Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Musiba nguvu za matusi yale alizipata wapi,most likely ni kutoka TISS ya Hayati Magufuli.Bahati yake mbaya Musiba ni kwamba hii ni TISS ya Samia.Kwa hiyo bad luck for him,sidhani kama itakuwa na msaada kwake.
 
Mkuu,

Kwanza vitabu vinatuambia tutii mamlaka kama alijua Membe ni kiongozi mbona hakumtii?

Lakini mali zinauzwa kwa sababu alishindwa kutetea hoja(uozo) unasema Musiba aliwaambia wananchi. Kushindwa huko maana yake umemchafua mtu pasipo sababu, adhabu yake ndio hiyo. Na kwa sababu mali alizonazo amezipata kutokana na kuchafua watu wacha zichukuliwe walipwe waliochafuliwa. Hapo Karma ndio imefanya kazi. Umelipwa hela kwa kuwapakazia watu sasa fedha hizo zinaru kwa waliopakaziwa
 
Ungemuuliza Membe swali hili wakati kesi inaendelea. Lakini kama walivyofanya maaskofu ukaacha sheria ichukue njia yake kisha unatafuta dini ya Membe.!! Angeshindwa kesi hii bado ungetaka kujua dini ya Membe?

Lakini ningependa kukusaidia jibu. Membe ni mfuasi wa dini ya ukristo dhehebu la Roma. Kwa kufuata Imani yake akaomba amalize suala hili nje ya mahakama. Pia akaomba chama kisaidie kwa kuwaita yeye na Musiba. Katibu wa chama wakati ule Bashiru akagoma kukutana na Membe na akakataa kutomshirikisha Musiba. Badala yake Bashiru akatumia tuhuma za magazeti ya Musiba kumfukuza Membe chama, huku Musiba akiomba Membe akamatwe na avunjwe miguu kwasababu alikuwa anaandaa mapinduzi ya serikali ya mungu wa Chato.

Membe akabakiwa na risasi moja tu: mahakama. Mahakama ikamwona Musiba anakesi ya kujibu wakati mungu wake wa Chato akiwa hai. Musiba akasema mahakama isingeweza kumpa ushindi Membe labda mungu wake awe amekufa. Sasa Membe ameshinda wewe unauliza ni wadini gani? Ili iweje kwa wakati huu?
 
Membe itakua kafulia anataka hela hakuna kingine hapo nimemshtukia.
Naam. Nami nimewashtukia viongozi wa dini waliotumwa na Musiba kuwa ni wale wale waliotumika kipindi kile cha giza kumtukukuza mfalme na kuutakasa utawala wake wa giza! Bahati nzuri kachero anawafahamu fika.
 
Alifukarishwa kwa makusudi. Alipwe pesa zake kama wanavyolipwa wengine.
Yule ibilisi mwenye roho mbaya kuliko shetanj mwenyewe alimzuilia kuwa Katibu Mkuu wa Jumuia ya Madola kama alivyowazuilia marehemu Likwelile na Mulamula kufanya kazi Umoja wa Afrika! Badala yake akamtuma Musiba kumchafua. Achukue tu hizo mali; kwanza Musiba alifanya biashara gani kustahili kuwa na hizo mali? Hizo ni mali za nchi zilizoporwa kipindi kile cha giza kuwazawadia vichaa waliomtukuza na kumpigania mwenzao!
 
Hawa si Mungu, ni binadamu tu kama wengine......wasikataliwe wana nini cha kumzidi Membe?
Musiba amewacagua hao kwa kujua jinsi walivyokuwa pamoja kuupigania utawala wa giza. Kwa macho ya kibidamu bora hata Membe kuliko hawa kwani aliweza kujitenga na ubatili wa awamu ya tano; hawa waliwatelekeza kondoo na kusimama na shetani! Sijui hata wanapata wapi ujasiri wa kuwasiliana na Membe!
 
Siyo kweli kwamba Membe sasa amepata nafasi na kwamba walioko madarakani ni wezake! Ukweli ni kwamba vyombo vya nchi sasa angalau vimeanza kutekeleza wajibu wao. Kabla ya hapo vyombo vyote vilikuwa butu vikitumikia maslahi ya kisiasa ya mtu mmoja na genge lake la mashetani. Kesi kama hii ya Membe ingefutwa haraka kwa amri kutoka juu au angepangiwa wale majaji wa voda fasta wanaotoa hukumu bila kunukuu vifungu vya sheria.
 
Membe ni failure anayetapatapa.

Aliwahadaa ACT wazalendo kwamba ataingia dakika ya 89 na kufunga goli alafu akaishia kufanya kampeni za urais kwenye kijiji cha Rondo
Musiba kwisha habari yake. Tulimuonya hakusikia
 
Wacha historia iandikwe vizuri kijana huyu mjinga alitukana vibaya huku akitishia hata kuua hafai kabisa kuachwa hivihivi... Alipokuwa anatukana askofu hakuna na kukemea Leo anajiingiza kumwombea msamaha wanini?? Musiba anastahili kuvuna alicho panda!! Alitukana watu na kuwazushia mambo ya hovyo mitandaoni hadharani na mpaka Leo hajarudi mtandaoni kuomba msamaha na kufuta maneno machafu yaliyomtoka kisa kusaka umaarufu!!!
Viongozi wa makanisa wawe makini kabla ya kuingilia mambo au wataishia kutumika vibaya na kushusha heshma Yao.
TAFADHALI NDUGU MEMBE MIMI NIMMOJA YA WATU TULIOKUSAPOTI TOKA UKIWA WAZIRI MAMBO YA NJE,HUYU KIJANA ANADHARAU NA KIBURI KIBAYA MWACHE AWE FUNZO KWA VIZAZI VIJAVYO JINSI SHERIA INAWEZA KUMSHUKIA YEYOTE ANAYETUSI NA KUCHAFUA VIONGOZI WALIOIPIGANIA NCHI NA KUJITOA KUIJENGA...
 
Upuuzi tu sijaona sehemu Musiba ameomba radhi Nini kuhangaika viongizi wa dini Kuna wakati wanatakiwa kuacha unafki Musiba anatukana wako kimya Tena wanasifia tu,Musiba anaombwa aombe radhi wao kimya ,Musiba amepelekwa mahakamani kimya,mahakama inatoa hukumu kimya Membe anataka kukaza hukumu hao...kwani wametumwa na nani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…