Nimekuwa nikisema kuwa matumizi ya pesa kwenye mpira kufanya ushawishi kwa wachezaji wa timu pinzani, kwa waamuzi na wachambuzi wa mchongo, matokeo yake yataonekana mechi za kimataifa.
Katika mechi hizi hakuna cha wazee waliopigania uhuru wala sijui mashabiki wa ukweli, Ni uwezo wa wachezaji na akili. Mechi hizi siyo za kukamia kama inavyofanyika kwenye ligi yetu.
Kama mnataka kushinda punguzeni matumizi ya vipesa vya kuhonga honga na kutumia wazee kuwatia kiwewe makochaa wa timu pinzani wafanye mabadiliko ya kijinga.
Wekezeni kwenye uwanja kuliko kuwekeza nje ya uwanja na propaganda nyingi.
Wape salaam.