Mchungaji Mtikila alisema Kikwete ni Gaidi na akashinda ile kesi

Mchungaji Mtikila alisema Kikwete ni Gaidi na akashinda ile kesi

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Hii wadau ilikaaje? Mch. Christopher Mtikila. Msomi wa juu wa Sheria, mtu mwenye akili na ujasiri. Alisema wazi bila kuuma uma maneno. Kuwa aliyekuwa Rais wa Tanzania kipindi hicho ndugu kikwete ni gaidi.

Sielewi ile kesi alishindaje shindaje. Je ilithibitishwa kweli ikafunikwa au ilikuaje? Ni mwanasiasa pekee ambaye ameshawekwa sana ndani na kushinda kesi nyingi sana Tz.

Pia soma > Tupige kidogo ‘mastori’ ya Mchungaji Christopher Reuben Mtikila

----
Ni kwamba Mtikila alidaiwa kutoa maneno ya uchochezi na kashfa dhidi ya Rais Kikwete kwa kumuita gaidi kwa madai kuwa serikali anayoiongoza inataka kuanzisha mahakama ya kadhi, jambo ambalo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari mwaka 2009 na Aprili 17, mwaka 2010 jijini Dar es Salaam, kwa nia ya uchochezi mshitakiwa alisambaza kwa umma nyaraka zilizosema 'Kikwete kuuangamiza ukristo', 'wakristo waungane kuweka mtu Ikulu'

Shitaka la pili likadai kuwa

Aprili 16, mwaka 2010 eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam, bila kibali alikutwa akimiliki waraka wenye uchochezi kwa jamii.

Nakumbuka polisi walivamia nyumbani kwa Mtikila kusaka waraka huu

Katika kesi hii Mtikila hana wakili wa kumtetea na anajitetea mwenyewe.

Kesi hiyo ilisikilizwa na mahakimu watatu tofauti ambao ni Waliarwande Lema, Sundi Fimbo

Mahakimu wawili walilazimika wajitoe baada ya Mtikila kuwakataa kwani anaamini hawana hadhi na hawawezi kumtendea haki.

Mwisho wa siku, kesi hiyo akapangiwa hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo (kwa wakati huo Elvin Mugeta) ambaye aliisikiliza Kesi hiyo na Septemba 25 Mwaka 2012 ,alitoa hukumu ya kumuachilia huru Mtikila baada ya upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha kesi yao.

Nakumbuka siku Mtikila alipotoa utetezi wake katika Kesi hii nilikuwepo.

Mtikila Kama kawaida alikanusha madai ya jamhuri uwa ule waraka wake uliokuwa na kichwa cha Habari kisemacho (KIKWETE KUANGAMIZA UKRISTO) kuwa ni wa uchochezi.

Mtikila alikubali kuwa ule waraka ni wake na aliundaa yeye na siyo wa uchochezi na kwamba hawezi Kuukana waraka ule kwasababu Kuukana walaka ule ni sawa na kumkana YESU KRISTO"

Baada ya kuachiliwa huru Mtikila akasikika akisema Haleluya!

Huku polisi wakijiandaa kumkamata tena

Kule nje polisi walipomsogelea kwa lengo la kumkamata, Mtikila akawaambia

"Nyie Polisi hamna uwezo wa kunikamata kwanza mnavyeo vya chini sana....Kama mnataka kanifungulia kesi nyingine nitakwenda Mwenyewe Kituo cha polisi kuripoti"

Mtikila akaendelea

"Hata boss wenu IGP- Said Mwema ananiita kwa heshima kwa kunipigia simu naenda mwenyewe Polisi,ebu toeni Ujinga wenu hapa"

Mtikila alisema na kusababisha watu kuangua vicheko na Polisi wale waliokuwa wamepanga kumkamata kumuacha Mtikila aende zake nyumbani.

Credit: Fortunatus Buyobe
 
Baba mzazi hata kama anakosea HATUKANWI...

Kiongozi mkuu wa nchi yuko juu zaidi ya baba zetu wazazi....maana yake Kikwete baba wa Ridhiwani anatakiwa asitukanwe hata kidogo ila Kikwete Rais yuko juu zaidi ya Kikwete baba wa Ridhiwani kwa mwanaye mwenyewe huyo Ridhiwani.....

Kiongozi HATUKANWI....

Kiongozi HAZUSHIWI....

Mtikila alikuwa ni mzushi wa kuleta chokochoko za UDINI...udini ni UWENDAWAZIMU....

#Nchi Kwanza[emoji2956]
 
Mtanganyika Mtikila alikuwa ni big brain, huwezi fananisha na hawa chawa wa leo wanaokimbia midahalo.
 
Mikristo inataka itawale yenyewe tu, na ndio maana rais akiwa muislam kila baya anazushiwa,
Kuweni waadilifu wagalatia
 
Tatizo Mtikila alijiganga kwa kutumia utamaduni wa Kiyahudi, angetumia jadi yake ya asili wasingemmaliza. RIP.
 
Hi ya "..wewe huwezi kunikamata, cheo chako ni kidogo..." nakumbuka niliiona kwa TV, I think ilikua ITV. Ni kama alikua na wakili, hakua pekee yake. Anyway, nyakati zinabadirika sana, Kikwete kwenye issues za kukosolewa kwa mtazamo wangu, nadhani apewe MAUA yake. Ingekua kipindi cha JPM au hiki, sidhani kama Mtikila angekua hai, tungekua tumeisha mzika kaburini. Kwanza hata kesi hiyo angeshindaje? Na police awatamkie vile wamuache? Subutu. Hata kama sheria inamlinda but sijui angekuaje yaani
 
Hii wadau ilikaaje? Mch. Christopher Mtikila. Msomi wa juu wa Sheria, mtu mwenye akili na ujasiri. Alisema wazi bila kuuma uma maneno. Kuwa aliyekuwa Rais wa Tanzania kipindi hicho ndugu kikwete ni gaidi.

Sielewi ile kesi alishindaje shindaje. Je ilithibitishwa kweli ikafunikwa au ilikuaje? Ni mwanasiasa pekee ambaye ameshawekwa sana ndani na kushinda kesi nyingi sana Tz.

Pia soma > Tupige kidogo ‘mastori’ ya Mchungaji Christopher Reuben Mtikila

----
Ni kwamba Mtikila alidaiwa kutoa maneno ya uchochezi na kashfa dhidi ya Rais Kikwete kwa kumuita gaidi kwa madai kuwa serikali anayoiongoza inataka kuanzisha mahakama ya kadhi, jambo ambalo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari mwaka 2009 na Aprili 17, mwaka 2010 jijini Dar es Salaam, kwa nia ya uchochezi mshitakiwa alisambaza kwa umma nyaraka zilizosema 'Kikwete kuuangamiza ukristo', 'wakristo waungane kuweka mtu Ikulu'

Shitaka la pili likadai kuwa

Aprili 16, mwaka 2010 eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam, bila kibali alikutwa akimiliki waraka wenye uchochezi kwa jamii.

Nakumbuka polisi walivamia nyumbani kwa Mtikila kusaka waraka huu

Katika kesi hii Mtikila hana wakili wa kumtetea na anajitetea mwenyewe.

Kesi hiyo ilisikilizwa na mahakimu watatu tofauti ambao ni Waliarwande Lema, Sundi Fimbo

Mahakimu wawili walilazimika wajitoe baada ya Mtikila kuwakataa kwani anaamini hawana hadhi na hawawezi kumtendea haki.

Mwisho wa siku, kesi hiyo akapangiwa hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo (kwa wakati huo Elvin Mugeta) ambaye aliisikiliza Kesi hiyo na Septemba 25 Mwaka 2012 ,alitoa hukumu ya kumuachilia huru Mtikila baada ya upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha kesi yao.

Nakumbuka siku Mtikila alipotoa utetezi wake katika Kesi hii nilikuwepo.

Mtikila Kama kawaida alikanusha madai ya jamhuri uwa ule waraka wake uliokuwa na kichwa cha Habari kisemacho (KIKWETE KUANGAMIZA UKRISTO) kuwa ni wa uchochezi.

Mtikila alikubali kuwa ule waraka ni wake na aliundaa yeye na siyo wa uchochezi na kwamba hawezi Kuukana waraka ule kwasababu Kuukana walaka ule ni sawa na kumkana YESU KRISTO"

Baada ya kuachiliwa huru Mtikila akasikika akisema Haleluya!

Huku polisi wakijiandaa kumkamata tena

Kule nje polisi walipomsogelea kwa lengo la kumkamata, Mtikila akawaambia

"Nyie Polisi hamna uwezo wa kunikamata kwanza mnavyeo vya chini sana....Kama mnataka kanifungulia kesi nyingine nitakwenda Mwenyewe Kituo cha polisi kuripoti"

Mtikila akaendelea

"Hata boss wenu IGP- Said Mwema ananiita kwa heshima kwa kunipigia simu naenda mwenyewe Polisi,ebu toeni Ujinga wenu hapa"

Mtikila alisema na kusababisha watu kuangua vicheko na Polisi wale waliokuwa wamepanga kumkamata kumuacha Mtikila aende zake nyumbani.

Credit: Fortunatus Buyobe
Wakati huo kulikuwa na mahakama.
 
kipindi flani alibondwa jiwe la kisogo sijui ilikuwa ni Mara kule?
 
Wakati huo kulikuwa na mahakama.
Halafu na jaji mkuu hakuaga profesa wa sheria kama sasa hvi. Kwa miaka hi, sioni umuhimu wa wana sheria wa serikali kua na elimu kubwa, certificate or Diploma ya sheria inatosha kabisa kumfanya mtu kua JAJI. Maanake case zinavyo amriwa huko mahakamani halafu unasikia kwamba mwamuzi wa kesi hiyo ana degree kadhaa, huelewi yaani. Tuna najisi elimu, elimu inaonekana kama haina maana, so ili tusidhalilishe elimu, napendekeza, sifa za kua jaji au hata hakimu wa mahakama zote kuanzia ya mwanzo hadi ya rufaa, Diploma is more than enough, degree zitumike sekta binafsi, huko walau elimu inaheshimika
 
Halafu na jaji mkuu hakuaga profesa wa sheria kama sasa hvi. Kwa miaka hi, sioni umuhimu wa wana sheria wa serikali kua na elimu kubwa, certificate or Diploma ya sheria inatosha kabisa kumfanya mtu kua JAJI. Maanake case zinavyo amriwa huko mahakamani halafu unasikia kwamba mwamuzi wa kesi hiyo ana degree kadhaa, huelewi yaani. Tuna najisi elimu, elimu inaonekana kama haina maana, so ili tusidhalilishe elimu, napendekeza, sifa za kua jaji au hata hakimu wa mahakama zote kuanzia ya mwanzo hadi ya rufaa, Diploma is more than enough, degree zitumike sekta binafsi, huko walau elimu inaheshimika
We acha kabisa. Umuhimu wa elimu kwa sasa Tz hakuna. Hakuna tofauti na clasa 7 na Phd za hii mihimili. Same same
 
Back
Top Bottom