Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Umedhihirisha ujinga wako. Nini maana ya historia kama unahitaji uone kila kitu? Pia Yesu Kristu yupo katika ROHO, na walio wa rohoni humuona!! Sasa neno hili ni gumu kwa mnaopima mambo kwa jinsi ya mwili. Nimepata kumwona? Katika roho, YES!!

Sent from my TECNO-J8 using Tapatalk
 
Vyovyote vile utakavochagua kuamini, Upo sahihi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni thread ya swali, inayoambatana na hoja, kama unamajibu, jibu hoja.

Swali ni dogo sana na very simple, hiki kinachofanywa na mchungaji huyu ndio kazi ya Mungu wa kweli au hii ni kazi ya mungu?!.
P
Ukitazama kwa kigezo cha NENO LA MUNGU, afanyacho mch Gwajima ni kutumia mgawanyiko wa kisiasa uliopo kwa maslahi binafsi. Nasi waumini wakristo tumehama kwenye njia ya NENO ambayo yatutaka kuishindania imani, na sasa tunawapigania watumishi. Ndio maana kitokacho kinywani mwa "mtumishi wa Mungu" kina nguvu kuliko andiko lililomo kwenye Biblia Takatifu.

Mch Gwajima anachofanya ni kucheza na akili za watu for personal gain. Na kama unabisha, ibada za aina hii huhudhuriwa na watu wenye mlengo sawa "wa kisiasa" kuliko imani. Pia baada ya ibada hutarajii kuna watu makundi makundi waliohudhuria kuchomwa dhamira zao hata kuokoka. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua

Sent from my TECNO-J8 using Tapatalk
 
Hata hiyo sheria ya Mungu haijawahi kuoana. Ama ni sheria mbili tofauti, ama kitabu kimojawapo kimefanyiwa mabadiliko.
Mungu kweli ni mmoja tuu, sheria ya Mungu ni sheria moja tuu ya Mussa, imeletwa kwenye Torati. Yesu hakuja kuitengua sheria ya Musa, amekuja kuikamilisha. Ni kweli sheria ya Musa, imepindishwa kwenye kitabu kimoja.

P.
 
Chochote kisemwacho madhabahuni na mchungaji ni wakati wa ibada ni mahubiri.
 
Mi nashangaa sana ili jambo
Na naona mh makonda yeye mwenyewe analikuza hili jambo
Na najiuliza kwa nini asitoke hadharani akalimaliza ili jambo?
Tunajadili mambo ya kijinga huku mambo ya msingi tukiyapuuzia
Hivi mkuu wamekuja watu wakasema ukiwa tumbo wazi una kinundu mgongoni, wakaongeza kama unabisha vua shati.NA ukivua tu demu uliyempenda na kumkubali ukamfukuzia karibu ya kumpata anakukataa mazima. Wewe utavua.
 
Ni rahisi sana muumini wa kawaida kuingia mbinguni kuliko mchungaji kuingia mbinguni. Trust me

Je, naweza kuuliza ni kwa nini? Yaani walio wachungaji kama wanaitafuta mbingu waache kuchunga kundi la Bwana wakachungwe wao? Nisamehe tu ila nayaita hayo; Mawazo mufilisi kabisa.

Pia Paskali namwambia; Manabii huwa wa kweli pale ayasemayo yanapotokea. Be patient Pascal
 
Kwa hili la Makonda naanza kuamini kuwa Gwajima ni NABBIII
 
we pasko ni gwiji la uandishi,wataelewa tu endelea kuandika.lile jibu la mayala kwetu ni njaa,halijakutoa njiani bro, nakuona upo, tena uko sawa,ALUTA continua
 
Mkuu
Hii ni thread ya swali kumhusu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo wa Uzima, Mchungaji, Dr. Josephat Gwajima, Jee ni Mtumishi wa Mungu wa Kweli?!, ni Nabii wa kweli au ndio wale manabii wa uongo aliowazungumza Bwana wetu Yesu Kristo?.
Mkuu huyu sio Nabii.
 
Kauli ya gwajima ni sahihi. Kati ya mtoa baraka na muomba baraka ni nani aliye mkubwa kuliko mwingine?

Ukijibu swali hili utaelewa. Raisi mwenyewe tumemuona mara kibao akielekea kwa hawa watumishi akipiga magoti kupokea baraka angekuwa mkubwa kuliko wao viongozi wa kiroho si angejipa mwenyewe. Mimi binafsi nasema kiongozi wa kiroho ni mkubwa mno kuliko kiongozi wa kidunia.

Tusifananishe viongozi wa dunia na wa kiroho. Kila aliye kiongozi wa kiroho pia ni kiongozi wa dunia lakini si kila kiongozi wa dunia ni kiongozi wa kiroho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…