Media za Tanzania zinaweza kufa kipindi hiki cha miaka mitano ya CCM

Unadhani Ni watanzania wangapi wanauhitaji wa haya uliyoyaandika.ungeniambia magazeti ya michezo kusurvive ningekuelewa.

Watanzania wengi sana wanahitaji magazeti mfano Kampuni zinazotafuta na kutangaza tenda watu wanaopotelewa na nyaraka muhimu kama hati zanyumba paspoti na vyeti wanatangaza magazetini wanafunzi waliomaliza masomo wanaotafuta ajira huduma za mahakama matangazo ya sammons ya kuitwa mahakamani nk taarifa muhimu kutoka serikali kila chombo cha habari kina umuhimu kama sio kwako ni kwa watu wengine.
 
Wenye uelewa mpana zaidi watakujibu.
 
Kile unachokiwaza wewe hakiwazwi na wengine mi naona ndo yatauzika Sana Tena Sana kwani wasomaji walikuwa Ni Upinzani?
 
Mvuto wanini tena jamani? Muhimu ni MAENDELEO na Rais Magufuli ni Kiongozi mpenda MAENDELEO kwahiyo Watanzania hatuna wasi wasi na hilo
 
Hizo zife kabisa kwani zimekosa msaada,kwa taifa letu Hadi wakati huu.
 
Mkuu mbona huchangii mada? Au wewe unapendelea vile vijarida vya kina Mustafa Waziri na Emmanuel Shaluwa? [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji2445][emoji2445][emoji2445]
 
Kwa sasa zimeshakufa binafsi sikumbuki mara ya mwisho nilinunua gazeti lini,kwa sasa labda tutayanunua kufungia maandazi na kuwapa watoto kujaladia madaftari,hata tv channels wengi hatuangalii kabisa wala kuzisikiliza huwa naangalia channels za kenya na nje pamoja na za michezo,cartoon na wild animals,siwezi kupoteza muda wangu kuangalia channels za ndani...
 
TV zote ukifungua unakutana na maombi ya taifa ya kusifu na kuabudu. Chanel ten (CCM media) wamejiongeza na Chanel ten plus miziki mitupu. Na kile kipindi Cha old screw ambavyo vinaangaliwa.
Binafsi nalipia king'amuzi kwaajili ya mtoto kuangalia katuni tu...hakuna habari yakuangalia kwa mtu mwenye akili timamu
 
Yes mpaka sasa cement mfuko elf 35
Watu kwa lawama hauchelewi kusema mpaka sasa hivi ndio maana mke wako hajaamka.. nafikiri hili la cement serikali imelielezea vizuri.

Tukipunguza macho ya kuona lawama na kuona neema basi mioyo yetu itakuwa yenye amani sana.
 
Tuseme ukweli nani huko atanunua gazeti asome habari za Jiwe? Hata Mataga sidhani kama wanaweza nunua hizo gazeti
 
Mimi nitanunua tu kwani kuna vitu muhimu kama matangazo ya tenders matangazo ya kupotelewa vitu, hati za watu kuitwa kwenye mashauri nafasi za kazi matoleo maalumu taarifa za kibenki kila robo mwaka nk bila kusahau kusoma nyota
Kufa haimaanishi kuwa watu wote wataacha kuyasoma/kununua mara moja, mtabaki wachache sana msiyoleta tija/faida yoyote kwa media husika hivyo kupelekea media kufunga/kufa. Hizo habari unazozitafuta/kuzisoma zinatafutwa na watu wachache sana kama wafuasi wa yule mgombea urais wa kike (Queen)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…