Ni mtoto wa baba yangu mdogo, anafanya kazi kwenye Embassy fulani (jina la Embassy kapuni), ila ana umri mdg bado na ni mlimbwende sana!
Sasa nimetoka zangu church muda si mrefu, baada ya kupata breakfast nikawa nashushia na ka-juice baridiii!
Nikaanza kumuona ananisogelea, mara ooh kaka nikudokeze jambo? nikamwambia go ahead. Amenizoea ndio, ila leo naona kama kavuka mipaka!
Akaanza ooh kaka jana nilikua Igoz Lounge, kuna mkaka alikua pembeni yetu nikamuelewa sana!!! Nikamuuliza anaposema anamuelewa anamaanisha nini?
Akasema amempenda! nikapigwa na butwaa! Akaendelea kusema eti amempendea perfume aliyokua amepulizia na ana uso wa upole!
Sasa to cut the long story short, we jamaa uliyekutana na mdg wangu jana, kama umo humu naomba uwe mstaarabu, kama umempenda kweli fuata taratibu. Ndio mdg wangu ameshakua mtu mzima lkn sipendi achezewe ktk umri mdg huu, she has a long way to go.
Unafanya kazi CBA, umemuachia business card, ulimkuta dogo na rafiki zake wanakunywa peroni ukataka kuwaagizia wakashukuru tu hawakukubali.
Mimi ni lawyer sasa kama unataka kupotezwa upuuzie haya maneno yangu, nimeshatoa 'disclaimer', jina lako ninalo hapa kwenye hii business card yako, sawa umependwa lkn uje nyumbani ufate taratibu tukupe mke, nimefunguka makusudi kwamba dogo kakupenda ingawa hakukwambia, coz nikificha huenda madhara yakawa makubwa zaidi.
Hata kama haumo humu naomba uzi huu uwe fundisho kwa wengine.
A.C