Mechi ligi Kuu Bara: Mbao FC na Simba SC zatoshana nguvu, Kirumba

Simba kwa visingizio hamjambo!!! Kubali ukweli kuwa huo ndio uwezo wenu Mkuu.
 
Uwanja uliinama na Okwi hakucheza ndo maana mmetoka sare. Hiyo ndo ligi baba.
 
Wadau wa simba poleni sana msipende kutukana mamba kabla ya kuvuka mto. Leo kikosi cha 1.6bl kimedhibitiwa vilivyo na kikosi kisicho zid ml150 au okwi hakucheza Jana nini? tunajua mmewaweka kambi ndanda morogoro ili kuifunga yanga lakin kwa taarifa yenu ndanda hachomoki mpira hauchezwi kwa fitina mpira uwanjan tukutane kesho shamba la bibi wakati napotoa kichapo kikali cha Mwana ukome .
 
Ule mgoli wa jana nilidhani bwana kim amemtupia kombora mapanki
 
THIS IS SIMBA BWANA, HAHAAAAAAA (In Manara's voice)
 
Waliopwaya mechi ya mbao fc.
Beki Shabalala,
magoli yote yamepitia kwake, anajiamini sana hadi anazarau pasi anazopewa, na kuokonywa mpira kirahisi na kufunga.

Kipa Manula.
Naye alijisahau sana na kuwa nje ya move za mpira.
Magoli yote amefungwa toka mbali na alikuwa hafuatilii mchezo, ni kama alizubaa na kudhani mchezaji hawezi kuupiga mpira.

Suluhisho.

Shabalala nadhani hajawa fiti bado hivyo anaogopa kuumia.
Erasto nyoni au Mwambeleko acheze namba 3 hadi Shabalala atakapokuwa fiti, 2 acheze Mbonde, 4 Juuko, 5 Mwanjali.

Kipa aliyesajiriwa toka timu ya Mbao fc, acheze badala ya Manula kwani ni mzuri sana golini na ana nguvu kupita manula. Acheze hadi Manula atakapojirekebisha maana anajiamini sana.

Kocha Amog aijuie timu vizuri na sio kubahatisha wachezaji, huwezi cheza na timu ngumu kama mbao fc halafu unamtoa Gyan na unamwingiza Luizio ambaye hakabi anasubiri kupewa pasi.
Mchezaji hasa mshamvuliaji akipwaya afanyiwe Sub haraka, amjaribu MO ktk ushambuliaji anashabaha nzuri pia.
Kuna wachezaji kwa mazoezini tu wanacheza vizuri ila ktk mechi ni hawafanyi vizuri. Boko na Luizio ni mojawapo.

Simba sc, Msimu huu hatutaki uzembe hasa wachezaji wasiojituma wanaosubiri waletewe mipira miguuni.
Simba hatutaki Sare, tunataka ushindi ktk mechi zote.

Simba sc tunataka ubingwa wa VPL, na sio vinginevyo. Wachezaji wajitume maana wanalipwa vizuri kutokana na mikataba yao waliyosaini.

Simba Hatutaki uzembe wa wachezaji mnamponza hadi kocha.

Hatutaki visingizio, kama mchezaji unaleta uvivu mchezoni nenda kacheze ndondo.
Tunaanza kuwachoka.
 
Kama ni mpenzi wa soccer [emoji460], karibu tupeane updates za ligi mbali mbali kama vile VPL, EPL, LA LIGA, UEFA, N.K<br /><br />FOOTBALL FANS
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…