Media tour ya Mbosso sijaielewa kabisaa

Mengine uache yakupite sio kila kitu lazima uelewee hii dunia INA mengi madhari mwenyewe wanajua wanachokifanya inatosha.
Huna kazi.
 
Mimi nampenda sana Mbosso ila kwa ubora wa hizi nyimbo mbili alizozitoa MBOSSO, kiukweli haingii hata robo kwa ASLAY, nyimbo ni za kawaida sana na Melody zimenyooka tu kama kwaya zinawahi kuboa.
ASLAY ni noma sana sana bila hata sapoti ya CMG, WCB wakubali tu hilo hakuna namna
 
Hebu weka link ya iyo interview yenye viewers milion 4 maana naona unabwabwaja
Mbona interview za wcb zinazofikisha milionn zaidi ya hizo zipo kibao tu vichannel vingi vya youtube vinategemea kiki za wcb ndo wapate cha kuandika
 
Sijali nani atakua juu ya mwenzake, ninachojali je huyo msanii kipato chake kinaendana na jina lake.?

Huyo Asley Clauds watampandisha sana jina, lakini mwisho wa siku ataishia kuzunguka kwenye mafiesta.

Juzi tu hapa ametoka kumwandikia barua mama yake marehemu kuwa anachokitafuta hakiendani na jina lake.

Clauds ni wazuri sana kwenye kumjenga msanii ila sio kujali maslahi ya msanii mwenyewe.

Mwisho wa siku wanaishia kuwa mateja ......

Darasa nae nasikia amekuwa teja baada ya kutumika sana na kulipwa kidogo.

Sasa msanii kama Diamondi anaejali haki lazima aungwe mkono kwa juhudi zote.
 
hivi kati ya msanii na manager nani ni mwajiriwa na nani anatakiwa amlipe mwenzake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…