Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Siyo kweli kwamba Membe sasa amepata nafasi na kwamba walioko madarakani ni wezake! Ukweli ni kwamba vyombo vya nchi sasa angalau vimeanza kutekeleza wajibu wao. Kabla ya hapo vyombo vyote vilikuwa butu vikitumikia maslahi ya kisiasa ya mtu mmoja na genge lake la mashetani. Kesi kama hii ya Membe ingefutwa haraka kwa amri kutoka juu au angepangiwa wale majaji wa voda fasta wanaotoa hukumu bila kunukuu vifungu vya sheria.
Hahahahah sawa bwana, sasa wewe kafungue mashataka kuhusu ufisadi uliokithiri kisha tutaona jinsi hizo mahakama zita respond juu ya malalamiko yako.
 
Mimi ni mkatoliki Niliacha kusali sababu ya huyu mzee. Ndiye kiongozi mkuu wa kanisa lenye waumini wengi Tanzania na duniani kote.

Cha ajabu hata Watz 1000 wakafa au kuuawa kwa siku moja huwezi kusikia salamu za rambi rambi za huyu Bwana.
Alikuwa swahiba wa wauaji kama hakina Bashite nk.
 
Wakati dalali wa Mahakama kampuni ya Yono (vijana wa kazi) ikihesabu siku zilizobaki katika 14 (siku za kazi) alizolewa mtukanaji Cyprian Majura Musiba kumlipa fidia Kachero Bernard Membe jumla ya shilingi 9.2 Bilioni, Bwana Musiba amewaangukia viongozi wa dini Askofu Alex Malasusa (KKKT Diyosisi ya Pwani) na Kardinali Porlycarp Pengo kumwombea msamaha kwa Membe asipige mnada mali zake.

Taarifa kutoka ndani ya familia ya Membe nyumbani kwake Mikocheni zinaeleza kwamba Jumatatu ya tarehe 24/4/2023 majira ya saa 10 alasiri mjumbe kutoka kwa Pengo alifika kwa Membe kumpa ujumbe wa Pengo kumsihi amsamehe Musiba.

"Alikuja hapa padre wa moja ya makanisa yetu kuleta ujumbe huo lakini naona Mzee alimkatalia na kumwambia 'namheshimu sana baba Askofu Pengo lakini kwenye hili anisamehe yeye (Pengo) huyu kijana lazima alipe gharama ya matusi yake' " anasema mwanafamilia aliyetajwa kwa jina la Colleta na kuongeza:

"Lakini jioni yake ya saa moja Askofu Malasusa naye alimpigia simu Mzee kuongelea suala hilo hilo lakini naye Mzee alimpa majibu yale yale aliyompa mjumbe wa Pengo." Hata hivyo kwa maelezo ya Colleta ni kwamba si tu ni msimamo wa Mwanadiplomasia huyo Bali ni msimamo pia wa familia.

Hii inakuja baada ya jitihada za Askofu Mwamakula pia kugonga mwamba baada ya kumwandikia barua Membe ya msamaha kwa Musiba.

Wakati hayo yakijiri hapa Mikocheni, tayari kampuni ya Yono imeshatua jijini Dodoma itakapoanzia kazi ya mnada kwa kuanza na apartments za Musiba zilizoko Ihumwa, nyumba yake ya Chamwino, guest house yake ya Msalato na shamba la hekari 10 njia ya Singida.

Baada ya hapo Yono atatimba apartment ya Kigamboni, shamba la hekari 5 Bagamoyo kabla ya kugeukia mitambo yake ya uchapaji iliyoko jengo la Exim ghorofa ya 8 jirani na Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam.

Ikumbukwe kwamba huko nyuma Musiba alichapa magazeti yake kampuni ya Malindi Printing huko Mbweni ambayo ni mali ya TISS. Jambo hili lilileta ukakasi wa kisheria kwani sheria ya vyombo vya habari (2016) inamtaka mlalamikaji kumshitaki Mwandishi, mhariri, mchapaji na msambazaji. Kwa mantiki hiyo DG wa TISS angetakiwa kusimama kortini. Ili kuokoa jahazi Musiba "alinunuliwa" mitambo mingine Mpya kutoka Ujerumani na kwa "huruma" mwana TISS Membe aliridhia. Nayo itanadiwa baada ya siku 14 kutamatika pamoja na nyumba na mashamba yake ya kijijini nakadhalika.

My take: Vijana tujifunze kitu katika sakata hili la Musiba na Membe kwamba tuwe na akiba ya maneno. Lakini pia akili ya kupewa changanya na zako. Waliokuwa wakimpa akili karibia wote wamemkimbia tena ndio wamekuwa jirani na Membe. Amtegemeae mwanadamu mwisho huwa kama hivi. Musiba kwishney!
Huenda familia nia yao sio kurudisha heshima Bali wanataka kurudisha zile zilipunguzwa wakati wa Jiwe😁😁anyway.. Kama angetaka Heshima irudi... Angemsamehe Musiba... Maana anaesamehe ndio mtu strong, maana anakana matakwa yake, na kutanguliza furaha ya mwingine... Lazima abarikiwe... Ila kama anangangania kisasi... Na yeye ajihoji ameumiza wa ngapi.... Na je aliumiza kama atalipa kisasi.. Hiyo pesa na kisasi chake vitampa furaha?
 
Huenda familia nia yao sio kurudisha heshima Bali wanataka kurudisha zile zilipunguzwa wakati wa Jiwe😁😁anyway.. Kama angetaka Heshima irudi... Angemsamehe Musiba... Maana anaesamehe ndio mtu strong, maana anakana matakwa yake, na kutanguliza furaha ya mwingine... Lazima abarikiwe... Ila kama anangangania kisasi... Na yeye ajihoji ameumiza wa ngapi.... Na je aliumiza kama atalipa kisasi.. Hiyo pesa na kisasi chake vitampa furaha?
Mahakama inatoa hukumu haitoi kisasi😅😅
 
Wacha historia iandikwe vizuri kijana huyu mjinga alitukana vibaya huku akitishia hata kuua hafai kabisa kuachwa hivihivi... Alipokuwa anatukana askofu hakuna na kukemea Leo anajiingiza kumwombea msamaha wanini?? Musiba anastahili kuvuna alicho panda!! Alitukana watu na kuwazushia mambo ya hovyo mitandaoni hadharani na mpaka Leo hajarudi mtandaoni kuomba msamaha na kufuta maneno machafu yaliyomtoka kisa kusaka umaarufu!!!
Viongozi wa makanisa wawe makini kabla ya kuingilia mambo au wataishia kutumika vibaya na kushusha heshma Yao.
TAFADHALI NDUGU MEMBE MIMI NIMMOJA YA WATU TULIOKUSAPOTI TOKA UKIWA WAZIRI MAMBO YA NJE,HUYU KIJANA ANADHARAU NA KIBURI KIBAYA MWACHE AWE FUNZO KWA VIZAZI VIJAVYO JINSI SHERIA INAWEZA KUMSHUKIA YEYOTE ANAYETUSI NA KUCHAFUA VIONGOZI WALIOIPIGANIA NCHI NA KUJITOA KUIJENGA...
Sahihi
 
Mimi ni mkatoliki Niliacha kusali sababu ya huyu mzee. Ndiye kiongozi mkuu wa kanisa lenye waumini wengi Tanzania na duniani kote.

Cha ajabu hata Watz 1000 wakafa au kuuawa kwa siku moja huwezi kusikia salamu za rambi rambi za huyu Bwana.
Sali tu mkuu kama mimi, ila mambo zake na hata nikimuona tu Pengo moyo wangu unarudi nyuma sana. Natamani angekaa tu kimya.
 
Mh Membe hakuna kumsamehe huyo muhuni musiba piga mnada kila kitu ,ulitoa fursa ya kuomba msamaha lakini alijifanya mbabe na kuendelea kukudhalilisha....Piga mnada hadi makobazi yake najua mali zake hazifikii hizo 9.9B ,kufidia pia mfunge mpaka ndugu zake walipe ndiyo atoke ,hii utaweka precedent kwa wahuni wajao.
 
Wacha historia iandikwe vizuri kijana huyu mjinga alitukana vibaya huku akitishia hata kuua hafai kabisa kuachwa hivihivi... Alipokuwa anatukana askofu hakuna na kukemea Leo anajiingiza kumwombea msamaha wanini?? Musiba anastahili kuvuna alicho panda!! Alitukana watu na kuwazushia mambo ya hovyo mitandaoni hadharani na mpaka Leo hajarudi mtandaoni kuomba msamaha na kufuta maneno machafu yaliyomtoka kisa kusaka umaarufu!!!
Viongozi wa makanisa wawe makini kabla ya kuingilia mambo au wataishia kutumika vibaya na kushusha heshma Yao.
TAFADHALI NDUGU MEMBE MIMI NIMMOJA YA WATU TULIOKUSAPOTI TOKA UKIWA WAZIRI MAMBO YA NJE,HUYU KIJANA ANADHARAU NA KIBURI KIBAYA MWACHE AWE FUNZO KWA VIZAZI VIJAVYO JINSI SHERIA INAWEZA KUMSHUKIA YEYOTE ANAYETUSI NA KUCHAFUA VIONGOZI WALIOIPIGANIA NCHI NA KUJITOA KUIJENGA...

Sure huyo Muhuni MUSIBA inabidi awe funzo kwa WAHUNI wengine.

Membe hakuna kumsamehe kabisa.
 
Mahakama kujihusisha kuamua kesi za madai zenye mlengo wa kisiasa kunaenda kuua demokrasia, uhuru wa kutoa habari na maoni na kunaenda kuziba watu midomo kuibua kashfa mbalimbali za uhujumu nchini kwa kuhofia kuamuriwa na mahakama kulipa fidia za bilioni 9!!!
Ni aibu sana mahakama kufuata mikumbo ya mihemko ya kisiasa.. Uko wapi uhuru wa kutoa maoni wa mtu?
 
Ni aibu sana mahakama kufuata mikumbo ya mihemko ya kisiasa.. Uko wapi uhuru wa kutoa maoni wa mtu?
Yaani ni mambo ya kushangaza, fidia ya bilioni 9 kuamuriwa kulipwa kwenye nchi maskini ambayo wastani wa kipato cha mwananchi kwa mwaka hakifiki hata laki 5 na zaidi ya asilimia 80 ya watu wakiishi chini ya mstari wa kima cha umaskini.​
 
Huenda familia nia yao sio kurudisha heshima Bali wanataka kurudisha zile zilipunguzwa wakati wa Jiwe[emoji16][emoji16]anyway.. Kama angetaka Heshima irudi... Angemsamehe Musiba... Maana anaesamehe ndio mtu strong, maana anakana matakwa yake, na kutanguliza furaha ya mwingine... Lazima abarikiwe... Ila kama anangangania kisasi... Na yeye ajihoji ameumiza wa ngapi.... Na je aliumiza kama atalipa kisasi.. Hiyo pesa na kisasi chake vitampa furaha?
Ili Iwe fundisho kwa waandishi makamjanja na chawa,huu upuuzi unawasumbua chawa wengi Sana.

Mahakama ikitekeleza Hali atayokuwa nayo musiba baada ya kuuzwa Kila kitu chake na Bado hata robo haifiki,waliobaki wakimua galia musiba hawatakubali kamwe kutumika
 
Mahakama kujihusisha kuamua kesi za madai zenye mlengo wa kisiasa kunaenda kuua demokrasia, uhuru wa kutoa habari na maoni na kunaenda kuziba watu midomo kuibua kashfa mbalimbali za uhujumu nchini kwa kuhofia kuamuriwa na mahakama kulipa fidia za bilioni 9!!!
Ni aibu sana mahakama kufuata mikumbo ya mihemko ya kisiasa.. Uko wapi uhuru wa kutoa maoni wa mtu?

Mkuu ulifuatilia mwanzo wa kesi hadi mwisho? Ukimdhalilisha mtu bila ushahidi ni kosa ,Musiba alimsema vibaya sana Membe ,Membe alimsihi Musiba afute kauli na kumwambia aombe radhi aotherwise atapeleka kesi mahakamani na yeye apate haki yake ,Musiba kwa jeuri hakumsikiliza Membe kisa alikuwa analindwa na "STATE".

Umeangalia kwa upande wa Musiba ila wa Membe haukuangalia kabisa ,Uhuru gani wa kutoa maoni kwa kumkashifu mtu kwa tuhuma za Uongo? Huyo Mpuuzi mwache apate fundisho ili wahuni wenzake waje kujifunzo in the future.
 
Wakati dalali wa Mahakama kampuni ya Yono (vijana wa kazi) ikihesabu siku zilizobaki katika 14 (siku za kazi) alizolewa mtukanaji Cyprian Majura Musiba kumlipa fidia Kachero Bernard Membe jumla ya shilingi 9.2 Bilioni, Bwana Musiba amewaangukia viongozi wa dini Askofu Alex Malasusa (KKKT Diyosisi ya Pwani) na Kardinali Porlycarp Pengo kumwombea msamaha kwa Membe asipige mnada mali zake.

Taarifa kutoka ndani ya familia ya Membe nyumbani kwake Mikocheni zinaeleza kwamba Jumatatu ya tarehe 24/4/2023 majira ya saa 10 alasiri mjumbe kutoka kwa Pengo alifika kwa Membe kumpa ujumbe wa Pengo kumsihi amsamehe Musiba.

"Alikuja hapa padre wa moja ya makanisa yetu kuleta ujumbe huo lakini naona Mzee alimkatalia na kumwambia 'namheshimu sana baba Askofu Pengo lakini kwenye hili anisamehe yeye (Pengo) huyu kijana lazima alipe gharama ya matusi yake' " anasema mwanafamilia aliyetajwa kwa jina la Colleta na kuongeza:

"Lakini jioni yake ya saa moja Askofu Malasusa naye alimpigia simu Mzee kuongelea suala hilo hilo lakini naye Mzee alimpa majibu yale yale aliyompa mjumbe wa Pengo." Hata hivyo kwa maelezo ya Colleta ni kwamba si tu ni msimamo wa Mwanadiplomasia huyo Bali ni msimamo pia wa familia.

Hii inakuja baada ya jitihada za Askofu Mwamakula pia kugonga mwamba baada ya kumwandikia barua Membe ya msamaha kwa Musiba.

Wakati hayo yakijiri hapa Mikocheni, tayari kampuni ya Yono imeshatua jijini Dodoma itakapoanzia kazi ya mnada kwa kuanza na apartments za Musiba zilizoko Ihumwa, nyumba yake ya Chamwino, guest house yake ya Msalato na shamba la hekari 10 njia ya Singida.

Baada ya hapo Yono atatimba apartment ya Kigamboni, shamba la hekari 5 Bagamoyo kabla ya kugeukia mitambo yake ya uchapaji iliyoko jengo la Exim ghorofa ya 8 jirani na Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam.

My take: Vijana tujifunze kitu katika sakata hili la Musiba na Membe kwamba tuwe na akiba ya maneno. Lakini pia akili ya kupewa changanya na zako. Waliokuwa wakimpa akili karibia wote wamemkimbia tena ndio wamekuwa jirani na Membe. Amtegemeae mwanadamu mwisho huwa kama hivi. Musiba kwishney!
 
Back
Top Bottom