Mengi and Litigations

Mengi and Litigations

Status
Not open for further replies.
Mkuu Mwanakijiji,
Wee Umeamua kugeuza tu kwa manufaa yako binafsi na mapenzi yako binafsi kwa Mengi au?

sijageuza lolote; kwanini ushuku motives zangu wakati mimi sijashuku za kwako? umepost ulivyoona na miye nimepost "mtu mwingine" anavyoweza kuona.
 
[quote=mkereme;404601]Tatizo ni kwamba hawakutaka mtu mweusi amiliki himaya ya viwanda na MEDIA ya ukubwa wa IPP.

Wewe nani kakuambia haya? huku ni kutafuta sababu za kuanzisha ubaguzi rangi. Tafuta hoja za maana achana na hizi za watu wasio na upeo mkubwa. Hakuna mtu anayegombana na Mengi sababu ya rangi yake bali inaonesha mzee ni bingwa kutafuta au kununua ugomvi na mara zote kutumia wananchi kama ngao(human shield). Uzoefu pia unaonesha hajui maana ya ushindani wa biashara kwani kila mtu akiingiza katika soko bidhaa zinazoleta ushindani na zake kinachofuata ni bifu. Haya ya ufisadi ni janja ya nyani sema kwetu sisi tunafaidi acha wao wapambane waumbuane wananchi wapate kuwajua viongozi wao.[/QUOTE]

HApa kuna harufu ya ukweli, wagombane wao kwa biashara zao wanatafuta support kwetu ETI TUNACHUKIWA KWA VILE TUNAFICHUA UFISADI. mbona wanaowataja kwa majina hawajachuykiwa?????????
 
Hapa kijijini kuna watu wengi wanatoa hasira zao bila kutafakari.Kwa mtizamo wa watu wengi ambao upeo wao wa kuona sio mbali zaidi ya pua zao wanafanya mzaha na vita vya Kibiashara iliyopo kati ya Wahindi/Waarabu wanaofanya biashara na IPP inayomilikiwa kwa asilimia kubwa na familia ya Reginald Mengi . Kabla sijawapatia data nilizo nazo nawaagiza wote akiwepo MzeeMwanakijiji kuanzia leo mtembelee mahoteli yote yanayomilikiwa na akina Subash Patel,Ladwa na yote makubwa ambayo yako chini ya uongozi wa menejimenti za waasia kama mkikuta bidhaa za IPP group zinauzwa huko. Ni nadra sana na hii ipo hata kwenye migahawa mingi. Watakuambia hatuuzi Cocacola kwa sababu za kidini. Kwa vile fomula ya Coke ni ya kimarekani hata huko Uarabuni haziuzwi eti ni solidarity ya kupinga Mmarekani na nimeyaona kwa macho yangu nilipotembelea mashariki ya kati hivi karibuni. Tatizo ni kwamba hawakutaka mtu mweusi amiliki himaya ya viwanda na MEDIA ya ukubwa wa IPP. Serikali ya CCM hilo wanalijua lakini hawataki kulizungumza hadharani. Hasa awamu ya fisadi Mkapa hilo lilinguruma na yeye alitoa macho na kuona sawa. Kwa sababu CCM wamejaa MAFISADI kwa hiyo mpambano umekuwa mkali hata makakati wa kununua Habari Corporation ni moja ya njama za kummaliza Mengi. Kutokana na msimamo Imara alio nao dhidi ya mafisadi anaadhibiwa. Bahati mbaya hakuna kabila la Wachaga ni bahati iliyoje, Mungu aliangusha Mnara wa Babeli kwenye maporomoko ya Mlima kilimanjaro kwa hiyo tuna bahati wao wenyewe kwa weneyewe hawaelewani hata lugha! Inatakiwa ubaguzi huu wa kibiashara ukomeshwe vinginevyo sitashangaa watu kukataa kununua maji ya Uhai na mikate ya Azam kwa vile tu mmliki wake ni Mwislamu.Kuna huyu jamaa kasema anazima TV HUKO ni kujinyonga punguza hasira nadhani ukipewa baruti hukawii kujilipua! CCM huko mnakotupeleka sio kuzuri. WANAKIJIJI badala ya kuorodhersha idadi ya watu waliokwisha kuingia kwenye mgongano wa kimaslahi na IPP {sipendi kuzungumzia watu} tuliangalie hili kwa mapana yake tusiishie kumjadili mtu hapa.Kuna wazo limetolewa MENGI ashauriwe ajitolee kutoa muda hewani bure kuendesha mijadala ya wazi kwenye ITV na sisi tuchangie pamoja na kwezesha kila Kata iwe na UMEME/TV watu waweze kushiriki huo mjadala. Vinginevyo tutabakia na maoni yale yale ya watoto wa mjini tu. Tuache porojo na ushabiki usiokuwa na mwelekeo.

JF siku hizi imekuwa WANAKIJIJI? au hili ni bandiko la kuleee na sasa mnaleta COPY PASTE ZENU HAPA
 
Mengi VS Manji,Mengi Vs Comedi,Mengi vs Mkapa,Mengi VS Masha,Mengi vs Mtikila,Vs RA? Gembe VS Mengi

Hahahaha! Mengi VS Gembe,your next my friend,the fact that you have asked this you must be on the payroll of 1 of Mengi's many real and IMAGINARY ENEMIES.I personally find him paranoid.

I once read an indian proverb which went 'a real winner does not take stress from others and complain but gives stress to others and let them complain'
 
duh! duh! duh! yap,yap,yap, ebwanaeee...
 
Hahahaha! Mengi VS Gembe,your next my friend,the fact that you have asked this you must be on the payroll of 1 of Mengi's many real and IMAGINARY ENEMIES.I personally find him paranoid.

I once read an indian proverb which went 'a real winner does not take stress from others and complain but gives stress to others and let them complain'

Mie Ugomvi na mengi utatoka wapi?sina mwanamke Mkali ambaye anaweza kumvutia,sina haja au Fursa ya uongozi wala sina ukaribu na Mkulu.


Kuna vitu hapa watu naona mnaongea juu juu tu,hivi jitihada za mzee kuwasaidia masikini ni kuwapa chakula na kula pamoja na JK? alafu baadaye unamuacha anaendelea kuwa omba omba?hivyo ndivyo kuwasaidia masikini,tena mara moja kwa mwaka?and why?

Suala la pili,Naomba mtu achanganue ni kwa kiasi gani mzee Mengi ameweza kufanikisha suala la kuondoa umasikini,aidha kwa kutoa mikopo midogo midogo kwa wananchi masikini ama kuwa na mradi enedelevu wa kusaidia masikini?
Watanzania ndivyo tulivyo na ni tabia yetu kushabikia mabo mengine ambyo si ya msingi na kusahau shida zetu.

Hoja yangu kuandika haya nilitaka kuamsha hisia za watanzania ili watambue ni nini kinaendelea hapa nchini mwetu,kama utakuwa umefuatilia kwa ukaribu toka mwaka 2006 uanze utaona ni jinsi gani magazeti ya nyumbani yalivyoshindwa kujadili masuala muhimu yahusuyo maisha ya wananchi wa kitanzania,khali duni ya watananzania,nini wanahitaji ili waweze kusonga mbele

Hata wahisani wetu,mabalozi wameshindwa kujua matatizo ya nchi yetu kwa kuwa kila siku wamekuwa wakisoma habari za ugomvi wa watu tu ukiachilia suala muhimu la fedha za EPA,wanasiasa wamekuwa wakirumbana wao kwa wao bila kuelezea ni nini wanataka na kwa faida ya nani.

Kwanini nimeanza na Mzee Mengi,ni kwasababu yeye ndiyo anomiliki magazeti mengi na amejiingiza katika siasa ya maji taka kwa kuwa na urafiki na wanasiasa wanopenda siasa za kuchafuana,wamekuwa wakitumia gazeti lake kupitia yeye ili kuchafuana wao kwa wao ambayo haitusaidi sisi.

Ndugu watanzania wenzangu,
Ni matatizo mangapi yanaendelea huko vijijini na hatuyafahamu?Je nani aliyejua kuwa wilaya ya Bagamoyo hakuna hata gari la kuzimia moto?Je kwanini wandishi wa kitanzania hawafanyi habari za utafiti na kuandika habari za kila jimbo huku wakipima maendele yaliyoletwa na mbunge aliyepo madarakani?

Imetosha sasa,Nilimuunga mzee mwanakijiji pale aliposematuanze Moja,wale wote walitufikisha hapa waachwe tu na tuanze upya kujenga taifa letu kwa kuwa miaka inazidi kwenda na tunaendelea na blah blah,siasa za kuchafuana,tunafurahia siasa hizi za maji taka,na hii ina maanisha kuwa tunawacheka walio masikini nakufurahia umasikini wao.

We need to change!
 
Last edited:
Nilikua namkubali sana Bagenda kabla sijaujua undani wake..nasikia ni strategist mzuri sana wa sabotage(sasa sijui ni kiintelijensia,kisiasa au kiuchumi)...mwenye tetesi zake na Libya connection enzi za Ghaddafi vs US amwage hapa....
 
Mheshimiwa Gembe jibu langu lilikuwa kwenye utani zaidi na wala sijapinga hoja yako na hata mimi hushangaa kuitwa masikini kula pilau Diamond halafu usiku analala viwanja vya Mnazi mmoja.
Huwezi pambana na ufisadi 'when it suits you' nani asiyejuwa mchango wa mengi kuiuwa NBC na NIC enzi zilee na alivofanya juu chini majina yasichapishwe magazetini?
 
Mheshimiwa Gembe jibu langu lilikuwa kwenye utani zaidi na wala sijapinga hoja yako na hata mimi hushangaa kuitwa masikini kula pilau Diamond halafu usiku analala viwanja vya Mnazi mmoja.

lagatage,
Tupo ukurasa mmoja mkuu!
 
Mheshimiwa Gembe jibu langu lilikuwa kwenye utani zaidi na wala sijapinga hoja yako na hata mimi hushangaa kuitwa masikini kula pilau Diamond halafu usiku analala viwanja vya Mnazi mmoja.
Huwezi pambana na ufisadi 'when it suits you' nani asiyejuwa mchango wa mengi kuiuwa NBC na NIC enzi zilee na alivofanya juu chini majina yasichapishwe magazetini?

lagatage,
Tupo ukurasa mmoja mkuu!

Na mimi msiniache,
mpaka magazeti yalumuambia "DAWA YA DENI NI KULIPA" kizazi cha enzi za EPA hakiyajui haya, sijui alililipa madeni hayo? hili la PILAU LIMENIACHA HOI BIN TAABANI.
 
Na mimi msiniache,
mpaka magazeti yalumuambia "DAWA YA DENI NI KULIPA" kizazi cha enzi za EPA hakiyajui haya, sijui alililipa madeni hayo? hili la PILAU LIMENIACHA HOI BIN TAABANI.

Alipe wapi? mpaka kipenzi chetu NBC ikauzwa kwa makaburu na NIC mpaka leo imebaki mifupa tu.Huwezi amini huwa nashikwa na hasira kuona wengi waliouwa STC,NDC,Ushirika,NTC etc leo eti wabunge au wafanya biashara MAARUFU.
 
Kuna vitu hapa watu naona mnaongea juu juu tu,hivi jitihada za mzee kuwasaidia masikini ni kuwapa chakula na kula pamoja na JK? alafu baadaye unamuacha anaendelea kuwa omba omba?hivyo ndivyo kuwasaidia masikini,tena mara moja kwa mwaka?and why?
Mbona hujiulizi kwa nini kila sikukuu RAIS anatoa msaada wa kiroba cha mchele na mbuzi na baadae anawaacha?


Naomba mtu achanganue ni kwa kiasi gani mzee Mengi ameweza kufanikisha suala la kuondoa umasikini,aidha kwa kutoa mikopo midogo midogo kwa wananchi masikini ama kuwa na mradi enedelevu wa kusaidia masikini?
Binadamu haendelezwi bali hujiendeleza-Madela Madilu
Yani unategemea Mengi ndio atoe misaada ya kuwaendeleza huyo JK na mabilioni yake lakini amechemka

Hoja yangu kuandika haya nilitaka kuamsha hisia za watanzania ili watambue ni nini kinaendelea hapa nchini mwetu,kama utakuwa umefuatilia kwa ukaribu toka mwaka 2006 uanze utaona ni jinsi gani magazeti ya nyumbani yalivyoshindwa kujadili masuala muhimu yahusuyo maisha ya wananchi wa kitanzania,khali duni ya watananzania,nini wanahitaji ili waweze kusonga mbele
Mbona wamiliki wa magazeti hayo wako wengi RA, Karamagi ,Nyaulawa,Ulimwengu ,Kubeneana mengi yameibuka hivi karibuni but why Mengi

nimeanza na Mzee Mengi,ni kwasababu yeye ndiyo anomiliki magazeti mengi na amejiingiza katika siasa ya maji taka kwa kuwa na urafiki na wanasiasa wanopenda siasa za kuchafuana,wamekuwa wakitumia gazeti lake kupitia yeye ili kuchafuana wao kwa wao ambayo haitusaidi sisi
.
Vipi kuhusu ROSTAM AZIZ

Ndugu watanzania wenzangu,
Ni matatizo mangapi yanaendelea huko vijijini na hatuyafahamu?Je nani aliyejua kuwa wilaya ya Bagamoyo hakuna hata gari la kuzimia moto?Je kwanini wandishi wa kitanzania hawafanyi habari za utafiti na kuandika habari za kila jimbo huku wakipima maendele yaliyoletwa na mbunge aliyepo madarakani?
Haya ndio mambo ambayo tunatakiwa kuyajadili na sio mambo ya Mengi
 
Lakini mngejua Gembe ni nani, naamanisha jina lake halisi msingepoteza muda kujadiliana na naye kuhusu mambo ya Mengi. Ni sawa na Mwiba kumwambia CCM iko bomba
 
Orodha ya watu wanaogombana na Mengi ilikuwapo kwa muda mrefu kutokana na umiliki wake wa vyombo vya habari (TV, radio na magazeti). Watu wengi tu, kwa namna moja au nyingine, walikuwa wanaguswa (ki-ubaya) na vyombo vyake hivyo – na mara ya kwanza kabisa Mengi alikosana na mfanyabiashara mmoja wa Kiasia aliyekuwa anamiliki CTN (nimemsahau jina lake) kuhusu hakimiliki ya kutangaza mechi za World Cup mwaka 1994 kupitia ITV, wakati tu kituo hicho kinaanzishwa.

Mfanyibiashara huyo kumbe alikuwa fisadi maana baadaye alitoroka nchini na fedha nyingi za wafanyabiashara wengine aliowatapeli.

Orodha ya watu wanaogombana na Mengi imeongezeka kwa haraka baada ya vyombo vyake vya habari kuanza kupiga vita ufisadi kwa nguvu zote. Mimi sioni sababu nyingine.

[Chanzo cha vita hii labda kinatokana na yeye kukosa kuuziwa Hoteli ya Kilimanjaro, kwa kile alichokielezea “mchezo mchafu uliofanyika” akimaananisha milungula ilitembea. Katika tukio hilo Masilingi (akiwa waziri wa mambo ya usalama wa taifa) alimtisha Mengi kwa kutamka ”Vyombo vya dola vitamshughulikia.” (Miaka kadha baadaye waziri Masha alirudia kauli kama hiyo dhidi ya Mengi.)]

Kila mtu ana orodha ya watu anaogombana nao, na umaarafu wa watu hawa unategemea na umaarufu wa yule wanaogombana naye.

Manji, kwa mfano, anao maadui wake wengine wengi tu (ukiacha Mengi) lakini hawa hawajulikani kwani Manji si maarufu sana kama Mengi (kwa mtazamo wa jamii) na pia si mmiliki wa vyombo vya habari ambavyo angeweza kuvitumia kikamilifu kukabiliana nao.

Na ni kweli kabisa idadi kubwa ya wale waliomo kwenye orodha ya Mengi ni watu wachafu, au wapambe wao. Kuna wengine wamechomekwa tu kwenye orodha ili ionekane ndefu sana.

Aidha nakubaliana na wale wanaosema thread hii ni mojawapo ya zile ambazo huanzishwa kwa lengo la kuwatakasa mafisadi – eti kwa kujaribu kuelezea kuwa Mengi naye fisadi tu.

Lakini hili wanashindwa kabisa kuthibitisha – hatujapata uthabiti, hata wa kimazingira wa kumfunga Mengi na ufisadi wa kuchota mapesa ya umma kama vile yale ya EPA, Deep Green, Twin Towers, Meremeta n.k.

Wanabakia kusemasema tu mambo yasio na msingi kabisa na diyo maana hata vyombo vya dola havimgusi. Inawezekana alikopa fedha kwenye mabenki (inasemekana alikopa fedha nyingi NBC, wakati benki hiyo ikiwa bado ya umma), lakini kukopa si ufisadi, aliomba, akapewa mkopo, na kama hajarudisha basi hilo ni suala la mdai na mdaiwa – na si jinai kamwe.

Kwa kuangalia tu posts hadi sasa, thread hii inaonekana imekwama -- majority wanapinga ufisadi -- na habari ndo hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom