Mdahalo wa Wagombea Urais Zanzibar: Septemba 20, 2015 #Mkikimkiki

Mdahalo wa Wagombea Urais Zanzibar: Septemba 20, 2015 #Mkikimkiki

Joined
Jul 2, 2015
Posts
20
Reaction score
23
Shiriki kwa kutuma swali lako hapa JamiiForums kwa ajili ya kuwatumia viongozi watakao shiriki mdahalo hapo kesho Tarehe 20, September 2015.

attachment.php



Mkikimkiki‬ iko Zanzibar wiki hii na wamealika wagombea urais wa vyama vitano ambavyo ni CCM, CUF, ADC, CHAUMMA na ACT-Wazalendo Kushiriki ni kwa mwaliko tu!

Wakti huo huo, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Shirika lisilo la kiserikali la Twaweza, kuna ongezeko kubwa zaidi la Wazanzibari kupatiwa huduma ya umeme kati ya mwaka 2002 na mwaka 2012 pia huduma ya maji ya bomba imeongezeka kwa kiasi kidogo sana kati ya miaka kumi ya 2002 na 2012.

Utafiti huo unaonyesha kwamba Wazanzibari wanapedelea kuona ongezeko la Uhuru wa kujitawala wa Zanzibar na uwepo wa serikali tatu na pia asilimia 5 ya Wazanzibari wanajiona kuwa wao ni Wazanzibari zaidi kuliko kuwa Watanzania.

Tarehe: Jumapili Septemba 20 2015
Muda: 7:00 – 10:00am (Saa saba mchana hadi saa kumi jioni)
Mahali: Hoteli ya Double Tree Hoteli Zanzibar

Midahalo hii inalenga kuvipa vyama vyote fursa ya kunadi Ilani zao na kwa wananchi kuuliza maswali muhimu yatakayo pelekea maamuzi yao katika uchaguzi. Vyama vinavyoshiriki ni vile vyenye wagombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar na wagombea Ubunge angalau majimbo 65.

- Midahalo hii itarushwa moja kwa moja na Star TV na Redio RFA. Vyombo vya habari vinakaribishwa kushiriki lakini lazima wajiandikishe kabla.

- Kupata nafasi ya swali lako kuulizwa kwenye mdahalo, tuma neno KUULIZA acha nafasi, andika swali lako na tuma kwenda namba 15678.

- Kama unapenda kuwa mmoja wa watazamaji ukumbini tuma neno KUSHIRIKI acha nafasi tuma jina na kazi yako kwenda 15678.

- Utatozwa bei ya kawaida ya ujumbe wa simu (SMS). Hakuna gharama ya ziada.

TUWAHOJI, TUWACHAMBUE, TUWAPIME!!

Karibuni!

===============

Update
:
Maandalizi ya kuanza kwa Mdahalo wa Wagombea Urais Zanzibar utakaofanyika Double Tree Hotel yanaendelea..

CPVg_P2UEAAtmFj.jpg

Washiriki Mdahalo leo ni Dk. Ali Shein (CCM), Seif Hamad (CUF), Hamad Rashid (ADC), Mohamed Rashid (CHAUMA), Khamis Lila (ACT).

Mdahalo wa #MkikiMkiki unakaribia kuanza. Kati ya wawakilishi watano wa vyama waliothibitisha kuwepo katika mdahalo, wawili wametoa udhuru.

Wawakilishi wawili waliotoa udhuru wa kutokuwepo kwenye mdahalo ni Dk. Shein (CCM) na Maalim Seif (CUF).

CCM hawajahudhuria Mdahalo huu kwa sababu wanazodai ni za 'kiitifaki'; CUF waliweka sharti kuwa watashiriki kama CCM watakuja.

Muongozaji anatoa taarifa kwa hadhira na anaeleza kwamba mdahalo utaendelea na wawakilishi waliopata fursa ya kuhudhuria.


================

Swali: Ni namna gani vyama vitaendelea kuulinda Muungano wa Tanganyika & Zanzibar?

Khamis Lila (ACT-Wazalendo): ACT-Wazalendo ingependa kuimarisha Muungano na si kuuvunja. Zanzibar na Bara tumeingiliana sana. Muungano una faida nyingi; ukienda kokote Bara na Visiwani huulizwi na mtu umetokea wapi na unafanya nini.

Hamad Rashid (ADC): Watanzania wanauhitaji Muungano. Sisi tunaamini Muundo wa Serikali unatokana na wananchi na kura ya maoni. Maamuzi ya wananchi yaheshimiwe juu ya aina ya Muungano wanaoutaka. Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu; Mataifa yote yana nguvu kwakuwa yanakuwa yameungana.

Mohamed Rashid (CHAUMMA): Wananchi wanataka Muungano wa Serikali 3 zisizobagua kokote. Aina ya Muungano ya sasa inawanyonya wazanzibari ndio maana tunataka Muungano wa Serikali 3.

Swali: Vyama vitahakisishaje Zanzibar haiachwi nyuma kwenye maswala ya huduma za kijamii?

ELIMU
Hamad Rashid (ADC):
Hakuna mwalimu wa Sayansi anayekaa Zanzibar kwa zaidi ya miezi 3; wengi hukimbilia Bara kutafuta maslahi.

Khamis Lila (ACT): Tuna walimu wa kutosha, wanafunzi wa kutosha lakini shule na vifaa vya kutosha ndiyo changamoto. Walimu hapa Zanzibar wamekosa uzalendo kwa kuwa wamekosa maslahi mazuri, sisi tutaboresha maslahi yao. Tutatoa huduma za jamii bila ubaguzi wowote kwa wananchi wa Zanzibar.

Walimu hapa Zanzibar wamekosa uzalendo kwa kuwa wamekosa maslahi mazuri, sisi tutaboresha maslahi yao. Tutatoa huduma za jamii bila ubaguzi wowote kwa wananchi wa Zanzibar.

Mohamed Rashid(CHAUMA):
Nilikosea nikasema mimi ni mgombea kupitia NCCR, naomba nirekebishe kuwa nipo CHAUMA. Sisi tutatoa huduma ya Afya bure; Majengo yatakarabatiwa; Vituo vya Afya hapa Zanzibar vitakuwa wazi masaa 24.

AFYA
Lila(ACT): Tutaboresha huduma ya Afya kwa kuwatenga wajawazito kwenda wodi maalum ya wazazi. Tutaweka utaratibu mzuri wa matibabu.

Hamad Rashid(ADC):
Bajeti inayoenda kwenye Sekta ya Afya ni ndogo sana. Ndilo tatizo la msingi kwa sasa!

SUALA LA OIC
Lila(ACT):
Kuhusu OIC tutataka kujua wananchi wanataka nini; tukiona kuna uwezekano wa kujiunga OIC tutajiunga, sio suala baya.

Hamad Rashid(ADC):
Suala la OIC ni miongoni mwa kero za Muungano... ADC itaanzia hapo!

Mohamed Rashid(CHAUMA):
Suala la OIC liko wazi, Zanzibar yenye mamlaka yake kamili hili ni suala dogo sana!

AJIRA
Hamad Rashid(ADC):
Zanzibar hakuna viwanda hasa vya kuzalisha ajira kwa vijana. ADC ikichaguliwa itajenga viwanda vya uzalishaji. Tuna tatizo la ajira hapa Zanzibar,tukiingia madarakani tutaitumia rasilimali ya Bahari kutengeneza ajira.

Lila(ACT): Kuna watu wamestaafu wanarudishwa kazini; vijana wengi wanakosa ajira sababu hii. Tutafufua pia viwanda vidogovidogo.

UCHUMI/KILIMO
Mohamed Rashid(CHAUMA): Tutatumia Jeshi la Kujenga Uchumi kuweza kuelimisha wananchi juu ya kilimo bora ili wapate kipato.

Lila(ACT): Tutawasaidia wakulima kuweka Hifadhi ya Jamii ili waweke akiba yao kwa faida ya baadae.

Hamad Rashid(ADC): Tutawafundisha wakulima jinsi ya kuweka akiba na tutahakikisha wanakuwa na bima.

UTALII
Lila(ACT): Tutaondoa vikwazo vidogovidogo kwenye sekta ya Utalii. Tutakuwa na mipango mizuri ili tufanye utalii wa kisasa.

Hamad Rashid(ADC)
: Sekta ya Utalii inaongoza kwa Zanzibar kwa kuingiza kipato. Watalii wakija wanahitaji Amani na Utulivu. Watalii wakija wanahitaji pia wakute Hoteli zinazoendana na viwango; wanataka walipe malipo kwa njia rahisi.

Tutaboresha njia za malipo kwa watalii ili kuweza kuvutia watalii zaidi. Tunautambua uwepo wa Mwenyezi Mungu. Nchi yetu inazo sheria lakini hazisimamiwi..

NAFASI YA WANAWAKE (JINSIA)
Hamad Rashid(ADC):
Tunahitaji usimamizi wa kutosha kwa sheria zilizopo ili unyanyasaji kwa wanawake (wa kijinsia) usiwepo.

Khamis Lila(ACT):
Tukiingia madarakani tutaisimamia Wizara ili iweze kufanya kazi zake vema. Tutaweka wanawake viongozi wasomi. Bila wanawake hata sisi tusingekuwepo, ni mama zetu na ni wake zetu.

RUSHWA
Mohamed Rashid(CHAUMA): Kitendo cha Polisi kuwa wanachukua rushwa ni kutokana na Utawala mbovu; tatizo linaanzia juu zaidi.

Khamis Lila(ACT):
Rushwa kwa Polisi inasababishwa na vishawishi, ugumu wa maisha... Wakiwezeshwa vema basi Rushwa itapungua!

Hamad Rashid(ADC): Tatizo la Rushwa ni kubwa; tuhuma dhidi ya rushwa zinatakiwa kufanyiwa kazi haraka, wahusika wasilelewe. Tutatumia teknolojia zilizopo kuweza kupambana na rushwa. Tutatumia utaratibu wa manunuzi kwa njia ya mtandao.

MAHAKAMA YA KADHI
Khamis Lila(ACT): Mahakama ya Kadhi ipo Zanzibar, hili halina mjadala; labda tuangalie jinsi ya kuiboresha tu.

Hamad Rashid(ADC):
Kenya, Uganda wana Mahakama ya Kadhi. Tanzania Bara kwa bahati mbaya mpaka sasa haijawa nayo. Mahakama ya Kadhi si mbaya, ni jambo la muhimu kwa Waislam na ni suala lililomo kwenye Kitabu Kitakatifu.

Mohamed Rashid(CHAUMA): Zanzibar inayo Mahakama ya Kadhi, kwa Bara napenda kuwambia kuwa ni haki ya msingi ya binadamu.

AMANI BAADA YA UCHAGUZI
Hamad Rashid(ADC): Tutalinda amani; tutaheshimu matokeo, tukidhulumiwa tutafuata taratibu zilizopo.Tunaviheshimu vyombo vya Dola.

Mohamed Rashid(CHAUMA):
Amani yetu ikitoweka, itatugharimu zaidi ya miaka 40 kuweza kuirejesha!

Khamis Lila(ACT):
Sisi hatupo tayari kusababisha vurugu wala kuivuruga amani iliyopo. Tukishindwa tutakubali matokeo!

WALEMAVU
Mohamed Rashid(CHAUMA): Tukipata madaraka tutawapa walemavu haki zao kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.

Khamis Lila(ACT): Tutawashughulikia walemavu kama tutakavyowashughulikia wananchi wengine. Tutawapa huduma wanazostahili.

Hamad Rashid(ADC): Bila mfumo mzuri wa Kisheria hata huduma nzuri kwa walemavu ni ngumu kutolewa. Tunatambua vipaji vya walemavu. Sisi kwetu walemavu wana nafasi ya kipekee, ni tofauti na kwa wenzangu walivyosema

MADAWA YA KULEVYA
Lila(ACT): Tukipata madaraka, tutapambana na wanaoingiza madawa ya kulevya; baadhi wanajulikana! Tutawafunga maisha hata kuwaua. Madawa ya Kulevya hapa Zanzibar yanaingia kwa kupitia Uwanja wa Ndege na Bandarini; tutayadhibiti maeneo haya.

Hamad Rashid(ADC)
: Zanzibar ni sehemu ndogo sana, ni rahisi kudhibiti wauza madawa. Tatizo ni Law Enforcement

Mohamed Rashid(CHAUMA): Kwa miaka 3 iliyopita kuna maendeleo mazuri kiasi ya upambanaji na madawa ya kulevya hapa Zanzibar. Sijawahi hata siku moja kusikia mtu kashtakiwa hapa Zanzibar wala kunyongwa kwa madawa ya kulevya.

SANAA NA MICHEZO
Hamad Rashid(ADC): Tunaamini Michezo na Sanaa ni soko linaloweza kuingiza kipato hapa Zanzibar. Tutatumia wataalam kuinua soko.

Mohamed Rashid(CHAUMA):
Mimi ni kiongozi wa mpira wa miguu. Ni wachezaji wangapi hapa Zanzibar wamesajiliwa Simba na Yanga?

Khamis Lila(ACT): Sanaa zetu lazima ziangalie mila zetu hapa Zanzibar, sio tunaiga tamaduni za magharibi..

MAFUTA NA GESI
Mohamed Rashid(CHAUMA):
Tukipata madaraka, tutaharakisha ndani ya miaka 2 tuanze kuchimba mafuta.

Khamis Lila(ACT): Tukiingia madarakani tutafanya utafiti kwanza kuhakikisha kama kweli mafuta yapo Zanzibar.

Hamad Rashid(ADC):
Tayari Zanzibar imeshaanza kuongea na SHELL juu ya uchimbaji mafuta; tukiingia madarakani tutaendeleza juhudi.

UMASIKINI
Mohamed Rashid(CHAUMA): Ili kupunguza umaskini, tutawashirikisha wananchi katika shughuli za maendeleo

Hamad Rashid(ADC): Kaya maskini sehemu kubwa zipo kwa wakulima. Ni kwa kuwa uzalishaji wao haujaboreshwa. Tutawapa pembejeo bure. Tutawalipa wafanyakazi kwa wanavyofanya kazi... Kwa taaluma zao, kazi wanazofanya na kuangalia mfumuko wa bei.

Hamad Rashid(ADC):
Tutawalipa wafanyakazi kwa wanavyofanya kazi... Kwa taaluma zao, kazi wanazofanya na kuangalia mfumuko wa bei.

Mohamed Rashid(CHAUMA):
Tutawalipa wafanyakazi wa kima cha chini USD 300, kwakuwa pesa yetu haina thamani.

SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA
Hamad Rashid(ADC):
Wananchi wa Zanzibar waliamua wenyewe kuwa Chama chochote kitakachoshinda kitashirikiana na kilichofuatia. Nadhani kuna haja tutoe uhuru kwa chama kinachoshinda kuchagua chama cha kushirikiana nacho hapa Zanzibar. Nadhani si jambo sahihi kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kutekeleza sera/ilani za chama kilichoshinda.

Mohamed Rashida(CHAUMA):
Tukipata madaraka tutaunda serikali itakayoshirikisha vyama vyote, dini zote na makabila yote.

Khamis Lila(ACT):
Tukishinda, tutaomba tubadilishe Katiba ya Zanzibar ili kurekebisha Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Mdahalo UMEKWISHA, tunawashukuru wote waliofuatilia; unaweza kufuatilia yaliyojiri kwa kina hapa...

==========

Kwa 'LIVE' updates zaidi tembelea JF Twitter account - https://twitter.com/JamiiForums


 

Attachments

  • MKIKIMKIKI - Washiriki Vyama [Zanzibar].jpg
    MKIKIMKIKI - Washiriki Vyama [Zanzibar].jpg
    69.7 KB · Views: 2,863
Last edited by a moderator:
Wameona bara mnauikanyaga kanyaga sasa waneanzia zanzibar....ingawa sisi ndo tuliotangulia kuanza kampeni...na tukishindwa kufanya mdahalo kwa wagombea wetu huku kwa sababu zozote I cant imagine how stupid are we?....
 
Labda swali moja tu kwa Maalimu SEIF SHARIF HAMAD, kwamba pamoja na kuwa kwenye serikali ya umoja wa kitaifa kwa kipindi chote cha miaka mi5, ukiachilia mbali limitation za katiba ya Zanzibar ya 2010 na nafasi kubwa ya kutoa ushauri wa moja kwa moja kwa rais wa Zanzibar, ni kipi kilichomzuia kutekeeza hayo anayoahidi leo, na kama kilimzuia kwa kiasi cha kuchelwesha maendeleo ya wazanzibar kwanini hakujiuzulu ili asubiri kupata ridhaa kamili ya wananchi 2015.........?
 
Swali hili ni kwa mgombea wa CUF maalim Seif Shariff Hamad:

Kwamba katika kampeni zako moja ya jambo unalosisitiza sana ni kuwa iwapo utachaguliwa kuwa Rais wa serikali ya mapinduzi Zanzibar utahakikisha kuwa unaona Zanzibar yenye mamlaka kamili inapatikana.

Hebu tunaomba utufafanulie Zanzibar yenye mamlaka kamili ni ipi hiyo tofauti na hii ya sasa ambayo wewe ni mmoja wa viongozi wake waandamizi ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa katika nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais? Na je, hayo mamlaka mengine yalibaki wapi baada ya mapinduzi ya mwaka 1964 ya kuung'oa utawala wa kisultani hata kuifanya Zanzibar isiwe mamlaka yake yaliyokamilika? Asante naitwa Kitaturu wa Jamii Forum
 
Labda swali moja tu kwa Maalimu SEIF SHARIF HAMAD, kwamba pamoja na kuwa kwenye serikali ya umoja wa kitaifa kwa kipindi chote cha miaka mi5, ukiachilia mbali limitation za katiba ya Zanzibar ya 2010 na nafasi kubwa ya kutoa ushauri wa moja kwa moja kwa rais wa Zanzibar, ni kipi kilichomzuia kutekeeza hayo anayoahidi leo, na kama kilimzuia kwa kiasi cha kuchelwesha maendeleo ya wazanzibar kwanini hakujiuzulu ili asubiri kupata ridhaa kamili ya wananchi 2015.........?

Akitoa ushauri huo lakini sio lazima kufatwa. Yeye ni boya tu lakini hana mamlaka yoyote. Ni ile kuwa kuna serikali ya msetto kuondoa chuki lakini serikali ni ya sheni na ccm
 
Swali hili ni kwa mgombea wa CUF maalim Seif Shariff Hamad:

Kwamba katika kampeni zako moja ya jambo unalosisitiza sana ni kuwa iwapo utachaguliwa kuwa Rais wa serikali ya mapinduzi Zanzibar utahakikisha kuwa unaona Zanzibar yenye mamlaka kamili inapatikana.

Hebu tunaomba utufafanulie Zanzibar yenye mamlaka kamili ni ipi hiyo tofauti na hii ya sasa ambayo wewe ni mmoja wa viongozi wake waandamizi ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa katika nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais? Na je, hayo mamlaka mengine yalibaki wapi baada ya mapinduzi ya mwaka 1964 ya kuung'oa utawala wa kisultani hata kuifanya Zanzibar isiwe mamlaka yake yaliyokamilika? Asante naitwa Kitaturu wa Jamii Forum

Jawabu znz ilikua nchi .
Ilikua memba wa UN
Memba wa Cimmonwealth
Memba wa W.Bank
Memba wa IMF.
Iliweza kukopa na kukopesha
Ilikua na Bank kuu yake


Sasa hivi vyote havipo na imebaki mkoa na yeye ni sawa na mkuu wa wilaya
 
1. Viongozi wanaogombea Zanzibar, wamejipangaje kudumisha Umoja wa Kitaifa na Aman ya Zanzibar.

2. Ilani za vyama vya Siasa, zinazungumziaje Muungano?

3. Nìni Mtizamo wa vyama vya siasa juu ya Mafuta na gesi ya Zanzibar?.
 
Swali:
Viongozi wa Nzanzibar, Wanzanzibar wamekuwa wakihitaji kujitawala wao wenyewe na wamekuwa hawahitaji muungano.Je nyinyi kama wagombea wa Zanzibar mtafanyaje kuwashawishi Wanzanzibar waendelee kupenda muungano Tanzania na Zanzibar udumu?
 
Hivi ni kwanini Wazanzibari wanataka kuwa na uhuru wa kujitawala na uwepo wa serikali tatu?
 
Leo Jumapili Septemba 20, 2015 midahalo ya Mkikimkiki inaendelea na inalenga kuvipa vyama vyote fursa ya kunadi Ilani zao na kwa wananchi kuuliza maswali muhimu yatakayo pelekea maamuzi yao katika uchaguzi.

Mkikimkiki‬ iko Zanzibar Jumapili hii na waalikwa ni wagombea urais wa vyama vitano ambavyo ni CCM, CUF, ADC, CHAUMMA na ACT-Wazalendo Kushiriki ni kwa mwaliko tu! Tuwe sote kujuzana yatakayojiri kutoka visiwani.

Pia Midahalo hii itarushwa moja kwa moja na Star TV na Redio RFA saa nane kasoro robo mchana.

TUWAHOJI, TUWACHAMBUE, TUWAPIME!!
===========

20150920034610.jpg

Wageni wetu leo ni Khamis Idd Lila kutoka ACT wazalendo, Hamad Rashid ambae ni mgombea wa ADC, Mohammed Rashid kutoka CHAUMA, Tulitoa mwaliko kwa CCM na ukakubaliwa na CCM lakini mgombea alikataa kwa sababu za itifaki na Hamad Rashid alitoa sharti la kuwepo Shein ili awepo.

Swali: Watu wa bara na Zanzibar hawapendi muungano lakini Zanzibar kuna wito wa kujitawala, tunawezaje kuimarisha umoja wa kitaifa takwimu hizi!

Lila ACT
: wazelendo haifikirii muungano kwa sababu jamii hizi zimeshaungana sana, kuvunja inaweza kuleta vurugu labda watu wataambiwa kila mtu arejee kwao, faida ya muungano unaenda popote na huulizwi na mtu wala kubugudhiwa, ACT wazalendo hatuko tayari kabisa kusikia muungano unavunjika

Hamad Rashidi
: Nasikitika wengine wameshindwa kufika japo wapo kwenye serikali pamoja, msingi wetu tunaamini uwepo wa mwenyezi Mungu, takwimu zinatatanisha kwa sababu tume ya warioba wazanzibari wengi wanataka serikali ya mkataba.

Mfumo wa serikali unatokana na matakwa ya wananchi na si maamuzi ya vyama kupitia kura ya maoni, lazima waheshimu matakwa ya wananchi na ADC itaheshimu mwatakwa ya wananchi. Pia umoja ni nguvu.

Mohammed Rashid CHAUMA
: Ni mgombea urais kupitia chama CHAUMA, muungano uliokuwepo katiba haiitambui Zanzibar kama nchi ndio maana wazanzibari wengi hawajinasibishi na muungano. Kuwe na serikali tatu ya Zanzibar, Bara na Muungano na kila mtu atajivunia utanzania wetu. Serikali iliyokuwepo ya muungano inawanyonya wazanzibari kwenye hasa kwenye kodi ambayo ndio tegemeo la Zanzibar.

Swali
: Kwenye huduma za jamii inaonekana Zanzibar imegawanyika ndani yake, tunawezaje kuhaahkisha Zanzibar hamna sehemu inayoachwa nyuma.

Mohammed Rashid Cha msingi kwanza ni kupambana na changamoto ya kielimu iwe sawa kwa sehemu zote, maslahi ya Pemba yako chini kuliko Unguja au Dar es Salaam, inajenga tabaka katika jamii.

Mohammed Rashid CHAUMA Sisi upande sera wananchi itashika hatamu, tunataka kutoa elimu bora na sio bora elimu, sisi tutaboresha elimu ili tupate huduma zilizokuwa bora. Kutoka nursery mpaka chuo kikuu itakuwa ni bure na kumpa ajira ili arejeshe taratibu.

Khamis Lila ACT wazalendo inaamini uzalendo umekosekana kwenye nchi, walimu wapo wa kutosha lakini vifaa vya kufundishia tatizo, ACT tutaleta vifaa vya kisasa na kuangalia maslahi ya walimu na kuongeza motisha. Madaktaeri tunao wa kutosha lakini maslahi na madawa yanatakiwa kuangaliwa vizuri na tutasimamia huduma hizi zisiwe na ubaguzi vijijini na mijini. Tutahamasisha wazee wakae na watoto wao wanapotoka shule.

Farida Haji: Huduma za afya badi haziridhishi, ukipata nafasi utafanya nini

Afya ya wazanzibari iko mbaya sana, sisi kwanza wanawake watazalishwa na wanawake wenzao na sio wanaume, afya kwa ujumla wake majengo yanafungwa saa nane na wikiendi linafungwa wakati maradhi hayana miadi, tutayafungua masaa 24.

ACT Tutashughulikia wodi maalum ya wazazi na tutakuwa na wakunga maalum kwa sababu hii ni kazi kubwa, bila huduma nzuri tutamkosa mtoto na kupungukiwa na nguvu ya taifa la kesho pia itakuwa ni bore na mama haendi na kitu mkituchagua serikali ya ACT wazalendo

Hamad Rashid Tunamjali mama anapokuwa mjamzito lakini la msingi hapa ni bajeti na bajeti inayoenda kwenye afya ni ndogo sana, kuwapatia nyumba bora wananchi zenye maji na huduma zote za msingi kuepusha maradhi ya milipuko na wanafunzi wote watapimwa na kuelimishwa.

Swala la OIC
Khamis Lila: Kama kuna fursa ya kujiunga na OIC tutajiunga lakini tutakaa kwanza kwenye baraza la wawakilishi na likiwezekana tutajiunga

Hamad Rashid
: Ni moja ya kero kubwa na kwenye tume ya jaji Warioba walishaondoa kwenye muungano hivyo ni swala la kupitisha sheria tu na tutatumia taasisi zetu za sheria kutunga taasisi hio na sisi tuko tayari haina tatizo lolote.

CHAUMA
: Mimi nimefurahi sana na kwenye serikali tatu Zanzibar itakuwa na mamlaka kamili na hilo litakuwa suala dogo sana kwa mujibu wa katiba.

Omari Shabani; Nataka kujua mipango ya wagombea katika kukuza na kuboresha sekta ya utalii Zanzibar

Khamis Lila; ACT tumetizama eneo hili, kwanza ni kuondoa vikwazo vidogo vidogo na kusimamia mapato ya utalii, tutaboresha utalii uli tupokee watalii na pato la taifa liongezeke.

Hamad Rashid; Kwanza tunatambua ndio sekta inayoingiza pesa nyingi hapa Zanzibar, lazima tuhakikishe usalama na pia tuziangalie hoteli pia tutaangaloia electronic payments bila ya kusumbuka kwenda ubalozini pia itaondoa upotevu wa mapato.

CHAUMA; Tunaangalia sehemu ya wananchi na investors, mikataba haiko sawasawa na kusababisha malumbano mengi. Mwenye ardhi pia apate pato mwaka hadi mwaka. Utalii ni nguzo moja ya uchumi katika nchi hii hivyo tutaifanya iwe transparent na serikali kuu ipate mapato bila kumtuma mtu kwenda physically kuepusha upotevu wa mapato.

Salma Ayoub; Endapo mtafinikiwa mtasaidia vipi kuhakikisha wanawake wanapata haki zao

Hamad Rashid; ADC tunatambua hizi haki za wanawake, zipo sheria lakini hazisimamiwa na law enforcement ina tatizo na zikisimamiwa vizuri mambo yataenda vizuri na watu wapate haki zao. Bila utawala wa sheria haki ni ngumu kupatikani.

Mohammed Rashid; Wanawake tunawapa kipaumbele ndio maana kwenye chama chetu wagombea wengi ni wanawake, NSSF mwanamke akienda kujifungua analipwa milioni moja kabla na baada lakini ZSSF analipwa elfu 40 na nasikia siku hizi wameongeza mpaka elfu 80 baada ya kelele nyingi.

Khamis Lila:Tutawachagua wanawake waongoze wizara ya wanawake na tutaisimamia hiyo wizara kuhakikisha haki inatendeka na wanazipata haki zao wanawake.
 

Attachments

  • 20150920034531.jpg
    20150920034531.jpg
    75.2 KB · Views: 91
  • Mkiki.jpg
    Mkiki.jpg
    49.7 KB · Views: 89
  • unnamed.jpg
    unnamed.jpg
    49.1 KB · Views: 106
Kituo gan mkuu cha telavisheni kitakuwa live na ni SAA ngap
 
Leo Jumapili Septemba 20, 2015 midahalo ya Mkikimkiki inaendelea na inalenga kuvipa vyama vyote fursa ya kunadi Ilani zao na kwa wananchi kuuliza maswali muhimu yatakayo pelekea maamuzi yao katika uchaguzi.

Mkikimkiki‬ iko Zanzibar Jumapili hii na waalikwa ni wagombea urais wa vyama vitano ambavyo ni CCM, CUF, ADC, CHAUMMA na ACT-Wazalendo Kushiriki ni kwa mwaliko tu! Tuwe sote kujuzana yatakayojiri kutoka visiwani.

TUWAHOJI, TUWACHAMBUE, TUWAPIME!!

Duh!! Ina maana CCM miaka yote hii ilikuwa inakwepa midahalo sababu ya JK???????? Uwezo wa huyo jamaa kweli uk chini duh!!!
 
CCM wanakimbia midahalo,na leo shein angekuwepo angeipata fresh.
 
Back
Top Bottom