Mercedes-Benz yauza gari lenye gharama kubwa zaidi duniani (Tsh. Bilioni 330)

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607



Kampuni ya Mercedes-Benz, Ijumaa ya Mei 20, 2022 iliweka rekodi ya kuuza gari la gharama zaidi Duniani, ambalo ni Mercedes-Benz 300 SLR ‘Uhlenhaut Coupe’ ya mwaka 1956 kwa kiasi cha dola milioni 142.7 sawa na Tsh. bilioni 330.

Kabla ya hapo gari aina ya Ferrari 250 GTO ya mwaka 1963 ndilo lilikuwa gari la gharama zaidi, mwaka 2018 liliuzwa kwa kiasi cha dola milioni 70 sawa na Tsh. bilioni 162.

Gari hilo limeuzwa katika mnada ambao waliokaribishwa katika manunuzi yam nada huo ni watu 10 pekee. Mnunuaji hajawekwa wazi lakini amekubali taarifa hizo ziwekwe hadharani

Pesa zilizopatikana katika mauzo ya gari hii zitatumika kuanzisha mfuko wa Mercedes Benz kwa ajili kusaidia ya wanafunzi katika masomo ulimwenguni.

Source: Supercarblondie
 

Hata ukiniuliza uzuri wake uko sijauona
 
Na mimi nipo hatua za mwishomwisho kuitoa IST yangu hapo maji chumvi. Muda si muda wote tutakuwa tunasafiri huku tumekaa,kiti gani ama kivipi huo ni mjadala mwingine.

Hallelujah
 
Walleye hizo pesa TZ
 
Unaweza kukuta Mtu Mwenyewe aliyenunua anatoka Nchi maskini kuliko Zote huku Africa Alafu hapo hapo Nchi yake inaenda kuomba Mikopo nafuu Kwa hao hao wazungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…