Nawe umerudia yaleyale ya Gwajima, umehukumu. Tafiti, yawezekana Gwajima yupo sahihi. Dunia hii ina jambo moja la ajabu ambalo wengi wetu tunapopanda kimadaraka au kupata fedha tunasahau kwamba kama tunavyowajua wengine ndivyo na wao wanavyotujua. Tulizaliwa na kulelewa huko vijijini na watu wanatujua.
Yawezekana madai ya Gwajima yasiwe na mashiko kwa sasa, lakini Paschal, elimu yetu Tanzania hasa hasa kati ya miaka ya 70 na 90 ilijaa magumashi tu, na hili la kutumia majina ya wanafunzi wengine lilikuwa jambo la kawaida. Leo hii ukizungumzia mwenye jina lake halisi kwa waliosoma kipindi hicho utachekwa sana kwa sababu kuchukua majina ya wanafunzi wengine lilikuwa jambo la kawaida, kwa hivyo sishangai kuyasikia haya maana ndo ulikuwa mtindo wakati huo--kukariri madarasa kwa majina ya wanafunzi watoro, wagonjwa nk. Kwa hiyo hili la Makonda kama ni kweli mimi sishangai, na watu wa aina hii wapo wengi tu, iwe serikalini au sekta binafsi. La Makonda linakuzwa tu kwa vile kagusa madawa ya kulevya!!