DENLSON
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 949
- 1,260
Wasalaam,
Leo tarehe 28 Juni 2021 Mahakama amemuachia huru aliyekuwa mtuhumiwa wa kosa la kuuza madawa ya kulevya.
Sitagusia juu ya kesi au namna ushahidi ulivyotolewa ila nataka kuongelea msimamo alionao Mdude Nyangali mwanachama mtiifu wa CHADEMA hata akajiita MDUDE CHADEMA.
Taifa linahitaji vijana wengi kama yeye. Ni kijana jeuri mwenye msimamo usioyumba wala kuteteleka labda kama Nelson Mandela.
Leo baada ya kuachiwa moja kwa moja ameongelea suala la Katiba Mpya. Ni watu wachache sana wenye ujasiri wa Mdude ambao bado wanaishi.
Fikiria wale vijana jeuri wa Magufuli leo wanavyo mkana hadharani? Kama wameshindwa kulinda falsafa za Magufuli kwa siku 100 tu wanaweza kusimamia misimamo yao binafsi pasipo mbeleko ya dola?
Mh. Rais unahitaji vijana aina ya Mdude kwenye Serikali yako. Wapime hata kwa moto na njia ni nyepesi tu kama huijui soma kitabu cha Daniel utaelewa ninachosema.
Ukipata vijana 10 kama Mdude unakuwa na uhakika juu ya falsafa ya chama/nchi itakuwa hai hata ukifa, huitaji kutumia fedha au nguvu kulinda legacy ukiwa na watu aina ya Mdude.
Kwa sasa Mdude Nyagali ni Nelson Mandela wa kizazi hiki.
Leo tarehe 28 Juni 2021 Mahakama amemuachia huru aliyekuwa mtuhumiwa wa kosa la kuuza madawa ya kulevya.
Sitagusia juu ya kesi au namna ushahidi ulivyotolewa ila nataka kuongelea msimamo alionao Mdude Nyangali mwanachama mtiifu wa CHADEMA hata akajiita MDUDE CHADEMA.
Taifa linahitaji vijana wengi kama yeye. Ni kijana jeuri mwenye msimamo usioyumba wala kuteteleka labda kama Nelson Mandela.
Leo baada ya kuachiwa moja kwa moja ameongelea suala la Katiba Mpya. Ni watu wachache sana wenye ujasiri wa Mdude ambao bado wanaishi.
Fikiria wale vijana jeuri wa Magufuli leo wanavyo mkana hadharani? Kama wameshindwa kulinda falsafa za Magufuli kwa siku 100 tu wanaweza kusimamia misimamo yao binafsi pasipo mbeleko ya dola?
Mh. Rais unahitaji vijana aina ya Mdude kwenye Serikali yako. Wapime hata kwa moto na njia ni nyepesi tu kama huijui soma kitabu cha Daniel utaelewa ninachosema.
Ukipata vijana 10 kama Mdude unakuwa na uhakika juu ya falsafa ya chama/nchi itakuwa hai hata ukifa, huitaji kutumia fedha au nguvu kulinda legacy ukiwa na watu aina ya Mdude.
Kwa sasa Mdude Nyagali ni Nelson Mandela wa kizazi hiki.