Hapa huwa hakuna middle ground, Kama wewe si muumba basi ni kiumbe. Sasa naomba nikuulize, mkuu wa mkoa ambaye unasema kumuita kiumbe ni kosa sasa yeye ni nani?! Ni muumba?! Ukishajua anafiti wapi basi ndio utajua kuwa ulikomenti kwa kuongozwa na mihemko.Haiwezekani amuite Mkuu wa Mkoa kiumbe...ni kosa kubwa sana
Kweli ndugu hata mfalme Daudi alimchukiza Mungu kwa kumchukua mke wa Jemedari wakeNi rahisi sana muumini wa kawaida kuingia mbinguni kuliko mchungaji kuingia mbinguni. Trust me
Ni kweli Mfalme Daudi alitenda dhambi nyingi na nyingine kubwa. kwanza alisema uongo kumdangaya jemedari wake Uria kumshawishi kwenda vitani, (amri ya 7: "usiseme uongo). Pia kwa kumtamani mke wa mtu mwingine (amri ya 9, usitamani mke wa mtu mwingine").Kwe
Kweli ndugu hata mfalme Daudi alimchukiza Mungu kwa kumchukua mke wa Jemedari wake
Mbingu ni ya kwako?Ni rahisi sana muumini wa kawaida kuingia mbinguni kuliko mchungaji kuingia mbinguni. Trust me
Unaweza vipi kutenganisha dini na siasa? Wewe siyo mzima kichwani.Tangu nianze kumuona mhubiri huyu katika media amekuwa more in politics ndiyo maana hata katika uchaguzi mkuu 2015 alizunguka nchi nzima akimnadi Fisadi Papa ili awe rais wetu.
Swali langu ni kwamba, sheria inasemaje kwa mhubiri anayechanganya dini na siasa?
Kwa nini serikali inakuwa na kigugumizi kumkanya ama kumchukulia hatua?
Au hayo anayoyafanya yana mkono wa serikali ndani yake?
Aulizaye anataka kufahamu
Tutahudhuria bila kukosa, ila kinachofanywa hapa ni kazi ya Mungu?.Siku ya Jumapili wakazi wa jiji la Dar es Salaam na viunga vyake mnashauriwa kukaa mkao wa kiroho maana Mtumishi wa Baba askofu Josephat Gwajima Asiyependa kuficha maovu ataweka kila kitu hadharani.
Huenda nafasi ya wote kuingia kanisani ikakosekana lakini mpango unafanywa ili ibada iwe youtube live
Kwa hisani ya Dada wa TaifaView attachment 851158
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kazi ya viongozi wa Mungu kuficha na kukemea maovuTutahudhuria bila kukosa, ila kinachofanywa hapa ni kazi ya Mungu?.
P.
Uwezo wa kuielewa na kuitambua kazi ya Mungu umefifishwa na ukakamavu wa jiwe "usiwe na miungu mingine ila jiwe"Tutahudhuria bila kukosa, ila kinachofanywa hapa ni kazi ya Mungu?.
P.
Hawa wanapaswa kuwa watumishi wa Mungu na kufanya kazi ya Mungu kuhubiri Injili, sasa hiki anachokwenda kufanya mtumishi huyu ndio kazi ya Mungu?!.
Nabii Issa, ndio nani huyu!!?Ni kati ya wale aliosena nabii Issa ( manabii wa uwongo ) tena yeye ni kiongozi wao . Ni kuchafua watu na kuhubiri uchawi
Sent using Jamii Forums mobile app
Nabii Issa ni Nabii wa Mungu, jina lake halisi ni Issa Bin Mariyam kwa Kiislsmu kwa Kikisto ni Yesu Kristo.Nabii Issa, ndio nani huyu!!?
Sent from my TECNO-J8 using Tapatalk
Mkuu watu wengi kwenye dini wanaingiza ushabiki. Maelezo yako wengi hawatakuelewa kwasababu moja tu ya Ushabiki! Walichosahau ni kuwa dini si kitu cha ushabiki kama mpira. Hakuna mshindi wala mshindwa hapa duniani kwenye suala la dini. Mshindi na mshindwa ni baada ya kifo siku ya kiama kwa wanaoamini kwamba kipo.Nabii Issa ni Nabii wa Mungu, jina lake halisi ni Issa Bin Mariyam kwa Kiislsmu kwa Kikisto ni Yesu Kristo.
Mungu ni mmoja, na sheria ya Mungu ni moja tuu, ile ile sheria ya Musa. Kitabu cha sheria ndani ya Quran ni Tourat, ndani.ya Biblia ni Kumbukumbu la Torati.
Adam na Eva ndio Adam na Hawa.
Nabii Ibrahim ndio Abrahamu.
Watoto wake, Ishamel na Isaka ndio Ismaili na Isihaka. Yakobo ndio Yakub, Mtoto wa Yakobo Joseph ndio Yusufu alioeapeleke wana wa Israel, utumwani Misri, na Moses ndie Musa!.
Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja na Mungu mmoja ila majina tofauti!.
P.
Nabii Issa wa kwenye quran na yesu kristo wa kwenye biblia ni watu wawili tofauti kabisa soma historia zao vizuri kwenye hivyo vitabu(kuanzia kuzaliwa kwao hadi kuondoka kwao hapa duniani).Ingawa kwa vitu vichache wanafanana kama uponyaji wa vipofu na viziwiNabii Issa ni Nabii wa Mungu, jina lake halisi ni Issa Bin Mariyam kwa Kiislsmu kwa Kikisto ni Yesu Kristo.
Mungu ni mmoja, na sheria ya Mungu ni moja tuu, ile ile sheria ya Musa. Kitabu cha sheria ndani ya Quran ni Tourat, ndani.ya Biblia ni Kumbukumbu la Torati.
Adam na Eva ndio Adam na Hawa.
Nabii Ibrahim ndio Abrahamu.
Watoto wake, Ishamel na Isaka ndio Ismaili na Isihaka. Yakobo ndio Yakub, Mtoto wa Yakobo Joseph ndio Yusufu alioeapeleke wana wa Israel, utumwani Misri, na Moses ndie Musa!.
Wakristu na Waislamu ni watoto wa baba mmoja na Mungu mmoja ila majina tofauti!.
P.
Ni haki yako kushangaa...you're what you know.Hawa wanapaswa kuwa watumishi wa Mungu na kufanya kazi ya Mungu kuhubiri Injili, sasa hiki anachokwenda kufanya mtumishi huyu ndio kazi ya Mungu?!.
Usiniambie kuwa, kuna watu na akili zao timamu, siku hiyo, watatoka majumbani mwao, kwenda kulishwa neno la Bwana kumhusu Bashite!.
Wakijitokeza kwa wingi, nitashangaa!.
P.