Mchungaji na mkewe wanusurika kuuawa

Mkuu hiyo ni fursa.Kama una uwezo wa kumkemea jambazi mpaka akakauka basi fungua kampuni za kulinda(Security Companies)ili ulinde kwa kukemea tu.
Za kuambiwa changanya na zako.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ aloooo!
 
Utukufu kwa Mungu
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ aloooo!
Ilitabiriwa zamani kuwa siku za mwisho watu watapenda pesa kuliko kumpenda Mungu. Unabii umetimia

2 TIMOTHEO 3:1-5​

Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake..."
 
Mbona heading inasomeka mchungaji na Mke wake wanusurika kuuawa? Alafu kwenye habari yenyewe anaonekana wewe na mchungaji????? Kama sijaelewa vile!!!!!
 
Mbona heading inasomeka mchungaji na Mke wake wanusurika kuuawa? Alafu kwenye habari yenyewe anaonekana wewe na mchungaji????? Kama sijaelewa vile!!!!!
Kwani heading huwa inaeleza kila kitu?
 
Kwani heading huwa inaeleza kila kitu?
Ulisoma kiswahili japo kwa level ya darasa la sita na ukajifunza kuandika Insha? unawezaje kuandika kichwa cha habari KUKU NA BATA wanasurika kuliwa na mwewe alafu habari yenyewe ikaishia kuelezea jinsi kuku na mbuzi na si bata na kuku walivyonusurika? Bata kwa maana ya mhusika mkuu na namba mbili unamwachaje? Wahusika wakuu kwenye habari ni mchungaji na mkewe na siyo mchungaji na msumliaji, hakukuwa na sababu ya msimliaji kuwa sehemu ya habari.
 
Kwanini kila mara unapatwa na majanga tu! Mara majambazi mra kuunguliwa moto nk! Na je umeokoka hivi karibuni?
Umesoma habari za Paulo? Mimi sijafikia hata robo ya majanga yaliyompata. Sikia anavyosema katika
2 Wakorintho 11:23-27
"...katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.
Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.
Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;
katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;
katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi..."

Unaonaje majanga hayo. Unafikiri ni kwa sababu ya kuokoka hivi karibuni?
 
Mtu anakuteka na panga we unamkemea shetan unaakili kweli bro? Utakuja kufa kijinga acha uboya
Ndo maana mchungaji alikufanya kimbola wake akakutuma ukatoe gogo jamaa wa panga angeanza na ww ndo ungejua mchungaji aliwahi kushiriki mbio za magari
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji119]
 
Mtu anakuteka na panga we unamkemea shetan unaakili kweli bro? Utakuja kufa kijinga acha uboya
Mambo ya rohoni ni vigumu kuyaelewa kimwili.

Mkuu, umewahi kusoma Mathayo 16:23? Imeandikwa hivi:
"Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, β€œRudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”

Hapo aliyekuwa anakemewa ni nani? Ni Petro au Shetani? Ni Shetani, ingawa maneno yalikuwa yanamlenga Petro. Kinachomfanya mtu ashike upanga na kutaka kumuua mwanadamu mwenzake ni nini? Hiyo roho ya Shetani iliyokuwa inamsukuma mtu yule kutaka kuiba na kuua ndiyo tuliyoikemea. Na kwa Jina la Yesu hiyo roho chafu ilisalimu amri. Jina la Yesu ni Jina Kuu kupita majina yote. Haleluya!
 
Itakuwa alikuwa anakata mti apate kuni. Kama umesema hiyo Barabara haiko bize, huyo mtu aliona mda mzuri wa kukata mti wake ndio huo..
HAKUA JAMBAZI
Na vile vijiti vilivyosimikwa pale mwanzo vilikuwa vya nini
 
Mkuu hiyo ni fursa.Kama una uwezo wa kumkemea jambazi mpaka akakauka basi fungua kampuni za kulinda(Security Companies)ili ulinde kwa kukemea tu.
Za kuambiwa changanya na zako.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…