Mdahalo: Kipi Ni Sumu Ya Muungano - Je, Ni Kwa Kuikataa Tanganyika au Ni Kwa Kuikubali Tanganyika?

Mdahalo: Kipi Ni Sumu Ya Muungano - Je, Ni Kwa Kuikataa Tanganyika au Ni Kwa Kuikubali Tanganyika?

Kwa faida ya wengi Ningependa niweke maneno mazito sana yaliyoongewa na Kijana wa BINO, aliyelelewa kwa kulishwa Kitei na Chui lililokuwa linapikwa na Mzee Lukumay na kijana wake Erasto. Huyo Ni TUNDU LISU.


``Mheshimiwa Spika, mapendekezo ya Rasimu ya Muswada hayakubaliki kwa sababu yanaweka mchakato wa Katiba Mpya kwenye huruma na/au fadhila ya Rais wa Zanzibar na siasa za Zanzibar kwa ujumla. Kwa mapendekezo haya, Rais wa Zanzibar asipokubaliana na jambo lolote linalohitaji ridhaa yake basi mchakato mzima utasimama au kusitishwa. Aidha, endapo katika kura ya maoni inayopendekezwa, theluthi mbili ya Wazanzibari hawatakubaliana na Katiba Mpya basi Katiba hiyo haitapitishwa hata kama inakubaliwa kwa kiasi kikubwa na wananchi wa Tanzania Bara.

Mustakbala wa taifa letu hauwezi kuwekwa tena rehani kwenye siasa za Zanzibar na kwenye matakwa ya Wazanzibari kwa kiasi hicho. Kuhusiana na jambo hili, Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar ahusishwe tu katika masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Nje ya masuala hayo, Rais wa Zanzibar hana sababu yoyote ya kuhusishwa na mchakato wa kikatiba unaohusu mambo ya Tanzania Bara."

Aidha, wajumbe wa Tume ya Mapitio ya Katiba ambao watatoka Zanzibar wahusike tu katika mchakato wa masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Vile vile, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza wananchi wa Zanzibar washiriki katika kura ya maoni inayohusu mfumo mpya wa Muungano tu. Hii ndio kusema kwamba, kama vile ambavyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Tanzania Bara hawajashirikishwa katika mchakato wa kikatiba wa Zanzibar kwa sababu ulihusu mambo yasiyokuwa ya Muungano, vivyo hivyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Zanzibar wasishiriki katika mchakato wa kikatiba wa mambo yasiyokuwa ya kikatiba kwa upande wa Tanzania Bara.``
 
Barubaru nilisema huko nyuma kuwa kuingia kwako katika mjadala na kukosa umakini wa kuelewa mada itakuwa tatizo katika nyuzi hii na hapo ndipo tulipo. Tulijaribu sana kuacha ushabiki wa kisiasa na kuongelea muafaka lakini kama kawaida yako umeingia na kutafuta mashindano.

Umeingia kutumbukiza chuki zao za kidini na binafsi. Kwa mantiki hiyo umesha derail and dilute the whole meaning ya thread. Siwezi kurudi kule kwa kujadili mambo yaiyojadiliwa kila mara wala kujadiliana na mtu asiyekabiliana na hoja bali kutafuta vitu visivyohusiana na mjadala ilimradi tu ku justify interest zake.
Hujajibu maswali umebaki kueleza kitu usichoulizwa.

Umewahi kujibainisha kuwa na PhD na pia mchumi wa nchi ya Tanzania, nadhani unapaswa kulindwa heshima za vitu hivyo kwasababu the bar is too high with alot of expectations.With that note I will not urge with you.

I need to add something in my upper chamber leaving no room for utter stupid comments
 
Barubaru nilisema huko nyuma kuwa kuingia kwako katika mjadala na kukosa umakini wa kuelewa mada itakuwa tatizo katika nyuzi hii na hapo ndipo tulipo.
vitu hivyo kwasababu the bar is too high with alot of expectations.With that note I will not urge with you.

I need to add something in my upper chamber leaving no room for utter stupid comments

Nguruvi3.

Napenda nikusaidie kitu kuwa mjadala wowote una pande mbili na watu wanajadili kwa kutoa facts katika maandiko yao na sio bla bla.

Upande wangu sijaandika chochote zaidi ya kujibu maswali yako ulouliza na kudai kuwa hujajibiwa toka last year Na nimejibu kw kuweka rangi na kukujibu kwa kina na vile vile kukuomba ufafanuzi wa baadhi ya mambo uloandika kama kama ULIPODAI MAMBO YA MUUNGANO 15 YAMEONDOLEWA NA VILE VILE ZNZ INAITEGEMEA TGK KIJIOGRAFIA. nimeomba ufafanuzi kwa faida ya wasomaji wetu na kutuelimisha. Hapo utakuwa umetiza lengo la jf la kuelimisha na kupashana habari.

Matusi si uungwana na ilmu yangu nafikiri haikhusu hapa kwani sote tunajadili kukhusu Muungano wenu na kinachotakiwa ni kutoa point tu na kuweka ushahidi au dalili ya kile ulichoandika kwa faida ya wasomaji wote na sio kutaka kile unachotaka wewe ndio kiwe na kisihojiwe hata kikiwa na makosa. Kumbuka huo sasa hautakuwa mjadala tena bali utakuwa UZUZu jambo ambalo mimi siwezi kulifanya.

Kumbuka kwa muungwana kama akivuliwa Nguo BASI ANACHUTAMA NA SIO KUSIMAMA. Hivyo tulia tukupe darsa na sio kuleta ubabe kwa jambo usonaujuzi nalo.

Nakupa pole sana.
 
Back
Top Bottom