Mdogo wa mke wangu (binti) amenidharau na kunitukana mbele ya mke wangu

Mdogo wa mke wangu (binti) amenidharau na kunitukana mbele ya mke wangu

Hiyo issue ya kugawana mali boss ni yakisheria ,sio ya kidini mzee upo? Sasa ww kama muislam siku puyanga uoe demu feminist au ana washkaj zake wanaharakati flani hivi utaelewa sasa,demu akisha jua tu sheria zikoje basi umeisha kweny Hilo,Mbona huku mtaani ndoa za kislam hzo hzo watu wanapigana 50% percent kila siku.
Utakubaliana na me kwambwa wanawake wakikristo tamaa ya mali zimewajaa san najua fika kama ishu ya kugawan mali ni ya kisheria ata kidini pia ipo ivo ukiachan na mwenza wako zile mali mlizochuma mkiwa pmj baada ya ndoa zinafaa kugaiwa pasu kwa pasu ila hukuti wanawake wa kiislamu kuwa na tamaa iyo ndio maana Bugatti anaoa kila leo 😂😂😂
 
Kaka hao ni wajita Amna mkurya wa hivyo aisee. Hizo ni tabia za kijita ndo baba mkwe anaweza kwenda kwa binti yake akakaa ata mwaka lakini sio mkurya

Sema nini na wajita ninao wajua Mimi wanatabia ya kuroga wanaume sio mkurya

Sas fanya hivi mkalishe mkeo umuulize nilichokisikia kutoka kwa ndugu yako ni sahihi na wew unaitaji iwe Ivo tena ongea nae kwa upole tu

Akikujibu ndio basi usipoteze mda achana nae, akikujibu hapana mpige marufuku kukanyaga dukani tena ikibidi ilo duka uza si umesema wew ni mwajiliwa uqezi kukuosa pesa ya matumizi nyumbn. Yeyeabaki kuwa mama wa nyumbani tu aleee watoto
Yes uko sahihi...Baba mkurya hakai kwa mkwewe hata siku 1
 
Wakuu naomba ushauri.

Mimi ni mkazi wa Morogoro ninaishi kwenye nyumba yangu niliyotafuta pamoja na mkewangu. Baada ya wahitimu kumaliza chuo mwaka huu mke wangu aliniomba mdogo wake aje kuishi nasi pamoja.

Sasa baada ya kipindi kupita mke wangu ameonesha ukaribu sana na mdogo wake ikafika mpaka kumueleza mengi juu ya maisha yetu ndani.

Kisa
Jana nilienda dukan kwetu na mke wangu (duka la vipodozi), lengo kumfuata shemeji na kupiga hesabu na kufunga duka. Dakika chache mke wangu alipokea simu kutoka kwa baba yake mazazi akimuomba aje aishi nyumbani kwangu.

Walikubaliana wao yeye na baba yake mzazi akiwa na mdogo wake na hata akaamua kumtumia nauli bila ya mimi kuhusishwa chochote. Ikumbukwe yote haya yanafanyika dukani tukiwa wote watatu namaanisha mimi, mke wangu na shemeji. Baada ya hili zoezi kuisha ndipo mke wangu ananieleza kuwa "Baba atakuja kesho na nimeshamtumia na nauli"

Mi nikamjibu kwa njia ya ujumbe wa simu, "Unaniambia ama unanipa taarifa?" Baada ya hii kauli alinuna na kukasirika sana na kuamua kuongea Kikurya yeye na mdogo wake (mimi mchaga). Mimi hapo sielewi kitu ila nyuso zao ni kama wamefura kwa hasira.

Dada mtu aliamua kurudi nyumbani kwa pikipiki, mdogo mtu (shemeji) alibaki dukani na kufunga hesabu. Baada ya muda kidogo niliwasha gari na kuelekea nyumbani. Nilipofika nyumbani sasa nikamuuliza mke wangu kwanini umekasirika kwa ujumbe kama ule angali sijaandika tusi?

Ailinijibu we niache kwanza, ushamzika baba yako hivyo huna cha kupoteza. Mimi nikamwambia taswira kama hiyo unanijengea picha mbaya kwa mdogo wako, maana yanayoongeleka ni mengi sana hasa juu ya mimi na wewe.

Maana unayomueleza nduguyo huwaeleza hata watu wa karibu. Dah, baada ya kusema hivyo akampigia simu mdogo wake na kumwambia shemeji yako anasema wewe huwa una muongelea vibaya hapo dukani kwa watu wake wakaribu.

Alifunga duka na akarudi nyumbani spidi ya jeti na kunikuta sebulen nimekaa naperuzi JF. Kwanza alipofika tuu nyumbani aligonga mlango kwa nguvu sana kana kwamba kuna mtu ana tuvamia. Alipotimba sebulen akaanza kwa kusema ilikuwaje mkanizungumzia mimi na hao marafiki (majirani wa dukani) zako?

"Halafu shemeji unajua wewe ni mnafiki sana? Unadhani matendo yako kwa dada siyaoni humu ndani? Ujue shemeji wewe una roho mbaya sana, naishi na wewe kwa kukuvumilia sana?Nlisha kudharau sana.

He he..he! Nlibaki nashangaa sana, kwanza ni mtoto mdogo sana kwangu, ni wa mwaka 98. Mwisho akasema bhana eeh kama vipi andika talaka kwa mkeo mgawane mlivyo chuma kila mtu asepe zake (shemeji huyo)! Hata dada yake hakuwahu kutamka maneno kama haya asee.

Wakuu, mimi nimeamua asepe kwao ifikapo Jumatatu ya tarehe 17, October. Japo mke anakuwa kama anajiuliza sana haya maamuzi yangu.

Pia msaada tafadhali maana nina mawazo sana kuhusu huyu dogo mwenye Degree ya Biashara, halafu pia ndugu lakini sina namna.

Nawasilisha.
Ukiona democracy haifanyi kazi Nyumbani kwako,jaribu udikiteta!!
 
Mkuu tatizo hapo ni wewe. Kwa sababu umemjengea shemeji yako kujua kua hapo ni kwa dada yake na sio kwako.

Na ndio maana ana uwezo wa kukutukana na kukwambia umpe dada yake talaka mgawane Mali.

Na ndio maana hata mahamuzi ya baba yao kuja hapo wewe ujashirikishwa.

Kama wewe ndo baba mwenye nyumba hakuna mtu au ndu anaweza kuja hapo bila wewe kukubali. So go back angalia ulipogikwaa upasawazishe.
 
Weka picha ya huyo shemeji yako hapa, ma..ma.e angekula kichapo cha nguvu yeye na dada yake na angelala nje sema mkeo pia inaonekana anatoa profile yako kizembe hii kwangu No staki kukaa na mtu zaidi ya wanangu mkwe apambane huko nililipa mahali/ brideworthy kwisha
 
Kaka hao ni wajita Amna mkurya wa hivyo aisee. Hizo ni tabia za kijita ndo baba mkwe anaweza kwenda kwa binti yake akakaa ata mwaka lakini sio mkurya

Sema nini na wajita ninao wajua Mimi wanatabia ya kuroga wanaume sio mkurya

Sas fanya hivi mkalishe mkeo umuulize nilichokisikia kutoka kwa ndugu yako ni sahihi na wew unaitaji iwe Ivo tena ongea nae kwa upole tu

Akikujibu ndio basi usipoteze mda achana nae, akikujibu hapana mpige marufuku kukanyaga dukani tena ikibidi ilo duka uza si umesema wew ni mwajiliwa uqezi kukuosa pesa ya matumizi nyumbn. Yeyeabaki kuwa mama wa nyumbani tu aleee watoto
aliye oa anakwambia mkulya, wewe unaleta ujuaji mwingine kukataa

wapi kasema baba mkwe amekuja kukaa mwaka.

wafundisheni dada zenu wakulya tabia njema, sio kusingizia makabila mengine

ama ndo ile unaambiwa mtoto wako ana tabia chafu unakataa na kusingizia wamemfananisha atakuwa wa jirani
 
W
Utakubaliana na me kwambwa wanawake wakikristo tamaa ya mali zimewajaa san najua fika kama ishu ya kugawan mali ni ya kisheria ata kidini pia ipo ivo ukiachan na mwenza wako zile mali mlizochuma mkiwa pmj baada ya ndoa zinafaa kugaiwa pasu kwa pasu ila hukuti wanawake wa kiislamu kuwa na tamaa iyo ndio maana Bugatti anaoa kila leo 😂😂😂
anadai ila mnawadhulumu, tunaishi nao huku lindi tunayaona
 
Ulishawahi Mpa kipigo Mkeo?.

Kama ni hapana...tatizo Hilo.


Wakurya ninawaelewa sana, Wanawake wao Wana dharau, jeuri, ubabe.

Kadiri unavyowapa kipigo, ndivo wanakuona mwanaume .


Ungekua ushampiga, huyo Mdogo mtu angekua anakuogopa kama ukoma.


Hata Ivo nikupongeze sana, Wewe no mwanaume, Kuna wakati, kua chini hakumaanishi wewe ni Mdhaifu, Sasa basi, MDOGO MTU AONDOKE HIYO JUMATATU

NARUDIA, AONDOKE, AENDE KWAO TARIME
 
Utakubaliana na me kwambwa wanawake wakikristo tamaa ya mali zimewajaa san najua fika kama ishu ya kugawan mali ni ya kisheria ata kidini pia ipo ivo ukiachan na mwenza wako zile mali mlizochuma mkiwa pmj baada ya ndoa zinafaa kugaiwa pasu kwa pasu ila hukuti wanawake wa kiislamu kuwa na tamaa iyo ndio maana Bugatti anaoa kila leo [emoji23][emoji23][emoji23]
Mimi nakataa ,Nishakutana na kesi nyingi za hao jamaa zangu waislam wengine wamestop mpaka kuachana baada ya kuskiaa wake wana mipango ya kugawana mali.

Mzee Ndomana nikasema uoe tu mwanamke asiekua na uelewa wa sheria hizo,lakini hawa wa sasa sio waislam wala wakristo, hivi unajua agenda wanazopush mafeminist kweny groups zao zile?

Bugatti yule ni mtu ambae ana washkaji zake wenye uelewa na sheria, hivyo anajua kufanya protection ya mali zake kabla hajaoa, mwenzangu na mimi utajua hata kufanya cohabitation agreements? Pre nuptials agreement?

Mkeo akikuburuza mahakamani basi hutoboi,Ukisoma vizur family law utaona kabisa sheria inambeba Mwanamke,na baadhi ya nchi anakula 75% ya mali.

Hivyo basi omba tu usikutane na mwanamke anejua haya mambo,hakuna mwanamke asietaka mali ikitokea devorce,sema wengine hawajui hayo mambo,na ndio maana feminism inahubiri hilo kuwapa elimu..Hapo hakuna cha dini ,ni mwanamke mwenyewe tu.

NB nakukumbusha, Mwanamke unae achana nae Sio Mwanamke uliemuoa [emoji2]
 
Wakuu naomba ushauri.

Mimi ni mkazi wa Morogoro ninaishi kwenye nyumba yangu niliyotafuta pamoja na mkewangu. Baada ya wahitimu kumaliza chuo mwaka huu mke wangu aliniomba mdogo wake aje kuishi nasi pamoja.

Sasa baada ya kipindi kupita mke wangu ameonesha ukaribu sana na mdogo wake ikafika mpaka kumueleza mengi juu ya maisha yetu ndani.

Kisa
Jana nilienda dukan kwetu na mke wangu (duka la vipodozi), lengo kumfuata shemeji na kupiga hesabu na kufunga duka. Dakika chache mke wangu alipokea simu kutoka kwa baba yake mazazi akimuomba aje aishi nyumbani kwangu.

Walikubaliana wao yeye na baba yake mzazi akiwa na mdogo wake na hata akaamua kumtumia nauli bila ya mimi kuhusishwa chochote. Ikumbukwe yote haya yanafanyika dukani tukiwa wote watatu namaanisha mimi, mke wangu na shemeji. Baada ya hili zoezi kuisha ndipo mke wangu ananieleza kuwa "Baba atakuja kesho na nimeshamtumia na nauli"

Mi nikamjibu kwa njia ya ujumbe wa simu, "Unaniambia ama unanipa taarifa?" Baada ya hii kauli alinuna na kukasirika sana na kuamua kuongea Kikurya yeye na mdogo wake (mimi mchaga). Mimi hapo sielewi kitu ila nyuso zao ni kama wamefura kwa hasira.

Dada mtu aliamua kurudi nyumbani kwa pikipiki, mdogo mtu (shemeji) alibaki dukani na kufunga hesabu. Baada ya muda kidogo niliwasha gari na kuelekea nyumbani. Nilipofika nyumbani sasa nikamuuliza mke wangu kwanini umekasirika kwa ujumbe kama ule angali sijaandika tusi?

Ailinijibu we niache kwanza, ushamzika baba yako hivyo huna cha kupoteza. Mimi nikamwambia taswira kama hiyo unanijengea picha mbaya kwa mdogo wako, maana yanayoongeleka ni mengi sana hasa juu ya mimi na wewe.

Maana unayomueleza nduguyo huwaeleza hata watu wa karibu. Dah, baada ya kusema hivyo akampigia simu mdogo wake na kumwambia shemeji yako anasema wewe huwa una muongelea vibaya hapo dukani kwa watu wake wakaribu.

Alifunga duka na akarudi nyumbani spidi ya jeti na kunikuta sebulen nimekaa naperuzi JF. Kwanza alipofika tuu nyumbani aligonga mlango kwa nguvu sana kana kwamba kuna mtu ana tuvamia. Alipotimba sebulen akaanza kwa kusema ilikuwaje mkanizungumzia mimi na hao marafiki (majirani wa dukani) zako?

"Halafu shemeji unajua wewe ni mnafiki sana? Unadhani matendo yako kwa dada siyaoni humu ndani? Ujue shemeji wewe una roho mbaya sana, naishi na wewe kwa kukuvumilia sana?Nlisha kudharau sana.

He he..he! Nlibaki nashangaa sana, kwanza ni mtoto mdogo sana kwangu, ni wa mwaka 98. Mwisho akasema bhana eeh kama vipi andika talaka kwa mkeo mgawane mlivyo chuma kila mtu asepe zake (shemeji huyo)! Hata dada yake hakuwahu kutamka maneno kama haya asee.

Wakuu, mimi nimeamua asepe kwao ifikapo Jumatatu ya tarehe 17, October. Japo mke anakuwa kama anajiuliza sana haya maamuzi yangu.

Pia msaada tafadhali maana nina mawazo sana kuhusu huyu dogo mwenye Degree ya Biashara, halafu pia ndugu lakini sina namna.

Nawasilisha.
MKIAMBIWA MSIOE MUWE MNAELEWA

TABU zote za nini hizi
 
ni mtoto mdogo sana kwangu, ni wa mwaka 98. Mwisho akasema bhana eeh kama vipi andika talaka kwa mkeo mgawane mlivyo chuma kila mtu asepe zake (shemeji huyo)! Hata dada yake hakuwahu kutamka maneno kama haya asee.
mkuu, kwanza pole sana!

nahisi haujawahi kupiga mwanamke kwenye maisha yako kwa kijinsi mambo yanavyokustaajabisha... ni jambo jema!

ila nimekuja kugundua dunia hufundisha watu! huyo shemeji atarudi kukuomba msamaha, acha akaolewe na mtu ambaye hataki porojo ndani ya nyumba yake!

na hilo swala la guwana mali na wife inaonekana wameshaliongea ukizingatia kuwa wife anashare mambo ya ndani yenu!

swali ni kwamba, wakisimama pamoja upo tayari kuwa msela tena? kwani kwa spidi ya shemeji yako na mambo kuchukuliwa kwa uwepesi ndani ya nyumba yako, wakati wowote kuna jambo litaibuka!

jikaze, weka mguu chini! ila utakapofanya hili, ujue unaweze kuanzisha mengine!

kama wewe sio mtu mkali, tuliatuli kwani hua dunia ina adabisha watu.

karma husaidia wanyonge!

Unaelewa maana ya karma?
 
Tumia ubabe tu timua wote ndani ya nyumba.

Huyo mkeo mpe muda atarudi kwenye default factory settings
 
Utakubaliana na me kwambwa wanawake wakikristo tamaa ya mali zimewajaa san najua fika kama ishu ya kugawan mali ni ya kisheria ata kidini pia ipo ivo ukiachan na mwenza wako zile mali mlizochuma mkiwa pmj baada ya ndoa zinafaa kugaiwa pasu kwa pasu ila hukuti wanawake wa kiislamu kuwa na tamaa iyo ndio maana Bugatti anaoa kila leo [emoji23][emoji23][emoji23]

Mahakamani talaka na haki zake haziangalii dini.
 
Jitahidi uwe na kipato chako tofauti na hivyo vipodozi vya mkeo
Nahisi hapa ndio chanzo cha yote hayo. Mtu hadi anakaa kijiweni karibu na anapofanya kazi shemeji yake na kuteta na watu wa kijiweni kuhusu shemeji yake, je alikuwa anatafuta nini?
 
Kwanza biashara yenu

Sheme anaendaje kufunga hesabu? Au mkeo kakuzidi Mali?

Kuna mazingira umetengeneza mpaka mwanamke anakua na ujasiri wa kukufanyia vituko
 
Back
Top Bottom