Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Mashambulizi ya Mayalla kwa Daudi ni ya hatari ni kisu cha mgongoni. Ni kweli Gwajima kaibua kufikirisha kutokana na ushaidi alioutaja... mfano Daudi hakuchaguliwa/hakupata nafasi ya kujiunga na sekondari baada ya kumaliza Nyanza primary halafu tunamuona Daudi kajiunga na Pamba secondary ambayo ni shule ya serikali (kunahitaji ufafanuzi) pili Christina ni nani kwa Daudi mpaka amuunge na Paul? Na kwa nini sasa Christina yuko tayali kumuumbua Daudi?

Kuna mahali dot za kupachikwa jina Makonda imepatiwa connection kwamba ni initial object M kwenye Paul Christian. M

Utata mwingine upo kwenye kuwa vyeti ofisini kwa mchungaji je ni copy ya results slip au original? Amevipataje?

Swali lako la msingi linajibiwa na swali hili kati ya mchungaji na rais nani humpigia magoti mwenzie kwa hiyari?
Viongozi wote wakienda kwenye ibada hupiga magoti kuomba mungu.
 
Haya yote yanayoendelea kwa ndugu yangu Paul Makonda ni matokeo ya kufanya kazi kwa sifa,uonevu,dhuluma,
kuwaharibia watu na kuwachafua wenzako ili ww ndio uonekane mchapa kazi,kufanya kazi kwa visasi ili kuwakomoa watu wengine.Hakuna mwanadamu mkamilifu kila MTU ana mapungufu yake ndio maana mwisho wa siku mtu ukimharibia anakaa kimya kujipanga ili nae akuharibie kwa namna yoyote ile.Watawala wetu,viongozi wetu wakifanya kazi kwa kufuata katiba,sheria, kanuni,miongozo
mbalimbali, Job descriptions,hekima na busara itapelekea kupunguza malalamiko kama haya ya Gwajima kwa viongozi wetu.
Tatizo taifa letu linawazee na viongozi wa dini waoga sana, kazi za wazee na viongozi wa dini ni kuwaonya vijana.
 
Kwanza nashauri tusimpuuze sana Gwajima. Ana watu wengi, na si ajabu kupata taarifa kama matokeo ya form 4. Kwani tuna uhakika gani kwamba hakuna muumini wa kanisa lake anayefanya kazi NECTA? Lkn kwa upande mwingine, tuombe pia kile anachoomba Paskali kiwe kweli. Kwamba isije kudhihirika kwamba yule kiumbe jina lake la kweli ni Daud Bashite! Itakuwa ni a shame of the century.. Cha muhimu zaidi, tunaomba ukweli ujulikane na kila mtu atendewe haki.
ikumbukwe kuwa makonda amewafanyia wengi mabaya na wale wote ambao wameonewa na makonda kwa namna zote ndiyo hao hao wameamua kumchimba kwa undani zaidi japo makonda na yy kaingiza pesa nyingi kuwanunua wale wote ambao wametajwa na Gwajma, kuna vioja vinakuja yaani ile ile style ya Steven nyerere, watu wote watapewa pesa na Dalali watakuwa pasco na Steven nyerere watachukuliwa watapelekwa kuongea na vyombo vya habari watakanusha kila kitu ndipo utajua kuwa pesa ni Adui wa Ukweli pia ni kikwazo cha vita juu ya vyeti feki.
 
Zamani enzi za mkoloni tukimaliza shule tulikuwa tunapewa leaving certificate,
sasa si hicho nacho ni cheti,au siku hizi hamna leaving certificate?,

mi kinachonitia shaka huyu makonda atakuaje Daud Bashije wakati bashije sidhani kama ni jina la kisukuma?,
hapa kuna watu wataumbuka wakifanya mchezo,kama makonda ni DAUD ALBERT BASHIJE na alichukua cheti cha PAUL CHRISTIAN,then jina makonda lilitoka wapi?,

babake na huyu mkuu wa mkoa anaitwa ALBERT BASHIJE au anaitwa MAKONDA?,

So mimi kuamini hii hekaya mpaka nilipate jina la babake na huyu mkuu wa mkoa,vinginevyo hapa kuna usanii

Baba na Mama walikuwa kwenye mahojiano Clouds last week, haikuwekwa vizuri issue hii. Miaka wanayosema amesoma Pamba Sekondari, Mkuu wake wa shule namfahamu sana, and she used to be a very good friend.....Hata mimi nautafuta huu ukweli, kwa hiyo navuta waya muda si mrefu.
 
Kuita kiumbe kwani wewe siyo kiumbe? Hili nalo ni shida kwani? Makonda aka Bashite ni kiumbe yule. Au unadhani mwanadamu ni mungu? Maana hata malaika ni viumbe. Hebu hapo rekebisha Paskally. Pia sijaona pungufu lolote kwa yeye kutaja historia ya Bashite ambaye alihama Kolomije kwenda Mwanza na akadunda la saba.
 
Kama Makonda angemjua ni mtumishi wa Mungu asingemhusisha na kashfa hii kubwa ya madawa ya kulevya na asimkute na ushahidi wowote.Mwacheni aongee apate ahueni wa fikra.Hiyo kashfa siyo ya kitoto
 
....................................Hili la kudai anavyo vyeti vya Daudi Bashite na Paul Christian, Jee hii inaweza kuwa kweli?!. Nijuavyo mimi, mtu ulikuwa ukipata Div. 0 hupewi cheti chochote na NECTA zaidi ya Leaving Certificate, sasa hicho cheti cha Daudi Bashite alichonacho Mchungaji Gwajima, kimetoka wapi?. Gwajima kama mtu wa Mungu wa kweli, anaweza kweli kusema uwongo madhabahuni, jee huyu ni mchungaji wa kweli anayemtumikia Mungu.
Paskali
Nawewe hii kitu umeiandika kishabiki, huoni kwamba huyu ni whistleblower mzuri sana katika kipindi hiki cha vyeti feki? cha kufanya vyombo vinavyohusika vifanyie kazi hii taarifa kama ni ya kweli makonda awajibishwe kama ni uongo Gwajima awajibishwe, suala la kwamba ni uongo au ukweli hutakiwi kulizungumzia wewe hapa, mimi ninafahamu mtu akipata zero hupewa Result slip sasa sijui gwajima angetumia jina gani rahisi la kiswahili la result slip. Na ishu aliyosema kwamba yeye kugombea urais au ubunge ni demotion kwake anaweza kua sahihi kabisa kwasababu amezungumza kiroho zaidi ndiyo maana Rais akiingia ibadani anakua mnyenyekevu sana anaweza kushikwa mpaka sharubu na mtumishi wa Mungu katika mchakato wa kumuombea.
 
Wanabodi,

Kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo, tunayemwamini Bwana wetu Yesu Kristo, kabla hajapaa mbinguni, alituhusia kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?, Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".

Hii ni thread ya swali kumhusu Mchungaji Gwajima Jee ni Mtumishi wa Mungu wa Kweli?!. Akiwa katika mimbari, madhabahuni, badala ya kuhubiri neno la Mungu lenye kujenga upendo, yeye anahubiri siasa za chuki dhidi ya binadamu mwingine hadi kumuita "kiumbe".

Isikilize Clip hii Akisema Uongo Madhabauni, tena mchana kweupe. Mara baada ya Mashekh wa Mkoa wa Dar es Salaam, kumuombea dua, Mkuu wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mchungaji Gwajima, amemuonea vivu kuwa dua zile zitazidi kumnyooshea mambo yake, hivyo ili kumbomoa, Mchungaji Gwajima, mwenye utajiri wa ajabu (Hammer, Helcopter, na kanisa kubwa), akaamua kuhubiri mahubiri ya kusingizia, kwa kumsingizia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda kuwa ni mhalifu wa kosa la jina la kuiba jina la mtu mwingine, na kosa la kughushi kwa vyeti, kwa kudai kuwa eti jina halisi la Paul Makonda, sii jina lake, ni jina la mtu mwingine, Makonda jina lake halisi ni Daudi Albert Bashite!, na hakuishia hapo, amedai Yeye nini Zaidi ya Rais, kugombea urais ni demotion!. Hivi kwa mtumishi wa Mungu wa kweli, anaweza kusema maneno kama haya madhabahuni kwa Mungu, au Mchungaji huyu, ni wale Manabii wa Uongo, Bwana wetu Yesu Kristu aliotuhusia?.

Msikiliza Mchungaji Gwajima.


Nimeisikiliza hii clip hii ya Mchungaji Gwajima, akimzungumzia Daudi Albert Bashite, A.K.A Paul Christian Makonda, akidai kuwa kilichomponza yeye Mchungaji Gwajima hadi kusingiziwa madawa ya kulevya, ni dhana kuwa anataka kugombea ubunge jimbo la Misungwi, kufuatia kutua kijiji Kolomije kwa Chopa, (Helcopter), hivyo Daudi Bashite, A.K.A Paul Manajipanga kugombea jimbo hilo mwaka 2020!. Mchungaji Gwajima akajitapa Ubunge, Uwaziri hadi Urais kwa Mtumishi wa Mungu aliye hai ni demotion!. "Mtumishi wa Mungu ni zaidi ya Rais wa nchi!". Jee hii ni kweli?.

Akielezea kuhusu Daudi Albert Bashite, na yeye Mchungaji Gwajima, ni watu wa kabila moja na wametokea kijiji kimoja cha Kolomije. Daudi Bashite alisoma Shule Msingi ya Kolomije hadi darasa la tano, akahamia Shule ya Msingi ya Nyanza hadi akamaliza Darasa la 7, hakuchaguliwa. Akajiunga na Shule ya Sekondari Pamba, akiwa anakaa kwa mama Kamese (Gwajima ana simu yake) ambako alipata Divisheni 0, ndipo dada mmoja wa Kihaya kwa jina la Christina (Gwajima ana simu yake) akamuunganishia Daudi Albert Bashite, kwa mdogo wake, Paul Christian, hivyo Daudi Bashite akaanza kutumia cheti cha kaka yake Paul Christian ndipo akajiunga Nyegezi kusomea certificate ya uvuvi kwa jina la Paul Christian Makonda, kisha akajiunga Chuo cha Mbegani Bagamoyo kuchukua diploma ya uvuvi na kumalizia Chuo cha Ushirika kuchukua degree kwa majina ya kughushi ya Paul Christian.

Katika kumuelezea Daudi Bashite, Mchungaji Gwajima amemuita "kiumbe huyu", hili sio neno zuri kwa kiongozi wa dini ya Mungu kweli, kumuita binadamu mwenzako kiumbe!.

Ila pia Mchungaji Gwajima amedai, anavyo vyeti vyote ofisini kwake tangu cha Daudi Albert Bashite alichopata Divisheni 0. hadi cheti cha Paul Christian alichounganishiwa na Christina!, na kudai kuwa ana mshitaki Makonda kwa Ndalichako na kwa Magufuli, na asipochukuliwa hatua zozote, yeye atashangaa sana na atavitoa vyeti hivyo hadharani, umma uvione.

Swali ni jee huu ndio utendaji wa watu wa Mungu, kuwatakia wenzao mabaya?, kuwazushia uongo mchana kweupe tena madhabahuni kwenye mimbari ya Mungu?!. Huyu ni mchungaji wa Mungu au mungu. Hili la kudai anavyo vyeti vya Daudi Bashite na Paul Christian, Jee hii inaweza kuwa kweli?!. Nijuavyo mimi, mtu ulikuwa ukipata Div. 0 hupewi cheti chochote na NECTA zaidi ya Leaving Certificate, sasa hicho cheti cha Daudi Bashite alichonacho Mchungaji Gwajima, kimetoka wapi?. Gwajima kama mtu wa Mungu wa kweli, anaweza kweli kusema uwongo madhabahuni, jee huyu ni mchungaji wa kweli anayemtumikia Mungu, au ndio hawa wachungaji wanaomtumikia mungu?!.

Jumatatu Njema.
Paskali


Kiutendaji ni kweli kabisa mchungaji ni zaidi ya Watawala,kwa maana kwamba wanafanya kazi ya Mungu.Ni kiimani zaidi kuliko kisiasa
 
ikumbukwe kuwa makonda amewafanyia wengi mabaya na wale wote ambao wameonewa na makonda kwa namna zote ndiyo hao hao wameamua kumchimba kwa undani zaidi japo makonda na yy kaingiza pesa nyingi kuwanunua wale wote ambao wametajwa na Gwajma, kuna vioja vinakuja yaani ile ile style ya Steven nyerere, watu wote watapewa pesa na Dalali watakuwa pasco na Steven nyerere watachukuliwa watapelekwa kuongea na vyombo vya habari watakanusha kila kitu ndipo utajua kuwa pesa ni Adui wa Ukweli pia ni kikwazo cha vita juu ya vyeti feki.

Hapana Mkuu. Issue ya vyeti haiko vile. Ni ngumu sana kufuta nyayo zake. Hata ukifunika kiana, watakuja watu watathibitisha kwamba hukuwahi kusoma katika darasa lile. Ni ngumu sana kufunika hii kitu, labda watu waamue tu makusudi kutochukua hatua..
 
Mkuu hawa wote ni viongozi mmoja wa kiroho na mwingine wa umma na wote wapo Dsm hivyo siyo busara kugombana waziwazi, busara za wazee zitumike, hawa wazee wakina Warioba, Paul Bomani, Mangula ndiyo kazi zao hizi.
Wazee wa CCM hao ............ Tangu lini ulishaona Mzee wa Kitanzania akija hadharani na kusema maneno na akayasimamia mpaka mwisho!!?

Tena Mzee wa CCM .......................!! Kama akina Mwinyi, Mkapa wanashindwa kusema hadharani bila kuuma wala kumungunya unategemea nani atakayeweza huko CCM!!
 
Kama Makonda angemjua ni mtumishi wa Mungu asingemhusisha na kashfa hii kubwa ya madawa ya kulevya na asimkute na ushahidi wowote.Mwacheni aongee apate ahueni wa fikra.Hiyo kashfa siyo ya kitoto
Gwajma anayo haki ya kujihami kwa 100% ndiyo maana wengi wanamuunga mkono, lakini pia amewasaidia watanzania kujua mengi juu ya wajibu wa mkuu wa mkoa pia vita juu ya vyeti feki ilivyokuwa ngumu hasa kwa wateuliwa wa mkulu.
 
Back
Top Bottom