Mechi za mwisho VPL,Vita ya ubingwa na kushuka daraja

Mechi za mwisho VPL,Vita ya ubingwa na kushuka daraja

Daah!,niliangalia ile game mwanzo mwisho ukweli mbao walicheza mpira kwa nguvu sana ili washinde wasishuke daraja na walifanikisha malengo yao.Hakuna ubishi.
 
Hatimae Klabu bingwa Tanzania Bara Yanga imejivunjia heshima Kwa kuuza mechi yake Kwa klabu ya mbao
Kwa hali ilivyo ni ngumu sana yanga kuwaza issue ya kuuza mechi wakati kuwa na point 68 kunamweka kwenye hatihati ya kumkabidhi simba ubingwa endapo Simba atapewa point zake tatu walizopokonywa kipuuzi
 
Upuuzi mlidhani hao ni toto?? Mwanza sasa tumepata team ya ushindani mkija mjiandae..

Hakuna point za bure bure..
 
Wauze wakati wanajua FIFA wanakuja na point tatu za wenyewe?
 
Mkuu Unakumbuka sababu alizotoa katibu mkuu wa TFF Kuhusu hili jambo? nikukumbushe tu hakugusia kabisa issue ya kadi 3 badala yake alisema simba imekata rufaa nje ya muda, hawakulipa ada ya rufaa na kuna wajumbe ambao hawakustahili kuwepo kwenye ile kamati iliyo ipoka kagera points! Taarifa zisizo rasmi zinasema report ya referee inatofautiana na ya kamisaa, Tukubaliane kitu kimoja hili suala lina utata mwingi na ndio maana nikasema kulikuwa na ugumu gani kusubiri maamuzi ya FIFA kabla ya kukabidhi zawadi?
Ni kweli linautata kwasababu ni kipi kiliwafanya kamati ya SAA 72 kujadili rufaa ilotolewa nje ya muda? Na nini kiliwafanya wamwite refa kutoa ushahidi wa kadi wakati inaeleweka SAA 48 baada ya mechi taarifa inatakiwa iwe imeshahifadhiwa.. Na nini kiliwafanya watumie zaid ya siku mbili kujadili kadi tatu wakati ni jambo Massa matatu tu yani kuangalia taarifa za waamuzi na kutoa maamuzi.. Kwa kufatilia mtiririko Huo unaona kabisa kuna ubabaishaji katika maamuzi ya kamati ya SAA 72.
 
Back
Top Bottom