Kimaro, kitu cha kwanza hajaokoka, hata mafundisho yake mimi huwa nashangaa watu wanayapapatikia ya nini, hayana mantiki yeyote na hayaokoi roho za watu. siku hizi kumeibuka mtindo wachungaji wengi ambao hawajaokoka wanafuata mtindo wa kuhubiri anaotumia mchungaji mgogo. anasimama pale hahubiri Neno la Mungu, anaongea tu maneno yake ya kibinadamu yenye hekima ya kibinadamu tu ila sio kutafisiri Neno la Mungu kwa watu. watu wanawapenda kwasababu wanatumia style ya kuchekesha kama wachekeshaji, ila hawahubiri Neno la Mungu. na wateja wao wakubwa ni wanawake, kama ilivyo ada, hao ndio wahanga wakubwa wa kila mihemko.
mchungaji mgogo ameharibu sana tasnia ya kuhubiri, ndio maana utakuta mch kimaro alikuwa anamuiga, mchungaji Hananga alikuwa anamuiga, kale ka kijana kembamba kenye kanisa nako kanaitwa Tony kanamuiga, ni kwamba wanaongea mambo yale yanayowafurahishwa watu, yale watu wanayapenda na kufurahi na kuchekacheka.
kwa Kimaro, kama yeye ana hekima, kwanza asingetangaza yale aliyokwazana na maboss wake (wanaompa mshahara) kwa waumini, na hakutakiwa kuongea kwa namna ya kuonewa huruma, ili wamuonee huruma aonekane anaonewa.
pili,angekuwa na hekima, angeshawatuliza, angeshatoa tamko ili hata wale wanaojifanya kuandamana au kumtetea wasingefanya vile kama angekuwa ametoa neno la hekima kwamba wasifanye hivyo.
kilichopo ni kwamba, kimaro na wengine, wanategemea kuinuka kwa kutumia wanadamu, hawajui kama kama wangekuwa watu wa Mungu, Mungu ndio huwa anainua mwanadamu na Mungu akikupa kibali hata mtu akupinge hawezi kukushinda, na ukipingwa unachotakiwa wewe ni kutumia hekima ili usiwapoteze hata wale wenye mioyo laini wakamkosea Mungu kwasababu yako, wabaki vilevile na Mungu atakusaidia atakavyo. kitendo cha yeye kunyamaza anaonyesha jeuri na matumaini ya kutetewa na wanadamu na anapenda aendelee kutetewa hadi arudishwe pale.
afterall, hata mahubiri yake sio ya kimungu, wakubwa zake na kanisa lote la lutheran tunalijua tumetoka huko hakuna Mungu kabisa na hakuna wokovu kwasababu misingi yake haijajikita kwenye uongozi wa Roho Mtakatifu bali uongozi wa dini na hekima ya kibinadamu.