Mchungaji wa Watu wa Mungu, ikiwa ulitajwa kwenye tuhuma za mihadarati na ulichunguzwa ukakutwa huna hatia, basi samehe tu kama ambavyo Dr Slaa alivyokusamehe bure kabisa,
Mtumishi wa Mungu halipi kisasi, mtumishi wa Mungu huachilia na kumkabidhi Mungu tu apigane na wanaopigana nae.
Ukristo hatufunzwi kulipa kisasi kabisa, sasa hii ya kuingia na kujivika vita vya kimwili umekosea sana Mungu wa majeshi hana vita ya aina hii kabisa ndugu mtumishi wa Mungu.
Piga goti utubu kabisa hii ni dhambi kubwa unayofanya ya kupambana kimwili na kumruhusu pepo mchafu mlipa visasi na mpigana vita ya mwili atoke kabisa, vinginevyo ataua huduma yako.
Rc Makonda pamoja na mambo mengine lakini bado tunaamini kuna watu wanawatumia viongozi wa dini na baadhi ya viongozi wa serikali wasio na maadili na wapiga dili ili kumdhoofisha kwa sababu tu ya kuvuruga biashara yao haramu,
Mtumishi wa Mungu usifuatane nao kabisa utajikuta ukicheza ngoma ya kuzimu na kuua huduma yako.
Mtemi Nyakarungu