Melchizedek na utata unaomzunguka

Melchizedek na utata unaomzunguka

Agano la kale ni kivuli cha Agano jipya. Maana yake yaliyotokea yaliakisi yatakayotokea katika Agano jipya. Mzee Mwanakijiji kaandika vema nami naandika kwa kiasi.

Tuanze na Yohana 8 ambapo Yesu alikuwa akijibizana na mafarisayo kuhusu Yeye ni nani:

Yohana 8
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵⁶ Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
⁵⁷ Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
⁵⁸ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.


Hapa Yesu anatupa dokezo kuwa kuna mahali wakati Ibrahimu akiishi hapa duniani walikutana hivyo basi tukitafuta kwenye Agano la kale tutakuta mahali fulani habari ya Yesu na Ibrahimu. Twende kwenye Agano la kale:

Mwanzo 14
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁸ Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
¹⁹ Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
²⁰ Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.


Hapa kuna mambo matatu muhimu kumhusu Melkizedeki:
1. Alikuwa mfalme wa Salem
2. Alileta mkate na divai wakala pamoja
3. Alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu

Ikumbukwe kuwa katika Biblia yote hakuna mwanadamu aliyetajwa kuwa mfalme na kuhani kwa wakakati mmoja isipokuwa masihi tu. Tuone andiko moja tu kwa mfano:

Zekaria 6
¹³ Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.


Ok, tukiangalia hayo mambo matatu, salem (shalem kwa kiebrania) sio mahali, bali ni ufafanuzi. Maana yake ni amani, hivyo alikuwa mfalme wa AMANI, sifa ambayo imetajwa kuwa nayo masihi pekee.

Isaya 9
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.


Alileta mkate na divai ambayo ni komunyo. Angalia jambo hilo lilifanyika pia kwenye Agano jipya.

Tuangalie sasa Waebrania:

Waebrania 7
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
² ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;


Kumbe hata neno Melkizedeki sio jina kama tulivyodhania, ni maelezo tu. Melkizedeki = mfalme wa haki. Yesu ndiye atakayehukumu kwa haki, yeye ni mfalme wa haki pia mfalme wa amani.

³ hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.


Nadhani umeona parallel iliyopo kati ya Agano la kale na jipya, hicho ndicho kivuli kilichokuja kudhihirika kwa Agano jipya.

Kama hujaelewa uliza.
Mkuu maelezo yameshiba hongera Sana
 
Agano Jipya lugha yake ya Asili ni Kigiriki na wala siyo kiingereza kwa hiyo hapa unafanya kosa unalodhani nimefanya.

Biblia ya Kiswahili (agano Jipya) ilitafsiriwa direct kutoka kwenye Kigiriki na siyo Kiingereza.

Hiyo ni point ya kwanza

Lakini lets us use your argument, kwamba badala ya kutumia neno "Kama", tuuangalie huo msitari kwa mantiki ya maneno "In the order of Melkizedek", bado inaprove kuwa hawa ni watu wawili tofauti, mathalani kwa upande wa wana Israel Makuhani wote waliofuata baada ya AARON wanahudumu in "the order of Aaron", inamaanisha wanadumisha huduma ileile iliyokusudiwa na Aaron haimaanishi kuwa wao ndiyo Aaron re-incarnate

Kwa hiyo hata Yesu naye ni Kuhani katika order ya Melkizedeki maana yake ni kwamba kama Jinsi Melkizedeki alivyokuwa Kuhani mtumishi wa Mungu aliyejuu sana ndivyo hivyohivyo jinsi Yesu alivyo Kuhani mtumishi wa Mungu aliyejuu sana.

Tukija kwenye Ishu ya umama, ishu ya Yesu kuwa na mama tangu kuzaliwa,
Ishu ya MAMA ni ishu ya hapa DUNIANI, Ukiondoa Adamu na Eva hakuna aliyewahi kuwa MTU/BINADAMU hapa duniani bila Kuzaliwa na Mwanamke.
Hakuna Ushahidi kuwa Huko Mbinguni viumbe walioko huko huzaliwa na Mwanamke/Mama
Kwa hiyo kujaribu kusisitiza kuwa existence ya Yesu kabla ya kuja duniani ilikuwa bila mama haina maana yoyote kwenye muktadha wa majadiliano yetu maana Ishu ya mama significance yake ni hapa duniani siyo huko Mbinguni

Kuhusu baadhi ya viumbe kuonekana katika umbo la mtu bila kuzaliwa na mwanamke hapa duniani, Malaika wao huonekana kama kuvaa miili ya Watu wakati mwingine lakini Siyo BINADAMU maana hawakuzaliwa na Uzao wa Adamu yaani ( WATU)
Haya ndio majibu yaliyo shiba
 
Mkuu Bado unahitaji kuendelea kujifunza Neno la Mungu, wala sishangai vile inaposhindwa kuelewa utofauti wa Mungu, Yesu na Kristo.

"Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika." Yohana 1:1- 3.

Mission ya Yesu alipokuja duniani haikuwa kuja kujitangaza kuwa yeye ni Mungu, bali kutangaza wokovu hata kufa kwa ajili ya mwanadamu, ndio maana hutakuta sehemu hata moja alitamka kujiita Mungu, bali alijiweka nafasi ya mwanadamu. Mtu anayehangaika kutafuta mahali Yesu alijiita Mungu ni wazi kuwa bado haelewi Biblia, haelewi mpango wa wokovu.

Yesu angejiita Mungu na kujaribu kujiweka nafasi ya ki-Ungu na heshima yake, hivi unadhani mpango wa wokovu ungekamilika?, unadhani ni mwanadamu gani angesubutu kumkamata?, nani angemshambulia Mungu?.

Ilikuww ni lazima ajiweke mbali na cheo cha Uungu, ili wawepo watu watakaomdharau na kumdhihaki na hata kumsulubisha.

Soma Neno la Mungu, Upate Maarifa.
Yesu sio Mungu ila ni nabii aliyetumwa kama walivyo manabii walio pita
 
Hakufa as kufa hapa duniani ila hauwezi muona Mungu kwa mwili wetu huu wa damu na nyama so nachoamini either alibadilishwa au mwili wake ulichomolewa ukawekwa mahali ili Roho yake iingie mbinguni.

Otherwise Biblia itacontradict maana ipo clear kuwa ukimuona Mungu na mwili huu UTAKUFA ila kuanzia Ufunuo 22 huko tutamuona Mungu sababu tutakuwa tumefufuliwa na miili mipya ambayo sio hii ya sasa midhaifu inayozeeka!!

Kama ambavyo Musa aliuacha mwili wake mlimani ukaenda zikwa na Malaika basi naamini pia Henoko alipitia the same kwa muktadha huu.
Kwanini bible aija nyooka Kimaandiko mpaka kila mtu anakuja na lake
 
Huku ndo kuishiwa hoja sasa!, Ukiona mtu anaanza kushambulia mtu badala ya hoja ujue kaishiwa!
Au hujui kuwa katika vyuo vya Theolojia hata Qur'an hufundishwa na mafundisho ya dini nyingine pia?(Ni somo linaloitwa Comparative religion)
Akina Pengo wale wako fiti mafundisho yote usiwaone vile
Na bahati mbaya sasa hujui miye nani!.Ndo uzuri wa JF huo, usije ukakuta wewe ndo ulikuja juzi kuungama!!
Kwani Pengo nani? Yeye akiijua quran ndio wote tujue!! Nini nakomaa na Neno la Mungu - Biblia inanitosha sana.
Nimekwambia unakariri biblia kama ulivyokariri quaran ndio maana unapata shida kuelewa biblia.
 
Kwani Pendo nani? Yeye akiijua quran ndio wote tujue!! Nini nakomaa na Neno la Mungu - Biblia inanitosha sana.
Nimekwambia unakariri biblia kama ulivyokariri quaran ndio maana unapata shida kuelewa biblia.
Biblia inakupa fursa ya kujifunza vitu vingine maana yenyewe wala aijaandika kila kitu,acha kujiaminisha kwenye box , utashindwa kuelewa.mambo yalivyo
 
hermēneuō - interpate

Outline of Biblical Usage

to explain in words, expound

to interpret

to translate what has been spoken or written in a foreign tongue into the vernacular
Mkuu, acha ku complicate mambo, imesema hivi, "tafsiri ya hilo jina" hapo complications za malugha lugha sijui ya kigiriki na kingereza yanatoka wapi? Mbona ipo wazi sana hiyo, hata haijajificha.
 
Samweli hakuwahi kuwa mfalme. Zamani za kuhani Samweli taifa la serikali ya wana wa Israeli ilikuwa Theocratic, yaani Mungu mwenyewe alikuwa akitawala kama mfalme. Kumbuka ni wakati wa Samweli waisraeli walilazimisha wawe na mfalme kama mataifa mengine, ndipo akachaguliwa mfalme wa kwanza aitwaye Sauli. Hoja ni hiyo hoyo kwa Eli kuhani.

Kuhani na mfalme ni Yesu Kristo peke yake, tafuta biblia nzima.

Nijibu hili swali, ukuhani kati ya wanadamu ulianza lini? Lengo la ukuhani huo lilikuwa lipi?
OK, nani labda alikua akifanya majukumu ya kisiasa Enzi hizo za kuhani Eli na Samuel katika taifa la Israel? I mean yale majukumu ambayo wafalme walipaswa kuyafanya, mfano kuamuru majeshi kwenda vitani etc, who was that!?
 
Mkuu, acha ku complicate mambo, imesema hivi, "tafsiri ya hilo jina" hapo complications za malugha lugha sijui ya kigiriki na kingereza yanatoka wapi? Mbona ipo wazi sana hiyo, hata haijajificha.
Sasa wewe unatembea gizani utayaelewaje mambo ya nuruni? Mbona hata Kuruani yenu ina kamusi? Acha kujionyesha huna hekima
 
OK, nani labda alikua akifanya majukumu ya kisiasa Enzi hizo za kuhani Eli na Samuel katika taifa la Israel? I mean yale majukumu ambayo wafalme walipaswa kuyafanya, mfano kuamuru majeshi kwenda vitani etc, who was that!?
Samweli hakjwa mfalme, umeielewa hiyo? Kwani wakati wa Musa naye alikuwa mfalme? Vipi wakati wa Yoshua? Biblia iko wazi nenda soma ujifunze kuhusu waamuzi na wafalme wa wana wa Israeli.

Kwa kukusaidia tu Samweli ndiye aliyewaapisha wafalme wawili wa kwanza kabisa wa Israeli, Sauli na Daudi. Soma biblia.
 
Samweli hakjwa mfalme, umeielewa hiyo? Kwani wakati wa Musa naye alikuwa mfalme? Vipi wakati wa Yoshua? Biblia iko wazi nenda soma ujifunze kuhusu waamuzi na wafalme wa wana wa Israeli.

Kwa kukusaidia tu Samweli ndiye aliyewaapisha wafalme wawili wa kwanza kabisa wa Israeli, Sauli na Daudi. Soma biblia.
Mkuu, Musa, Eli na Samuel walifanya kazi zote 2 kama ambavyo tunamuongelea huyu Melkizedeki pia, walifanya kazi za UKUHANI na ufalme pia, yaani walifanya kazi za siasa na za kiroho pia. Kama tu huyu Melkizedeki ambavyo pia tunamsoma kwenye BIblia kwamba was a king and a priest as well. Saul alikuja baada ya wana ISrael kutoridhishwa na kuamua na wao wawe kama mataifa mengine. Musa na Joshua wote walikua wakiamuru majeshi kwenda vitani. Unakumbuka watoto wa Eli walifia vitani, nani aliamuru majeshi ya Waisrael kwenda vitani kama sio kuhani Eli mwenyewe?
 
Mkuu, Musa, Eli na Samuel walifanya kazi zote 2 kama ambavyo tunamuongelea huyu Melkizedeki pia, walifanya kazi za UKUHANI na ufalme pia, yaani walifanya kazi za siasa na za kiroho pia. Kama tu huyu Melkizedeki ambavyo pia tunamsoma kwenye BIblia kwamba was a king and a priest as well. Saul alikuja baada ya wana ISrael kutoridhishwa na kuamua na wao wawe kama mataifa mengine. Musa na Joshua wote walikua wakiamuru majeshi kwenda vitani. Unakumbuka watoto wa Eli walifia vitani, nani aliamuru majeshi ya Waisrael kwenda vitani kama sio kuhani Eli mwenyewe?
Samweli hakuwa mfalme, umeelewa hiyo? Narudia tena, soma kuhusu waamuzi na majukumu yao, usome na kuhusu wafalme.

Kuhusu Melkizedeki, kqma kweli una nia ya dhati, jibu maswali niliyouliza huko juu, sio baada ya post tatu au nne mnarudi kule kule. Jibu maswali, yapaoa huko juu. Biblia imetofautiana sana na Quran kwa sababu yenyewe ni ya mambo ya rohoni wakati quran ni ya mwilini. Hivyo usijaribu kulinganisha usomaji wa biblia na quran, huku hakuna aya za kukariri, ni aya za kuelewa tu
 
Samweli hakuwa mfalme, umeelewa hiyo? Narudia tena, soma kuhusu waamuzi na majukumu yao, usome na kuhusu wafalme.

Kuhusu Melkizedeki, kqma kweli una nia ya dhati, jibu maswali niliyouliza huko juu, sio baada ya post tatu au nne mnarudi kule kule. Jibu maswali, yapaoa huko juu. Biblia imetofautiana sana na Quran kwa sababu yenyewe ni ya mambo ya rohoni wakati quran ni ya mwilini. Hivyo usijaribu kulinganisha usomaji wa biblia na quran, huku hakuna aya za kukariri, ni aya za kuelewa tu
DU, tunabishana, Sasa habari za Qurani zinatoka wapi hapa?Kuna sehemu hata 1 nimegusia habari za qurani? Well, haya ni masuala ya IMANI, bakia unavyo amini na mimi nibaki ninavyo amini.
 
Hii mada kuna watu wameshaiharibu, wakishindwa kuthibitisha hoja zao basi wanakimbilia kuwaita wale wasiokubaliana nao kimaandiko kuwa ni waislamu

Hajui kuwa pengine humu kuna
(1) Marastafari
(2)Wayahudi
(2) Mashahidi wa Yehova
(3) Unitarian Church of Christ

Hawa wote wana tafsiri tofauti za maandiko ya Biblia na hawakubaliani na mengi ya Tafsiri za kibiblia kwa mujibu wa madhehebu mbali mbali

Kwa hiyo hapa tuangalie hoja tu, mambo sijui wewe ni mtoto wa Kijakazi, au mtoto wa mama kambo yaache!

Hata kama ni mtoto wa mama wa kambo wewe kwa akili zako unadahni mama yako wewe ni mkuu kuliko yule mama wa kambo aliyeongea na malaika jangwani na ambaye Mungu kwa kauli yake alisema Mwanae atambaliki na atakuwa taifa kubwa?
 
Unachanganya mambo unaposema kuwa KRISTO NDIYE MUNGU
Mungu ni Mungu na Yesu ni Yesu

Yesu alimwabudu Mungu na wala Mungu hakumwabudu Yesu [" Akaenda kwenye bustani ya Gethsemane kuomba, Baba ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, siyo kama mimi nitakavyo bali wewe Utakavyo.."]

Yesu hajui muda wala Saa ya Siku ya Mwisho, Bali Mungu anajua[ Yesu alisema " Hakuna aijuaye saa wa la siku ile si malaika wala mwana bali BABA peke yake"]

Yesu alichosikia kwa Mungu ndicho alichofundisha na wala mafundisho yake hayakuwa kwa utashi wake [Yesu alisema "Nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu yangu ni ya haki...."]

Wote wanaomkubali Yesu, ni Mungu ndiye aliyemjaalia wampokee na wamkubali wala si kwa uwezo wake binafsi watu hao kupokea mafundisho yake [Yesu alisema "Baba ulionipa sikumpoteza hata mmoja"]

Yesu anatambua kuwa BABA ndiye Mungu wa pekee [Yesu alisema "Na uzima wa Milele ni huu, wakujue wewe Mungu wa KWELI na wa PEKEE na Yesu Kristo uliyemtuma"]

Yesu anakiri BABA ni mkuu kuliko yeye [Yesu alisema "BABA yangu ni Mkuu kuliko Mimi"]

Mungu wa Yesu ndiye Mungu wetu, Na Mungu huyo Yesu alipenda kumuita BABA (Yesu alisema "Ninakwenda kwa Baba Yangu naye ni Baba Yenu, MUNGU WANGU NAYE NI MUNGU WENU")

Utukufu wa Yesu ni BABA ndiye aliyempa wala Yesu hakujipa Mwenyewe [Yesu alisema "Baba Ningependa hawa ulionipa wawe nami nitakapokuwa, wauone utukufu wangu, Utukufu ULIONIPA kabla ya kuumbwa kwa dunia"]

Sasa wewe unaleta habari za Yesu kuwa Mungu wakati maandiko all the time yanakuonyesha kuwa kuna ALIYE JUU YA YESU KIMAMLAKA!

Au unataka kutwambia BABA ni Mungu Mkubwa mkubwa na YESU ni Mungu Mdogomdogo?

Kwa mujibu wa maandiko huwezi kumuequate FATHER (JEHOVAH) na SON (JESUS) yaani utakwama, maandiko hususan Kauli za Yesu mwenyewe zitakukatalia.

Tukubali tu kuna Mungu Mmoja ambaye YESU alikuwa akimuita BABA

Na tukubali tu kuwa Yesu alitumwa na Mungu kuwafunza watu wamjue BABA ili wapate Salvation

Na tukubali tu kuwa Yesu naye ana Mungu, na Mungu mwenyewe ndiye yule alikuwa akimuita BABA

Hili tatizo la kuconnect dots ndo limeharibu sana mafundisho halisi ya Kristo: Badala ya kutwaa mafundisho ya Kristo kama alivyofundisha, watu throughout centuries wakaanza kutengeneza nadharia kuwa "ooh, Yesu ndyo Baba lakini hakujifunua tu, Wengine wanasema hapana BABA na MWANA ni Separate entities lakini wote ni sawa(CO-EQUAL), Wengine wanasema BABA na MWANA ni Walewale tu ila kila mmoja ana role tofauti

Logic/Falsafa/ Nadharia na kuconnect dots kwa baadhi ya watu kumedilute na kupoteza muelekeo halisi wa Mafunzo aliyofundisha Kristo mwenyewe na kuyapeleka so far out of context!

Kristo mwenyewe anasema MY FATHER IS GREATER THAN I (Baba yangu yu Mkuu kuliko mimi), lakini wanakuja watu centuries later wanasema FATHER na SON ni CO-EQUAL and CO-ETERNAL!. hii CO-EQUAL wameipata wapi? wamejitungia wenyewe tu ili kuconnect dots kwao kuweze kumakes sense kwa mujibu wa akili zao za kupenda falsafa!
Yani mimi katika kitu ambacho siwezi kukielewa ni yesu kuwa mungu ili uamini hiki inabidi ujitoe akili na usiulize chochote nakubaliana na wewe 100 yesu sio mungu.
 
Hii mada kuna watu wameshaiharibu, wakishindwa kuthibitisha hoja zao basi wanakimbilia kuwaita wale wasiokubaliana nao kimaandiko kuwa ni waislamu

Hajui kuwa pengine humu kuna
(1) Marastafari
(2)Wayahudi
(2) Mashahidi wa Yehova
(3) Unitarian Church of Christ

Hawa wote wana tafsiri tofauti za maandiko ya Biblia na hawakubaliani na mengi ya Tafsiri za kibiblia kwa mujibu wa madhehebu mbali mbali

Kwa hiyo hapa tuangalie hoja tu, mambo sijui wewe ni mtoto wa Kijakazi, au mtoto wa mama kambo yaache!

Hata kama ni mtoto wa mama wa kambo wewe kwa akili zako unadahni mama yako wewe ni mkuu kuliko yule mama wa kambo aliyeongea na malaika jangwani na ambaye Mungu kwa kauli yake alisema Mwanae atambaliki na atakuwa taifa kubwa?
Wewe ndio unaharibu mada. Unaleta hoja zisizoendana na mada kwa lengo la ub8shani kuliko kuelimishana. Haya jibu hoja zangu nilizokupa halafu unazikwepa. Pia sio vema kuikana dini yako, hujui posts zako zinakuumbua?
 
Back
Top Bottom