Meremeta 00:00:00. EXTRA

Meremeta 00:00:00. EXTRA

Status
Not open for further replies.
- Wakuu tuwajibike japo kidogo tu, copies tunawapatia wananchi wasioweza kuingia hapa JF, lakini kwa wale wote tunaoingia hapa kila siku hakuna excuse ya kutoinunua hii copy toka kwa Mkulu Mwanakijiji, please tupunguze umatonya yaani dola thelathini tu kununua elimu ya taifa lako nayo ni taabu sasa tunaanza kusumbuana huko pembeni, Pleasee! Ahhhgggrrrrr!

Respect.

FMEs!


Mkuu FMEs, shilingi 30,000 ni robo ya mshahara wa mfanyakazi wa serikali na baadhi ya taasisi binafsi nyingi tu hapa nchini hivyo siyo fedha kidogo. Mwanakijiji ameuza ripoti ya Meremeta kwa bei ya kulangua
 
Mkuu ukifuatilia kwa umakini na kiundani hapa JF watu wengi tunatofautiana kwa kipato kama ujuavyo kipato cha kibongo bongo kuna wengine hapa wanafanya kazi mshahara wake hauzidi hata 100,000/= si unajua kazi za wahindi mkuu. Mtu kuchangia anataka sana lakini hali ya uchumi ina mkaba na anataka kupata elimu lakini anashindwa afanyaje ndo anaamua umatonya mbona hata mkuu wa akaya inapo bidi anatembeza bakuri kwa wahisani hali ngumu mkuu na watu tunatofautiana.
Naomba Mwanakijiji baada siku kadhaa kupita tuomba report uianike wazi ili kila raia apate na kufikisha ujumbe kwa ndugu na jamaa. Wakuu twende mbele na kurudi nyuma kipato tunatofautiana kabisaa hili halina ubishi.

Hakika umenena
 
utake usitake hii ni siku ya 3 tangu doc itoke na reporting yao imekuwa slow kuliko nilivyotegemea

sasa kama siyo wao ku colide na establishment kumbe ni nini

strategy zibadilishwe na hawa ma editors naona wanajiona wako kwenye comfort zone sana

si vibaya kuwakumbusha once in a while where they belong na watake watu for granted

yaani kila kukicha na scan magazeti na sioni mpya zaidi ya ile ya mwanzo ya Raia Mwema

nishai kweli hawa jamaa wa mainstream media


UKWELI NI KWAMBA KILA MMOJA ANAJIPANGA NAMNA YA KUJIBU. Wakati wa media kupick hili bado na pengine wahariri ni wavivu wa kusoma kama ilivyo kawaida yetu tulio wengi. Hata hivyo ni risk kubwa kwa media kwa sababu serikali inaweza kuamua kufa naye atakayejitokeza adherani na hii riport kwa kisingizio cha wizi wa nyaraka za siri za serikali. Kila mmoja anatahadhari ya kivyake. Nimefurahishwa na jibu hili

Kwanini ulitegemea hivyo? Mimi sikutegemea hivyo. just FYI wengi wao waliniuliza kama wangeweza kuirusha... jibu langu limezuia hiyo.

Tuna haraka sana, ukitaka haraka unabeba bunduki yako unaenda kwenye kikao cha kamati kuu ya sisiem na unafanya vitu vyako ndipo utapata majibu ya haraka. Harakati zenye hekima kama hizi za mwanakijiji zinahitaji subira kubwa na wote wenye busara wanafahamu hili.
 
Kwa sababu hajaon acha maana bali ni utafutaji tu, nini kipya kilichomo humo? mimi sijailipia na nilisema toka mwanzo silipii na sababu nilizitowa kwa nini silipii na sasa nataka mnambie nini kipya humo? mimi nimeisoma bureeeee, na sijaona jipya! wala lenye maana, uongo mtupu.

Ndugu yangu Dar es salaam, Wasema kweli daima huonekana wakorofi. japo Mwanakijiji na timu yake wanataka tuunge mkono tu na kuwapamba lakini mwitikio kidogo wa vyombo vya habari ni ishara tosha kuwa ripoti imeonekana kuwa siyo ya uchunguzi wa kina. Ilidaiwa kuwa ripoti itakuwa na ushahidi mzito na vielelezo ambatisho, mmmmmh mimi sijakutana navyo kama tulivyoelezwa awali na Mwanakijiji kabla ya kuilipia, lakini zaidi aliikweza sana ripoti hii na hadi kufikia kuiuza
 
Ndugu yangu Dar es salaam, Wasema kweli daima huonekana wakorofi. japo Mwanakijiji na timu yake wanataka tuunge mkono tu na kuwapamba lakini mwitikio kidogo wa vyombo vya habari ni ishara tosha kuwa ripoti imeonekana kuwa siyo ya uchunguzi wa kina. Ilidaiwa kuwa ripoti itakuwa na ushahidi mzito na vielelezo ambatisho, mmmmmh mimi sijakutana navyo kama tulivyoelezwa awali na Mwanakijiji kabla ya kuilipia, lakini zaidi aliikweza sana ripoti hii na hadi kufikia kuiuza


Dah!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ndugu yangu Dar es salaam, Wasema kweli daima huonekana wakorofi. japo Mwanakijiji na timu yake wanataka tuunge mkono tu na kuwapamba lakini mwitikio kidogo wa vyombo vya habari ni ishara tosha kuwa ripoti imeonekana kuwa siyo ya uchunguzi wa kina. Ilidaiwa kuwa ripoti itakuwa na ushahidi mzito na vielelezo ambatisho, mmmmmh mimi sijakutana navyo kama tulivyoelezwa awali na Mwanakijiji kabla ya kuilipia, lakini zaidi aliikweza sana ripoti hii na hadi kufikia kuiuza

Wewe ulitegemea kukutana na vielelezo gani? Wabongo mbona mnapenda ku-criticize sana?
 
Ndugu yangu Dar es salaam, Wasema kweli daima huonekana wakorofi. japo Mwanakijiji na timu yake wanataka tuunge mkono tu na kuwapamba lakini mwitikio kidogo wa vyombo vya habari ni ishara tosha kuwa ripoti imeonekana kuwa siyo ya uchunguzi wa kina. Ilidaiwa kuwa ripoti itakuwa na ushahidi mzito na vielelezo ambatisho, mmmmmh mimi sijakutana navyo kama tulivyoelezwa awali na Mwanakijiji kabla ya kuilipia, lakini zaidi aliikweza sana ripoti hii na hadi kufikia kuiuza

Kwa hali hii kweli Tanzania tunamwendo mrefu wa kuleta mageuzi,kuna watu wanamacho lakini hawaoni,wanamasikio lakini hawasikii.Sasa kama kilichopo kwenye ripoti hakitoshelezi wewe mchango wako ni upi ili ripoti ijitosheleze.

Tusiwe wepesi wa kukritisize tutoe michango ya mawazo na vitendo kuboresha juhudi za kumkomboa mtanzania toka kwenye kongwe la ukandamizaji.Binafsi nimeiona ripoti na on the balance of probabilities kama shutuma zilizopo ndani hazijibiwi kwa ufasaha,serikali iliyopo madarakani itabidi iwajibike kwa kuukalia uvundo huu.
 
meremeta2.jpg

Tunawashukuru kwa mwitikio wenu lakini kwa hakika mmetupa kibarua kipya kabisa na kazi imekuwa ngumu katika hiyo ripoti. Kutokana na ongezeko kubwa la watu wapya ambao wangependa kupata ripoti hii hasa wale ambao ndio wamepata tu taarifa zake tumeamua kuongeza nakala 50 tu hadi hii Ijumaa.

Maelezo ni yale yale na utaratibu ni ule ule wa kupata.

Pamoja na hilo, jana nilizungumzia kwanini tumefanya hili tulilolifanya na tunasukumwa na kitu gani ili kusiwe na utata wowote.

Sikiliza:

juuyameremeta.MP3 - Bonyeza

Inapatikana hivi:
Ripoti inapatikana kwa njia ya pre-ordering (yaani order zikishatimia zote zinatolewa kwa wakati mmoja) kwa wale ambao watachangia dola 30 au shilingi elfu thelathini tu au zaidi kwa njia zifuatazo:


  • Kupitia Mtandao wa http://www.mwanakijiji.com kuna kitufye cha kuchangia upande wa juu kulia (Donate Button) cha Paypal Inc., kwenye ukurasa wa mbele (homepage - siyo ukurasa wa forum). Hapo tunaweza kupokea malipo ya kadi za kibenki katika njia ya usalama wa hali ya juu na wachangiaji wote wanamakia sirini (rekodi yetu ya miaka mitatu hatujawahi kuvujisha jina la mchangiaji yeyote yule!).Kadi za Visa, MasterCard, Express zinapokelewa.
  • Kwa taasisi au watumishi wa umma (VIPs) ambao kwa sababu za wazi wangependa kutojulikana wasiliana nami kwa email au Private Message na utapata maelezo ya kuwasiliana na Mwandishi wa Habari Mchunguzi wa gazeti la kiingereza la kila siku la nchini aliyepo Tanzania ambaye atapokea fedha hiyo pamoja na email yako ambayo tutakutumia nakala hiyo katika usiri mkubwa. Yeye pia anaweza kupokea kwa njia ya Western Union kwa wale ambao wangependa kutumia njia hiyo.
  • Kwa mtu mwingine yeyote tuma fedha kwa njia ya recharge vouchers kwenda namba: 0713444649. Vouchers ziwe ni za tiGO, Zain au Zantel.
Kama mipango yote itakwenda ilivyo, basi tunatarajia kutuma nakala hizo 100 siku ya Jumatano wiki hii kwa wale waliochangia. Hivyo ina maana watu wana siku tano za kukamilisha oda zao. Pamoja na ripoti hiyo, tumeambatanisha pia ripoti yetu ya 2006 juu ya “Tracing Reports of Tanzania’s role in arms trafficking”.

Oda nakala yako mapema kwani tutafanya kwa mtindo wa “aliyewahi mpe” – first come, first serve.

NB: - Email moja kwa nakala moja.
- Hakuna nakala itakayotangulia mchango; na hakuna mtu atakayepata nakala kabla ya watu wengine. Watu wote watakaokuwa wamechangia watapata nakala zao Jumatano. NO EXCEPTION.

Shukrani

M. M. Mwanakijiji
Consortium of Concerned Tanzanians Intl.
+ 1 248-556-6748

unaweza kwenye email ya mwanakijiji ati jamiiforums dot com





[/CENTER]


Wadau baada ya Meremeta, tuanza kuwakama watoto wa mafisadi ili warudishe hela zetu. tumechoka kweli tena. Kidnapping will solve the matter
 
Wadau baada ya Meremeta, tuanza kuwakama watoto wa mafisadi ili warudishe hela zetu. tumechoka kweli tena. Kidnapping will solve the matter

that will not solve the issue. Hela zimeshakwenda na kuliwa. All we can do is start with a new clean slate. Bila hilo, tutabaki tukiumizana tu. Tuige mfano wa Mandela. Wewe unadhani angeamua kulipa injustices zote, leo SA kungekalika? Sometimes you have to be the bigger person, and say we forgive you. Turudishe tunachoweza...mfano kuvunja mikataba hovyo, lakini kudai personally sio sawa. Hata ukisilikiza audio ya MWJJ inasema hatutaki mali zao, bali tunataka resources zetu. Tukianza kudai katika personal level, itakuwa ngumu kuwatoa hapo.
 
Sorry Mkjj kuuliza

Hatupati kabisa hii kitu sie akina hohe hahe? maana nilijua eventually watu wakipata na sie tupewe walau na sie tupate hoja au somo hilo la wizi wa kodi zetu ambazo wengine zinatufanya hata kununua kopi hii inakuwa shida au inakuwaje maana tunahitaji uhasishaji kama huu ingawa wakati mwingine majukumu yanakuwa yamebana kiasi chake au watu 150 bado au badi una list ingine tena ya kuongeza may waombaji wameongezeka?.

I appreciate you all effort man
 
Bandugu,

Hii ripoti ya Meremeta kupitia Cheche bado inapatikana? Kivipi?
 
wakuu si mshaisoma......wekeni torrent au rapidshare tuinyonye....
 
Huwa tunapata doc za ufisadi kwa namna tofati leo hii haipatikani kabisa; mwanakijiji achia kidogo basi; au umewapiga ganzi hata wale walio lipia tayari? inakuwaje; nataka kusambaza ujumbe ila sina documents mkuu
 
Huwa tunapata doc za ufisadi kwa namna tofati leo hii haipatikani kabisa; mwanakijiji achia kidogo basi; au umewapiga ganzi hata wale walio lipia tayari? inakuwaje; nataka kusambaza ujumbe ila sina documents mkuu


duh.. wenzio wameanza kudownload hapa masaa kadhaa yaliyopita. Angalia threads za hapa..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom