akamuachia Mungu...........
 
Kunyamaza pia neno,huyo Mbasha angenyamaza akamuachia Mungu...........

Ndugu kukaa kimya kwa mambo ya namna hii ni kujiua polepole,ni bora aseme kuinusuru nafsi yake,then napata taabu zaidi na ukimya wa mchungaji Gwajima!!!kwa maelezo ya Emma nadhani Kuna elements za ukweli!!!
 
Ndugu kukaa kimya kwa mambo ya namna hii ni kujiua polepole,ni bora aseme kuinusuru nafsi yake,then napata taabu zaidi na ukimya wa mchungaji Gwajima!!!kwa maelezo ya Emma nadhani Kuna elements za ukweli!!!
sijui kwakeeli lakini ningekua mimi ningenyamaza tuu na chozi la mwenye kuonewa mwenye mungu hulipokea na ukizingatia ni mkewe hali wa ndoa,kama kweli ameonewa huyo Gwajima na mkewe hawato fumba jicho bila ukweli kujulikana........
 
Sasa hapa una mend ndoa ya Ema au unapigana na Gwajima? Maana hueleweki.

Gwajima hataki kuitikia mchezo wa kijinga unaotaka kumchezesha. Ana akili za kuu kuliko ninyi, kanyamaza kwa kuwa anaona kujibishan na watu wenye akili kama zenu ni kujidharirisha. Na ndoa ya Emma ndiyo hiyo mnazidi kuizika,kwa kudhani mnatumia akili kumbe ni makamasi.

Sasa mnafanya nini?? Acheni wehu!.

Hata kama ni mimi ningekuwa Gwajima, nisingejibizana na watu wenye kiwango cha chini kama chenu. Mnafanya fujo kama vibaka wa mahusiano? Mmekosa elimu hata ushauri wa wenye hekima hamna? Acheni upuuzi wenu huu.

Endeleeni kudanganyana, mwisho wake mtajutia nakwambia. Ninyi ndiio mmekuwa mawakala wa uharibifu kuliko kitu chochote.

MWAMBIENI EMA AWAELEZE, TATIZO LAKE NA FLORA LIMEANZA BAADA YA FLORA KWENDA KUSALI KWA GWAJIMA? MSITAKE KUMFANYA GWAJIMA MBUZI WA SHUGHULI, MKADHANI WOTE NI WAJINGA.



Gwajima nimesema ni public figure, na kama amekuwa na unyofu wa moyo maungamo au kukanusha ni uanaume, lakini kunyamaza ni dalili kisaikolojia kukiri kosa bila kujutia na kuondoa wingu linazofunika ndoa ya wenyewe. Mchungaji kuhusishwa na tuhuma za matatizo ya wanandoa si jambo dogo, hawa ni kondoo wake anaowachunga.
 
Mnalalamika Flora kwa nini apewe fedha na utajiri wa ghafla. Millioni 20 ni utajiri?

Kwa hiyo bila hizo fedha ndoa yao ingekuwa imara?

Tatizo ni pesa, ndoa ama Gwajima?

Msktake kutafuta sababu, tatizo la ndoa yao si la leo. Flora aliolewa na Ema akijua ni mtoto wa maskini hana kitu. Kama angelikuwa anatafuta pesa, kwa nini hakutafuta wenye nazo?

Gwajima alarundikiwa mzigo kwa kumpa financial confidence (kama ni kweli), Flora kitu ambacho nakiona kwe Emmanuel ni utashi (kama yalivyo madume mengi) kwa kulazimisha wanawake wakae kwenyehimaya yao kwa sababu ya economic dependency wala si mapenzi.

Mnataka kusema Flora kukaa na Mbasha bia mapenzi ila ni kwa kuwa hana namna ya kuishi, ndio uimara wa ndoa?

Acheni huo ujinga. Mmemharibia Emma ndoa yake kwa kumshauri vibaya na sasa itabidi mlinywe. Angepata washauri wazuri, pengine alikuwa na uwezo wa kumend uhusiano wao badala ya kusingizia matokeo kuwa ndiyo sababu.

Wehu!


Gwajima nimesema ni public figure, na kama amekuwa na unyofu wa moyo maungamo au kukanusha ni uanaume, lakini kunyamaza ni dalili kisaikolojia kukiri kosa bila kujutia na kuondoa wingu linazofunika ndoa ya wenyewe. Mchungaji kuhusishwa na tuhuma za matatizo ya wanandoa si jambo dogo, hawa ni kondoo wake anaowachunga.
 
Sasa hiyo mbasha anashindwa hata kumanage mkewe mpaka apeleke shituma magazetini .Kama mwanaume kweli siande mwenyewe kwa Gwajima na kumwonya kuhusu mahusiano yake na mkewe badala ya Kuna kuyaongelea huku mitandaoni.Naanza kuwa na wasiwasi na uanaume wake kama kichwa cha familia
 
Sasa hiyo mbasha anashindwa hata kumanage mkewe mpaka apeleke shituma magazetini .Kama mwanaume kweli siande mwenyewe kwa Gwajima na kumwonya kuhusu mahusiano yake na mkewe badala ya Kuna kuyaongelea huku mitandaoni.Naanza kuwa na wasiwasi na uanaume wake kama kichwa cha familia

Usiombe yakukute ya mwenye nguvu kushindana na mlalahoi. Mfalme Daud alimtamani mke wa Uria Mhiti, alipomwita na kuonja tu utamu wake, akaamuru Uria Mhiti vitani awekwe mbele eneo lenye wapiganaji wakali auawe. Alifanikiwa na kisha kumtia kiulaini mke wa Uria Mhiti kuwa mke wake. Historia ni mwalimu, hayo niongeleayo ni kutoka Biblia.
 
Mungu atamlipia mke anauma hasa akichukuliwa na mwenye nazo unabak kutazama tu machoz yk yataleta majibu cku moja
 
Back
Top Bottom