Meneja wa TANROADS mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji awajibishwe

Meneja wa TANROADS mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji awajibishwe

Mkuu,wananchi sisi ni wajanjawajanja mnoo.Huwa tunalima kiujanjaujanja kama tunapalia nyasi(wanyamwezi wanaita kukela).Kumbe ndiyo kilimo chenyewe.Utakuta tumeshapanda mahindi,mtama,karanga,maharage,kunde nk.
Ukiuliza hilo swali kwamba mamlaka ilikuwa wapi utakwama.Maana kuna "mabalozi",wajumbe wa s/mtaa,mwenyekiti,watendaji wa mitaa,watendaji kata na madiwani tunashinda nao humohumo mitaani.Lakini kuna sababu.
-na wenyewe huwa tunawapiga chenga hivyohivyo kwa kuwazevezya/kuwadanganya tukifanyacho.
-tunawavizia wakati hawapo hasa wikiendi,jioni na sikukuu.
-wengine ni ndugu zetu,marafiki,majamaa,wametuzoea sana au hata wakwe zetu.Hutuonea aibu.Kitanzania hiyo.
-wanatuogopa kwa upole wetu sana,midomo yetu mikali au uchawi.
-uzembe wao kutofuatilia kwa ukaribu.
-wakati mwingine tunawakaribisha "chai".
Ni hayo kwa uchache wake.
Well said kamanda
 
mpaka akashindwa hata kutumia busara
Amefuata SHERIA na sisi Wananchi tujifunze kufuata SHERIA.

Mhandisi Raphael Mlimaji anastahili Pongezi nyingi nashauri apandishwe cheo halafu ahamishwe kabla ya hajalogwa na Wanyamwezi.
 
Kwahiyo staff wa tanroads wawe wanashinda pembezoni mwa barabara kuona nani anapanda mahindi. Ili yasije kuwa marefu bure.

Maana wakikata yakiwa marefu Watakwaza wanyonge wasiojua mashamba yako wapi.
 
Mbona wengine hawafuati sheria na hakuna wanachofanyiwa?sheria za nchi hii zinawabana maskini tu ambao hawana uwezo.akina Gekul wamefanywa nini zaidi ya kufutiwa makosa lkn angekuwa Mlala hoi mpaka leo angekuwa ndani kolokoloni
Kuna neno "mbona" na "angekuwa" ninayafanyia kazi.
 
Kulima mjini/maeneo wanayoishi watu kuna hasara zaidi kuliko faida ya kupata mahindi ya kuchoma.
-kutengeneza mazalia na makazi ya wadudu hatari kwa afya mf.mbu,nyoka,nge,mijusi(hasa kenge wezi wa mayai na mifugo) nk.
-kupunguza au kuziba muonekano mzuri wa vyombo vya usafiri na watu wrnyewe.Hivyo ni chanzo cha ajali.
-huleta vichaka ambavyo hugeuka maficho ya vibaka na wanyama kama mbwa-koko na vimbulu wezi wa mifugo majumbani.
-ni hamasa na maficho ya wabakaji na wapendao kufanya uhuni/matusi vichakani.
-huharibu muonekano mzuri na mpangilio wa mji.Mahindi na mtama siyo maua.
-ni chanzo chema cha kufundishia watu hasa watoto udokozi wa mazao.
-ni uendelezaji wa tabia za kijima za kutotaka kuelewa shamba ni nini na barabara/makazi yako wapi.
-huzuia muonekano na mapito ya miundombinu ya umeme,maji,nyaya za simu/mkongo wa taifa na mabomba ya mafuta.
-hupunguza upana wa miundombinu yaani barabara na huduma zilizopo karibu yake.
-ni chanzo cha ugomvi wa kugombea mazao husika.
-huleta ugomvi na wapitanjia mara tu wakanyagapo,kung'oa au kugusa mazao.
Ni hayo kwa ufupi.
Huongeza mmomonyoko wa udongo
 
Meneja wa TANROADS mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji, awajibishwe kwa kitendo chake cha kinyama cha kufyeka mahindi kwa kisingizio kwamba yamepandwa kwenye hifadhi ya barabara.

Kama kweli yuko makini alikuwa wapi siku zote mpaka mahindi yakakua kiasi kile. Halafu mahindi yanachukua muda gani kukomaa mpaka akashindwa hata kutumia busara?

Watu wenye roho mbaya kama huyu bwana hawatakiwi kwenye jamii yetu.
Adhabu ya kosa huwa haijali faida au hasara kwako, ikitolewa adhabu ya kuukata mkono wako utakatwa, ikitolewa adhabu ya kufungwa utafungwa tu bila kujali nani atawatunza watoto wako.
 
Meneja wa TANROADS mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji, awajibishwe kwa kitendo chake cha kinyama cha kufyeka mahindi kwa kisingizio kwamba yamepandwa kwenye hifadhi ya barabara.

Kama kweli yuko makini alikuwa wapi siku zote mpaka mahindi yakakua kiasi kile. Halafu mahindi yanachukua muda gani kukomaa mpaka akashindwa hata kutumia busara?

Watu wenye roho mbaya kama huyu bwana hawatakiwi kwenye jamii yetu.
Yaani anafyeka chakula?
 
Hivi,ni sheria mpya ya kukataza kulima kandokando mwa barabara(hasa mjini kwa kipimo cha mita kadhaa)tangu lini?Kutokujua sheria siyo kinga ya wakosaji.Mkiteteana hivyo mtaanza kulima hadi ndani ya maofisi yenu.
Huwa kuna katazo kufanya shughuri za kilimo,biashara.ujenzi.Nk
jambo la kushangaza ni pale wahusika kuruhusu kazi hizo kufanyika wakati wapo na wanatakiwa kufanya ukaguzi Mara kwa Mara
Pamoja na kushindwa kubaini hilo, ingetumika busara kusubiri wavune kwa kuwa mahindi siyo zao la kudumu
 
Uko sahihi kabisa ila wangewakataza tangu wanalima na kuandaa masha,ba, namkumbuka Mzee Kikwete aliwahi kuwahoji akina Magufuli (akiwa Waziri wa ujenzi), kuwa mnawaona watu wanajenga, mmekaa kimya, wanahamia, mmekaa kimya, then ghafla mnakuja kuwabomolea. Nadhani hapa kulikua na uzembe wa kutosimamia sheria.
Wewe hiyo sio kazi yake kuanza kuhoji wakati wanajuwa hili ni eneo la hifadhi ya Barbara safi iwe funzo Kwa wrngine
 
Kwahiyo staff wa tanroads wawe wanashinda pembezoni mwa barabara kuona nani anapanda mahindi. Ili yasije kuwa marefu bure.

Maana wakikata yakiwa marefu Watakwaza wanyonge wasiojua mashamba yako wapi.
Mm bado sielewi hii akili ya wabongo kwani wakipanda [emoji535] kandokando ya barabara yanaharibu nini?
 
Meneja wa TANROADS mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji, awajibishwe kwa kitendo chake cha kinyama cha kufyeka mahindi kwa kisingizio kwamba yamepandwa kwenye hifadhi ya barabara.

Kama kweli yuko makini alikuwa wapi siku zote mpaka mahindi yakakua kiasi kile. Halafu mahindi yanachukua muda gani kukomaa mpaka akashindwa hata kutumia busara?

Watu wenye roho mbaya kama huyu bwana hawatakiwi kwenye jamii yetu.
Angalia mambo ya hao watu TANROAD ukiyagusia sana huchelewi kupigwa ban watch out
 
Asante sana kwa matusi. Uzuri wa JF mtu anaweza kuandika cho chote kwa sababu anayemlenga hamjui. Naambatanisha presentation "MAFUNZO MAALUM JUU YA MATUMIZI SAHIHIYA HIFADHI YA BARABARA...".
Mambo ya hao jamaa wa TANROAD kua makini usiyagusie sana utachezea ban mkuu watch out usiseme sikukwambia
 
Injinia Raphael Mlimaji 👊👊👊 chukua tano kwa kazi nzuri.

Hii Nchi watu hawafuati Sheria unakuta akina so called "Machinga" wanauza bidhaa zao Barabarani maeneo yetu yaliyowekwa kwa ajili yetu sisi wapitanjia.

Ni wakati sasa tuwe tunaandaa TUZO kwa watu kama huyu Mhandisi.
 
Mambo ya hao jamaa wa TANROAD kua makini usiyagusie sana utachezea ban mkuu watch out usiseme sikukwambia
Naamini tunaweza kuelimishana/kukosoana humu kwenye JF bila matusi. Unataka kuniaminisha kuwa wale wenye uwezo wa kuwa"ban" wenzao wanaweza kuandika cho chote pamoja na kuwatukana wenzao? Je "credibility" ya JF haitakuwa "jeopardized" tukiendekeza hivyo. Mimi binafsi naiheshimu sana JF na ndiyo maana nilijiunga. Nakushukuru sana kwa "warning".
 
Naamini tunaweza kuelimishana/kukosoana humu kwenye JF bila matusi. Unataka kuniaminisha kuwa wale wenye uwezo wa kuwa"ban" wenzao wanaweza kuandika cho chote pamoja na kuwatukana wenzao? Je "credibility" ya JF haitakuwa "jeopardized" tukiendekeza hivyo. Mimi binafsi naiheshimu sana JF na ndiyo maana nilijiunga. Nakushukuru sana kwa "warning".
Nimesemaje hao jamaa unawazungumzia wazungumzie kwa tahadhari usije ukachezea ban mkuu uwe unaelewa sijasema kuhusu wanaotoa ban nimesema kuhusu unaowazungumzia wana power ya kuweza kucommand wewe upigwe ban na ukapigwa ban copy that?
 
Back
Top Bottom