Mehran Karimi Nasseri: Mwanaume aliyeishi Uwanja wa Ndege kwa miaka 18

Mehran Karimi Nasseri: Mwanaume aliyeishi Uwanja wa Ndege kwa miaka 18

mcshonde

Member
Joined
Jul 15, 2022
Posts
66
Reaction score
154
C0B47FA3-3AE7-43D6-844E-31A6B6476E17.png

Mehran Karimi Nasseri ni mwanaume ambaye ameishi ndani ya uwanja wa ndege kama nyumbani kwake kwa zaidi ya miaka 18. Serikali ya Iran ilimfukuza nchini bwana Nasseri bila kumpa pasi ya kusafiria (passport) wala viza kwa sababu alitoa kauli za kumpinga kiongozi mkuu wa nchi.

Alipotoka Iran alikwama kwenye uwanja wa ndege wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa. Kwa kuwa hakuwa na nyaraka yoyote inayomtambulisha mamlaka ya uwanja wa ndege haikuweza kumruhusu aende popote na hata kumrudisha Iran ikawa ngumu kwani serikali ndiyo imemfukuza. Sheria kali za uhamiaji ulaya zikawa kikwazo kwani "ni mtu asiye na nchi" kwahiyo ilikuwa ni marufuku kwake kuvuka mlango na kutoka nje ya uwanja huo

Filamu ya The Terminal (2004) iliangazia uhalisia wa maisha yake na namna anavyotafuta pesa ya kujikimu hapo hapo uwanjani kuanzia Agosti 1988 hadi 2006: alikuwa anasaidia mafundi wanaofanya marekebisho mbalimbali, alisaidia kufanya usafi, alijenga urafiki na wasafiri waliokuwa wakimkuta kila wanapofika uwanjani hapo na wengine walimpa fedha kujikimu.

Alitumia muda huo pia kuandika historia ya maisha yake. Mwaka 2006 akawa dhaifu kiafya ndipo akapelekwa kwenye nyumba ya wazee aishi ingawa kila mara alikuwa anarudi uwanjani hapo kukaa kwani ameshazoea. Nasseri alifariki Novemba 2022 kwa mshtuko wa moyo.
 
Maisha ni kuamua tu hizi mambo za ntafia wapi achana nazo we songa mbele
 

Mehran Karimi Nasseri ni mwanaume ambaye ameishi ndani ya uwanja wa ndege kama nyumbani kwake kwa zaidi ya miaka 18. Serikali ya Iran ilimfukuza nchini bwana Nasseri bila kumpa pasi ya kusafiria (passport) wala viza kwa sababu alitoa kauli za kumpinga kiongozi mkuu wa nchi.

Alipotoka Iran alikwama kwenye uwanja wa ndege wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa. Kwa kuwa hakuwa na nyaraka yoyote inayomtambulisha mamlaka ya uwanja wa ndege haikuweza kumruhusu aende popote na hata kumrudisha Iran ikawa ngumu kwani serikali ndiyo imemfukuza. Sheria kali za uhamiaji ulaya zikawa kikwazo kwani "ni mtu asiye na nchi" kwahiyo ilikuwa ni marufuku kwake kuvuka mlango na kutoka nje ya uwanja huo

Filamu ya The Terminal (2004) iliangazia uhalisia wa maisha yake na namna anavyotafuta pesa ya kujikimu hapo hapo uwanjani kuanzia Agosti 1988 hadi 2006: alikuwa anasaidia mafundi wanaofanya marekebisho mbalimbali, alisaidia kufanya usafi, alijenga urafiki na wasafiri waliokuwa wakimkuta kila wanapofika uwanjani hapo na wengine walimpa fedha kujikimu.

Alitumia muda huo pia kuandika historia ya maisha yake. Mwaka 2006 akawa dhaifu kiafya ndipo akapelekwa kwenye nyumba ya wazee aishi ingawa kila mara alikuwa anarudi uwanjani hapo kukaa kwani ameshazoea. Nasseri alifariki Novemba 2022 kwa mshtuko wa moyo.

Ni doc gani zimetumika kumpeleka kukaa kwa Nyumba za kuhifadhi Wazee? Kukosa busara ni ujinga sometimes
 
Back
Top Bottom