Melchizedek na utata unaomzunguka

Melchizedek na utata unaomzunguka

Hivi kwa mujibu wa maandiko Yesu si ni mwana wa Mungu, vipi tena inakuwaje mnasema hana baba?

Mfano maandiko yanasema:
"Na kwa namna hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa MWANA WAKE WA PEKEE ili kila atakayemuamini asipotee"

"Mahali pengine yanasema:
Baba mtukuze Mwanao na mwanao naye akutukuze....."

"Sehemu nyingine panasema, Huyu ni MWANANGU mpendwa niliyependezwa naye.."

Sasa ni andiko gani kwenye Biblia linasema Melkizedeki ana baba?

Kama Yesu ndiye Melkizedeki basi Yesu hana baba kwa hiyo dhana ya Kuwa Yesu ni mwana wa Mungu inavunjika

Na kama Yesu ni mwana Pekee wa Mungu basi Yesu siyo Melkizedeki maana Melkizedeki hana baba
We jamaa unapiga sana za mbavu duh!.
 
Kama hiyo ndiyo hoja basi hata sisi tumekuwepo huko kwa Mungu kabla ya kuja duniani, kwa hiyo hata sisi hawa tunaowaita mama zetu ni njia tu ya kutuleta humu duniani.

HATA SISI HATUNA BABA WALA MAMA, HAWA TULIO NAO NI NJIA TU

Ecclesiastes 12:7
“Then shall the dust return to the earth as it was: and the spirit shall return unto God who gave it.”
Mkuu una hoja nzito sana aisee.
 
Hakuna mahali kwenye bible Yesu anatambulishwa kwa sifa ya uungu, hii ni theolojia ya kuunga unga tu kama hii ya kujaribu kumfananisha Yesu na Melkizedeki, lakini theolojia hiyo imebase kwenye logical inferences tu badala ya maandiko!, yaani imebase kwenye watu kuconnect dots badala ya kauli thabiti ya Yesu mwenyewe

Mathayo 24:36 Yesu mwenyewe kwa kauli yake anasema anasema, "hakuna ajuaye saa wala muda wa siku ile SI MALAIKA WALA MWANA AJUAYE ILA BABA PEKE YAKE (3“But concerning that day and hour no one knows, not even the angels of heaven, nor the Son,[a] but the Father only. ")
hili andiko peke yake linakuonyesha kuwa Yesu yuko limited in knowledge, hajui mambo yote na siri zote za ulimwengu huu, na hiyo peke yake ni ushahidi kuwa siyo Mungu
Asante sana mkuu!.
 
Tatizo siyo waraka wa Waebrania, Tatizo ni uelewa wa waraka huo
Nyinyi mnautafsiri out of context kwa kuungaunga maana.

Ngoja Niquote Maandiko

SOURCE: https://www.biblegateway.com/passage/?search=Waebrania+7&version=SNT

Yesu Na Melkizedeki (Waebrania 7:11-17)
11 Kama ukamilifu ungaliweza kupatikana kwa njia ya ukuhani wa Walawi, kwa maana watu walipewa sheria kupitia kwao, ilikuwapo haja gani tena ya kuwepo kuhani mwingine, yaani kuhani kama Mel kizedeki, ambaye si kama Aroni? 12 Kwa maana yanapotokea maba diliko kwenye ukuhani, ni lazima pawepo na mabadiliko katika she ria. 13 Maana Bwana wetu ambaye ndiye anayesemwa katika mambo haya, alikuwa ni wa kabila lingine, na hakuna mtu katika kabila lake aliyewahi kuhudumu katika madhabahu. 14 Inafahamika wazi kuwa Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na Mose hakuwahi kusema lo lote juu ya makuhani kutoka katika kabila hilo. 15 Na hili tunalosema linakuwa wazi zaidi anapotokea kuhani mwingine kama Melkizedeki; 16 ambaye ukuhani wake hautokani na kanuni za ukoo wake, bali hutokana na uwezo wa maisha yasiyoharibika. 17 Kwa maana ameshuhudiwa hivi: “Wewe ni kuhani milele, kama wa Melkizedeki.”

Ni dhahiri:
Kwa mujibu wa andiko hilo katika msitari wa mwisho nilioupigia msitari unaosema "WEWE NI KUHANI MILELE KAMA MELKIZEDEKI" inaonysha kuwa YESU ni YESU na MELKIZEDEKI ni MELKIZEDEKI ila wote wana Ukuhani wa Milele!.

Neno "Kama" limetumika kwenye hilo andika KULINGANISHA watu wawili, Nikisema Mtu X kama Mtu Y kwenye ishu Z maana yake siyo kwamba X ndiye Y bali hawa ni watu tofauti lakini wana role Z ambayo ni moja

KITU KIKISHAITWA "KAMA" MAANA YAKE KINAFANANISHWA (compared to) , KINAKUWA SIYO CHENYEWE HALISI!

Ni suala la lugha tu, Ukitaka kutumia logic yako kuungaunga visivyoungika basi bible unaweza kuitafsiri vyovyote unavyopenda na ikaleta justification zozote
Mimi ndiyo maana huwa nakaa kimya tu.Maana wenzetu hata lugha huwa hawaizingati.
 
Mkuu kwanza thanks for sharing with us hi kitu; miongoni mwa maada ambazo waumini wengi hua wanapata sana TABU basi ni story ya huyu mtu uliyemsema hapa, but kwa kusoma kwangu Biblia, huyu Melkizedeki ni mtu tu kama walivyo pata kua watu wengine, au niweke hivi, Melkizedeki alikua mtumishi wa Mungu kama walivyo pata kutokea wengine na hata waliopo( Yesu anabakia kua ndio kila kitu katika Imani ya Kikristo and may be na zingine ( huko kwingine sina interest nako cause sijasoma sana vitabu vyao) Kwenye huo mstari uliutaja, hebu rudi nyuma mstari 2, utaona imeanza hivi kwa kufungia mabano, "huyo Melkizedeki ( tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena mfalme wa Salem, maana yake mfalme wa Amani; ...inaendelea kama ulivyo copy hapo then akafungia mabano. KWahiyo huyu mtu sio kwamba hakuana na baba wala mama na wala hakua mfalme wa milele bali, tafsiri ya jina lake ndio hiyo. Kwa mfano, jina Emmanuel (jina la kwanza kabisa la ahadi la Yesu ) tafsiri yake ni Mungu pamoja na nasi; Kwa hiyo mtu yeyote aitwaye Immanuel hata leo either ana amini katika Mungu au la, hiyo ndio tafsiri ya jina hilo, hivi unajaua jina Yusufu au Joseph kwa kingereza maana yake ni nini? Ni kwamba mtoa jina ana maana hivi, "God you may give me another son" Haijalishi wazazi wanao toa jina hilo Yusufu/Joseph kwa watoto wao kama na wao wanaomba Mungu afanye hivyo au laa but hio ndio maana yake. So huyu Melkizedeki na yeye jina lake ndio lina tafsiri hiyo but yeye hakua kuahani wa milele na ndio maana hapo hapo ulipotoa maandiko, inasema ni mfano wa….., kitu mfano wa… means sio halisi ila kimebeba kitu kingine.
Again, thanks for sharing na huo ndio mchango wangu
Umekuja vizuri mkuu.Asante.
 
Unachanganya mambo unaposema kuwa KRISTO NDIYE MUNGU
Mungu ni Mungu na Yesu ni Yesu

Yesu alimwabudu Mungu na wala Mungu hakumwabudu Yesu [" Akaenda kwenye bustani ya Gethsemane kuomba, Baba ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, siyo kama mimi nitakavyo bali wewe Utakavyo.."]

Yesu hajui muda wala Saa ya Siku ya Mwisho, Bali Mungu anajua[ Yesu alisema " Hakuna aijuaye saa wa la siku ile si malaika wala mwana bali BABA peke yake"]

Yesu alichosikia kwa Mungu ndicho alichofundisha na wala mafundisho yake hayakuwa kwa utashi wake [Yesu alisema "Nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu yangu ni ya haki...."]

Wote wanaomkubali Yesu, ni Mungu ndiye aliyemjaalia wampokee na wamkubali wala si kwa uwezo wake binafsi watu hao kupokea mafundisho yake [Yesu alisema "Baba ulionipa sikumpoteza hata mmoja"]

Yesu anatambua kuwa BABA ndiye Mungu wa pekee [Yesu alisema "Na uzima wa Milele ni huu, wakujue wewe Mungu wa KWELI na wa PEKEE na Yesu Kristo uliyemtuma"]

Yesu anakiri BABA ni mkuu kuliko yeye [Yesu alisema "BABA yangu ni Mkuu kuliko Mimi"]

Mungu wa Yesu ndiye Mungu wetu, Na Mungu huyo Yesu alipenda kumuita BABA (Yesu alisema "Ninakwenda kwa Baba Yangu naye ni Baba Yenu, MUNGU WANGU NAYE NI MUNGU WENU")

Utukufu wa Yesu ni BABA ndiye aliyempa wala Yesu hakujipa Mwenyewe [Yesu alisema "Baba Ningependa hawa ulionipa wawe nami nitakapokuwa, wauone utukufu wangu, Utukufu ULIONIPA kabla ya kuumbwa kwa dunia"]

Sasa wewe unaleta habari za Yesu kuwa Mungu wakati maandiko all the time yanakuonyesha kuwa kuna ALIYE JUU YA YESU KIMAMLAKA!

Au unataka kutwambia BABA ni Mungu Mkubwa mkubwa na YESU ni Mungu Mdogomdogo?

Kwa mujibu wa maandiko huwezi kumuequate FATHER (JEHOVAH) na SON (JESUS) yaani utakwama, maandiko hususan Kauli za Yesu mwenyewe zitakukatalia.

Tukubali tu kuna Mungu Mmoja ambaye YESU alikuwa akimuita BABA

Na tukubali tu kuwa Yesu alitumwa na Mungu kuwafunza watu wamjue BABA ili wapate Salvation

Na tukubali tu kuwa Yesu naye ana Mungu, na Mungu mwenyewe ndiye yule alikuwa akimuita BABA

Hili tatizo la kuconnect dots ndo limeharibu sana mafundisho halisi ya Kristo: Badala ya kutwaa mafundisho ya Kristo kama alivyofundisha, watu throughout centuries wakaanza kutengeneza nadharia kuwa "ooh, Yesu ndyo Baba lakini hakujifunua tu, Wengine wanasema hapana BABA na MWANA ni Separate entities lakini wote ni sawa(CO-EQUAL), Wengine wanasema BABA na MWANA ni Walewale tu ila kila mmoja ana role tofauti

Logic/Falsafa/ Nadharia na kuconnect dots kwa baadhi ya watu kumedilute na kupoteza muelekeo halisi wa Mafunzo aliyofundisha Kristo mwenyewe na kuyapeleka so far out of context!

Kristo mwenyewe anasema MY FATHER IS GREATER THAN I (Baba yangu yu Mkuu kuliko mimi), lakini wanakuja watu centuries later wanasema FATHER na SON ni CO-EQUAL and CO-ETERNAL!. hii CO-EQUAL wameipata wapi? wamejitungia wenyewe tu ili kuconnect dots kwao kuweze kumakes sense kwa mujibu wa akili zao za kupenda falsafa!
Kila kitu kimeisha hapa.Good job brother.
 
Kifupi watu wote wanaodai Yesu ni Mungu,basi 90% utumia ufahamu wa Paulo.
JIBU LANGU NI KWAMBA KWENYE MAANDIKO FUATA KWANZA KAULI YA YESU MWENYEWE ILIYO CLEAR KABISA KABISA ISIYO NA MAWAA KABLA YA KUAFUATA KAULI AU OPINION YA MTU YEYOTE HATA KAMA MTU HUYO NI MWANAFUNZI WA YESU AU ANAYEDAI KUTOKEWA NA YESU NJIANI AKIELEKEA DAMASCUS (PAULO)

Ngoja nikuulize, hivi wewe kwa mtizamo wako maneno aliyoyasema Paulo, James, Petro au mtu yeyote yakikinzana na maneno halisi ya Yesu yapi unayapa precedent?. Maneno ya nani yanakuwa Final Finito?

Kwa mfano, ukisoma bible vizuri utaona mara kadhaa James ambaye ni mwanafunzi wa Yesu, aliyeishi na Yesu na ni ndugu wa Yesu akigombana mara kibao na Paulo juu ya mafundisho ya Paulo, James analalamika kuwa Paulo analeta baadhi mafundisho mapya na si yale aliyoyafundisha Yesu mwenyewe hususan mafundisho ya kuendelea kuheshimu Sheria za torati vs kuachana na sheria hizo!

Kwa mfano James anatofautiana na Paulo kwenye suala la nani mwenye kuhesabiwa haki, Paulo anasema kwenye Warumi 4:1-5 kuwa mtu anahesabiwa haki kwa IMANI yake na si Matendo yake, akaenda mbele kutoa mfano wa Abrahamu kuwa alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa Imani yake na si matendo yake japo matendo yake mazuri ni kitu cha kujivunia yeye binafsi.

James akamjibu Paulo kwenye James 2:24 kuwa Imani bila MATENDO imani hiyo Imekufa!, James akaenda mbali kutoa mfano wa kwenye agano la Kale juu ya yule kahaba Rahabu aliyewapoteza wapelelezi waliokuja kupeleleza katika nchi yao kwa kuwadanganya njia, na kwa kitendo cha kufanya hivyo tu huyo kahaba akahesabiwa haki!

Kwa hiyo Unaona hawa ni watu wawili wenye mawazo tofauti juu ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa hiyo point yangu ni kwamba, kwa kuwa hata wao wana mitizamo inayokinzana juu ya mambo ya Mungu Sembuse Mmoja apingane na Kauli ya Wazi ya Yesu Mwenyewe?


Yesu kajiita Mtu, Kasema wazi kuwa na yeye pia ana Mungu anayemwabudu, Kasema BABA yake ni Mungu wake na pia ni Mungu wetu THEN baadae atokee mtu mmoja anayeitwa Paulo au Yeyote yule kisha aseme "Jamani eeeh Hapana, Yesu naye ni Mungu", anatoa kauli opposite kabisa na Yesu mwenyewe, mimi nasema Kauli ya kusikiliza hapo ni KAULI YA YESU MWENYEWE, HAWA WENGINE WAMETOA OPINION YAO TU!, OPINION YAO ITAKUWA NA UZITO IKIFANANA NA MAFUNDISHO YA KRISTO MWENYEWE ,IKIENDA AGAINST NAYE SISI TUNACHUKUA MANENO YA KRISTO NDO YANAKUWA FINAL!
 
Wewe nafikiri kaanzishe mada yako maana naona hauelewi misingi ya hii dunia kuumbwa.
Haujui muunganiko wa maagano yote mawili.
Hapa tunanyonya ilimu kwa wabobezi.
Sasa ilimu hii itapotea ukiendelea kufanya huo upotoshaji wako wa kukariri neno moja moja.
Anzisha mada wenzako kina faiza wakufuate.
Acha kukimbia ukweli wewe.
 
Ukimgusa Paulo tutakuweka kwenye dustbin na hutakuwa na hoja yenye mashiko tena,,,hoja yako imefeli sasa umehamia kwenye baseless argument za watu flani wanaomchukia Paulo kwa sababu ya akili ndogo na ilio opposite.Pia unaharibu uzi mzuri wa Ndugu yetu ambae katulia akaandaa uzi wa uhakika.Kama huna hoja usiudhi watu humu.
JIBU LANGU NI KWAMBA KWENYE MAANDIKO FUATA KWANZA KAULI YA YESU MWENYEWE ILIYO CLEAR KABISA KABISA ISIYO NA MAWAA KABLA YA KUAFUATA KAULI AU OPINION YA MTU YEYOTE HATA KAMA MTU HUYO NI MWANAFUNZI WA YESU AU ANAYEDAI KUTOKEWA NA YESU NJIANI AKIELEKEA DAMASCUS (PAULO)

Ngoja nikuulize, hivi wewe kwa mtizamo wako maneno aliyoyasema Paulo, James, Petro au mtu yeyote yakikinzana na maneno halisi ya Yesu yapi unayapa precedent?. Maneno ya nani yanakuwa Final Finito?

Kwa mfano, ukisoma bible vizuri utaona mara kadhaa James ambaye ni mwanafunzi wa Yesu, aliyeishi na Yesu na ni ndugu wa Yesu akigombana mara kibao na Paulo juu ya mafundisho ya Paulo, James analalamika kuwa Paulo analeta baadhi mafundisho mapya na si yale aliyoyafundisha Yesu mwenyewe hususan mafundisho ya kuendelea kuheshimu Sheria za torati vs kuachana na sheria hizo!

Kwa mfano James anatofautiana na Paulo kwenye suala la nani mwenye kuhesabiwa haki, Paulo anasema kwenye Warumi 4:1-5 kuwa mtu anahesabiwa haki kwa IMANI yake na si Matendo yake, akaenda mbele kutoa mfano wa Abrahamu kuwa alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa Imani yake na si matendo yake japo matendo yake mazuri ni kitu cha kujivunia yeye binafsi.

James akamjibu Paulo kwenye James 2:24 kuwa Imani bila MATENDO imani hiyo Imekufa!, James akaenda mbali kutoa mfano wa kwenye agano la Kale juu ya yule kahaba Rahabu aliyewapoteza wapelelezi waliokuja kupeleleza katika nchi yao kwa kuwadanganya njia, na kwa kitendo cha kufanya hivyo tu huyo kahaba akahesabiwa haki!

Kwa hiyo Unaona hawa ni watu wawili wenye mawazo tofauti juu ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa hiyo point yangu ni kwamba, kwa kuwa hata wao wana mitizamo inayokinzana juu ya mambo ya Mungu Sembuse Mmoja apingane na Kauli ya Wazi ya Yesu Mwenyewe?


Yesu kajiita Mtu, Kasema wazi kuwa na yeye pia ana Mungu anayemwabudu, Kasema BABA yake ni Mungu wake na pia ni Mungu wetu THEN baadae atokee mtu mmoja anayeitwa Paulo au Yeyote yule kisha aseme "Jamani eeeh Hapana, Yesu naye ni Mungu", anatoa kauli opposite kabisa na Yesu mwenyewe, mimi nasema Kauli ya kusikiliza hapo ni KAULI YA YESU MWENYEWE, HAWA WENGINE WAMETOA OPINION YAO TU!, OPINION YAO ITAKUWA NA UZITO IKIFANANA NA MAFUNDISHO YA KRISTO MWENYEWE ,IKIENDA AGAINST NAYE SISI TUNACHUKUA MANENO YA KRISTO NDO YANAKUWA FINAL!
 
takbirrrr ..
Pale muislam utapotaka kuonekana unajua vyote Qur-an na Bible.
Yako Qur-an mkuu, bible huelewi na ndio maana points zako ni kakariri kama mlivyozoea kukariri qur-an.
Bible inahitaji uelewa chini ya uongozi wa Roho mtakatifu, sasa mkuu wewe sijui unaongozwa na nini katika kuielewa Bible wakati hata huyo Roho mtakatifu muhuamini.
Mkuu umemuelewa vizuri.Kaona uzi ni mzuri roho imemuuma akaamua alete tafakari zake za kipuuzi.
 
Nikupe saluti tu kwa elimu Nzuri.
Melkizedeki hakuwa "Kuhani Mkuu" bali "Kuhani wa Mungu aliyejuu sana". Kumbuka wakati huo Mungu aliye juu sana hakuwa amefunuliwa kwa Musa na wala Ukuhani haukuwepo. Lakini tunadokezwa tu kuwa huyu Melkizedeki tayari alikuwa anamtolea sadaka El Elyon (Mwenye Enzi)


Swali zuri sana; itabidi turudi kwenye text yenyewe. Lakini kiufupi ni kuwa Ibrahim alimpa heshima kubwa Melkizedeki na ndio pointi ya baadaye kwenye Waebrania. Kuwa kama Ibrahim alitoa fungu la kumi kwa Melkizedeki ina maana kiwadhifa au hadhi Melkizedeki alikuwa juu yake.



Hili ni swali zuri. Na hapa ndio wengi wanachanganyikiwa. Je, Yesu alikuwepo kabla ya Bikira Maria; au alianza kuwepo baada ya kuzaliwa? Dokezo kidogo ni kuwa katika ile inayojulikana kama "Sala ya Kikuhani" ya Yesu kwenye Yohana 17 tunakutana na ombi hili kwa babake "Na sasa Baba, nitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu" (Yoh. 17:5). Na mistari kadhaa chini anasisitiza hili (Yoh. 17:24). Ukisoma mistari hiyo lazima ujiulize? Yesu alikuwepo kabla ya misingi ya ulimwengu? Na kama alikuwepo kuzaliwa kwake na Bikira Maria basi kuna maana gani?
 
Habari za masiku wanajukwaa wote, leo ningependa tujadili watu mysterious kwenye vitabu vyetu vya dini kama ilivyo kawaida yetu. Hivyo twendeni pamoja ili tusolve mystery hii, kubwa ya yote tuongeze tu maarifa na kujibu maswali ambayo yameonekana magumu kwenye vitabu hivi.

Niweke rai mapema pamoja na kwamba inaongelea mtu wa kwenye imani zetu ila mada hii isijengwe kidini yaani kukashifiana bali ijikite kwenye mrengo wa kuelemishana. Karibuni

UTANGULIZI
Melchizidek anaongelewa kwa mara ya kwanza ndani ya Biblia kwenye kitabu cha mwanzo 14:18 ambapo baada ya Abraham kutokea vitani alikutana na Mfalme wa eneo la Salem (Jerusalem ya leo) ambapo alimbariki na Adam alimpa kikumi cha kila alichokuwa nacho wakati huo.

Kwahiyo kitabu cha mwanzo kinamueleza kama MFALME WA SALEM na kuhani wa Mungu YAHWEH

View attachment 1176929
AGANO JIPYA
Upande wa agano Jipya Melchizedek anaelezwa kuwa ana uhusiano ma Yesu.

Waebrania 5
6 kama asemavyo mahali pengine,Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki

Zaburi 110:4, Waebrania 5:10,6:20 zote zinaeleza kuwa Yesu ni kuhani kwa mfuatano na huyu melchizedek. Ikumbukwe Makuhani wengi wamepita hapo kati na Yesu ametokea kwenye uzao wa Abraham sasa iweje afananishwe na melchizedek na sio kuhani yeyote yule??

Je huyu melchizedek ni nani hasa?

UTATA ZAIDI
Utata zaidi unaibuka pale ambapo muandishi wa kitabu cha waebrania (ambaye mpaka leo hafahamiki ni nani) anaandika haya
Waebrania 7
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.

Tunaambiwa huyu ''Jembe'' hakuwa na baba wala mama na anaishi milele hata sasa???

Ukisoma sura yote inamsifia mtu huyu wa ajabu (mysterious) na kusema licha ya ukuu wa Abraham kama Baba wa wayahudi ila haoni ndani kwa huyu Melchizedek!!

Book of Enoch
Muandishi wa kitabu hiki anajaribu kutupa mwanga kidogo kuhusu utata huu. Ukisoma Enoch 2 sura ya 71 inaeleza kuwa Kuhani Nir (Kaka yake Nuhu) alikuwa na mke ambaye hakulala naye toka alipoteuliwa na Mungu kuwa kuhani. Siku moja anagundua mke wake ana mimba, hivyo ukazuka ugomvi mkubwa mwishowe yule mama akapata presha akaanguka akafa, sasa cha ajabu walipotaka kuizika maiti haraka haraka ''kuua soo'' Wakashangaa mtoto ametoka tayari!!!. Yaani maiti imezaa!!!
Hivyo ikawa concluded kuwa kazaliwa bila baba wala mama.

Ikumbukwe alizaliwa kabla ya gharika, hivyo ili unabii utimie kuwa atakuwa kuhani wa makuhani wote ikabidi Malaika Gabriel amchukue na kumficha bustani ya Eden hivyo akapona gharika na akarudishwa baada ya gharika kupita.

HITIMISHO
Katika pekua pekua zangu sijakutana kabisa na maandiko yeyote kwenye biblia na pseudepigrapha (vilivyoachwa) ambacho kinagusia mwisho wake zaidi vyote vinasema anaishi milele ingawa havisemi wapi ama lini aliacha kuwa mfalme wa Salem.

Sasa wajuvi wa Historia na Dini mtusaidie je mtu huyu alikua nani hasa??

Pia kma alikuwa mkuu kuliko Abraham na amefananishwa na Yesu kwanini hajaongelewa sana kwenye Bible??

Je historia yake ni ipi??

Je mwisho wake ni upi hapa duniani? Au bado anaishi na sisi kwa sura tofauti?

Karibuni....



Melchizedek, A god greater than Jesus?


In the Bible we can read about another god. His name is Melchizedek (or Melchisedec). He is first mentioned in Genesis

"And Melchizedek king of Salem brought forth bread and wine: and he was the priest of the most high God. And he blessed him, and said, Blessed be Abram of the most high God, possessor of heaven and earth: And blessed be the most high God, which hath delivered thine enemies into thy hand. And he gave him tithes of all."
Genesis 14:18-20

This in itself may not be all that significant until we read Hebrews

"For this Melchisedec, king of Salem, priest of the most high God, who met Abraham returning from the slaughter of the kings, and blessed him; To whom also Abraham gave a tenth part of all; first being by interpretation King of righteousness, and after that also King of Salem, which is, King of peace; Without father, without mother, without descent, having neither beginning of days, nor end of life; but made like unto the Son of God; abideth a priest continually. Now consider how great this man was, unto whom even the patriarch Abraham gave the tenth of the spoils."
Hebrews 7:1-4

Is this God's brother? Is this God's cousin? Is this a completely different God? For these are certainly divine attributes. According to the Bible in our hands today, Jesus (pbuh) had a beginning (he was "begotten"), and an end "he gave up the ghost" (Luke 23:46). This mighty being, however, is alleged to have had neither. It is stated plainly here in the Bible, that he was "made like unto the son of God." Why do they not worship him then? The church now will allege that Jesus peace be upon him was "begotten" by God. Tell us what you mean when you say "begotten." What did God Almighty do to "beget" Jesus (pbuh)? Further, if Jesus (pbuh) was "begotten," but Melchisedec who was "made like unto the Son of God," was not, then does this not make Jesus (pbuh) a "son of God" but Melchisedec an independent god with neither offspring nor parents? Is a god with no parents not greater than one who needs parents? Where is Melchisedec now?

From these verses we get the following picture:

1)Melchizedec is equal to the Son of God
2)Melchizedec's ministry is eternal
3)Melchizedec, unlike Jesus (pbuh), is an independent god, with neither father nor mother.
4)Melchizedec, unlike Jesus (pbuh), was never "born" or "begotten" but was ever present.
5)Melchizedec, unlike Jesus (pbuh), will never die but is eternally without death.
6)Everything but God has a beginning of days. Even air, water, and food have a beginning of days. Melchizedec, however, does not. Therefore, he is claimed to not need God nor water, food, nor air to breathe.

Does this not sound preposterous? Notice how when Jesus (pbuh), a man, is preached as being a god most people have no trouble with that. They are willing to see proof of his godhead even where it can not be found (see chapter one). This is because this is a well established doctrine in Paul's church. However, when the same Bible tells them in no uncertain terms that another man, Melchisedec, is a god, then they are willing to "interpret" the verses fifty different ways and attach to them all manner of abstract interpretations to disprove this claim since Melchisedec "cannot possibly" be a god. Why? Because the church has not told us to worship Melchizedec?. If the Bible remains the word of God then why should we place the words of men (the church) above the words of God?

Some people will object that: "Melchizedec was an imaginary character and not real." Once again, a valid possibility, so let us study this claim. Let us go back and read the above verses. Was prophet Abraham (pbuh) an imaginary character? Of course not! Well then, did Abraham "meet" a figment of his imagination upon returning from the "slaughter of the kings"? Was Abraham blessed by a figment of his imagination? Did he give a tenth of his spoils to a figment of his imagination?

I have searched far and wide in my quest for a logical answer to this dilemma. Many interpretations have been presented, however, these interpretations always attempt to either completely side-step the above issues, or when they do actually attempt to deal directly with them they say "of course it can not possibly be that the words are meant to be taken literally," with no valid explanation whatsoever. It is simply left up to the reader to have "faith" and only take the literal meanings of such words when they are applied to Jesus (pbuh), but when they are applied to others then they "can not possibly" be understood to be taken literally. Why?

It is easy to make excuses. It is much harder to keep an open mind. Many people have a tendency to quote only part of the command of the Bible. They read "Jesus said unto him, Thou shalt love the Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul" and stop!. Well what about the rest of the verse? What about "…and with all thy mind." I don't know about you, but my salvation is too precious a commodity to allow someone to dictate to me blind faith in doctrines they have inserted in the book of God, resulting in countless discrepancies. A truly unchanged religion of God must be able to convince me fifty ways from Sunday that it is faultless and unchanged by the hands of men. It should not need its propagators, and "correctors" to demand blind faith and my having to continually make excuses for it even though they themselves bear witness to the continuous and unrelenting attempts of the church to "correct" and "clarify" the Bible over so many centuries.

 
Melchi=Malki=mmiliki=King,
Zedek=righeousness=watakatifu,

Melchizedek=Malikzedek=king of righeousness=mfalme wa watakatifu,

pia kuna mfalme aliefuata pale Salem,aliitwa Adonizedeki,

Adon=Lord=Bwana.

Adonizedek=Lord of righeousness=Bwana wa watakatifu,

lakini tena Zedek alikuwa ni mungu wa kipagani wa caanan,akisimamia watakatifu,ujue enzi za zamani kulikua na miungu wa kila kitu,
mungu wa milimani,mungu wa samaki,mungu wa ardhi,mungu wa vita,mungu wa uzazi etc,

so huyu zedek ni mungu wa watakatifu katika jamii ya caanan enzi hizo,

lakini sasa tunaambiwa Melchizedeki ni Kuhani wa El elyon,yaani ni kuhani wa The most high god,ambae alikuwa ni mungu wa caanan yote,

Abraham alitokea Ur,huko mesopotamia yaani iraq ya leo,
alipofika caanan,huyu king Melchizedek ndo alimu introduce Abrahamu katika imani ya kumuabudu mungu wa caanan,El Elyon,

abraham hajapata kumuabudu wa kumfahamu Yahwew (jehova).

Na huu ukweli jehova mwenyewe amekiri ndani ya bible kuwa,si Abraham,isaka wala yakobo walipata kumfahamu jehova,

kwa hiyo hadi wanakufa,Abraham,isaka na yakobo walimjua El Elyon kama mungu wao
 
Kwahiyo Melchzedeki,kiuhalisia ni Title sio jina,
ni title kama Rais,waziri wa ujenzi,waziri wa afya etc,
huyu alikuwa mfalme,Malki,melchi wa watakatifu,
ambacho hicho cheo kilimfanya awe kuhani mkuu wa Mungu mkuu(The most high),
mungu alie juu=El Elyon,

katika nyakati hizo watu waliamini Mungu mkuu kuliko wote anaishi juu,

ndo maana utaona ilikuwa ni marufuku kujenga nyuma za ghorofa kwa kuonekana kuwa na wewe unataka kuwa juu kama mungu,
sasa connect dot na mnara wa BABEL,

BAB-EL,

watu wa sumeria walijenga mnara mrefu ili wamfikie mungu mkuu El,,lakini mungu huyo akawachanganya wasiweze,

ili kuongea na mungu moses alikuwa akipanda mlimani,hii ilitokana na iman kuwa mungu huishi maeneo ya juu,kama milimani vile,

yesu alikuwa akipanda mlimani kwenda kuomba,

yesu aliamini uwepo wa mungu El Elyon,ndo maana hata kabla hajafa pale msalamani alimlii na kumwita ,El El ,

yesu hajapata kumtaja Yahwew kwa jina,

lakini kwa kawaida katika biblia ukiona neno,LORD au BWANA,hasa katika agano la kale wanakuwa wanamaanisha yahwew,

unganisha Adoni=Lord=Bwana,

kwa ufupi dini za leo ni muunganiko wa dini za zamani,a.k.a dini za kipagani
 
Ukimgusa Paulo tutakuweka kwenye dustbin na hutakuwa na hoja yenye mashiko tena,,,hoja yako imefeli sasa umehamia kwenye baseless argument za watu flani wanaomchukia Paulo kwa sababu ya akili ndogo na ilio opposite.Pia unaharibu uzi mzuri wa Ndugu yetu ambae katulia akaandaa uzi wa uhakika.Kama huna hoja usiudhi watu humu.

Usiogope kumgusa yeyote katika wafuasi wake isipokuwa KRISTO mwenyewe, maana Injili aliifundisha yeye!, wengine wamerokodi tu au wameitafsiri na tafsiri yao si lazima iwe sahahi!

Wanafunzi wa Yesu kama vile James na Peter wenyewe walimkosoa Paulo Vikali juu ya baadhi ya mafundisho yake
Ilifikia hatua hadi James akamjibu Paulo kwa kutumia lugha kali sana ambayo kwa viwango vya sasa unaweza kusema alimtukana, haya yote yamo ndani ya Bible, Kwa hiyo siyo kweli kuwa mafundisho ya Paulo yalikuwa untouchable, na wanafunzi wa Yesu waliyaquestion pia, sembuse sisi?

unahitaji kusoma maandiko na historia ya mambo ili uweze kuelewa. Usikubali kumezeshwa Dogma/Doctrines za mathinkers, msome KRISTO wewe mwenyewe umuelewe!.
 
Huielewi bible na hutoweza kumwelewa Paulo maana na yeye alikuwa great thinker.Watu waliomezeshwa huwa wanabisha hadi facts.
Usiogope kumgusa yeyote katika wafuasi wake isipokuwa KRISTO mwenyewe, maana Injili aliifundisha yeye!, wengine wamerokodi tu au wameitafsiri na tafsiri yao si lazima iwe sahahi!

Wanafunzi wa Yesu kama vile James na Peter wenyewe walimkosoa Paulo Vikali juu ya baadhi ya mafundisho yake
Ilifikia hatua hadi James akamjibu Paulo kwa kutumia lugha kali sana ambayo kwa viwango vya sasa unaweza kusema alimtukana, haya yote yamo ndani ya Bible, Kwa hiyo siyo kweli kuwa mafundisho ya Paulo yalikuwa untouchable, na wanafunzi wa Yesu waliyaquestion pia, sembuse sisi?

unahitaji kusoma maandiko na historia ya mambo ili uweze kuelewa. Usikubali kumezeshwa Dogma/Doctrines za mathinkers, msome KRISTO wewe mwenyewe umuelewe!.
 
Back
Top Bottom