Meremeta Report: Released to the Public (Revised & Free!)

Meremeta Report: Released to the Public (Revised & Free!)

Sorry wakiipiga chenga kama kawaida inapelekwa kwa wananchi na hapo ndipo game itaanza upyaaaaa

Wananchi watapewa T shirt, kofia, kanga na pilau watafurahi na watasahau kuwa wanowapa hivyo vitu ndio washtakiwa. Ona sasa uchaguzi wa serikali za mitaa ni October takribani miezi miwili na siku kumi upinzani umejitayarishaje na uchaguzi huo?

Zingatia pia kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa ndio msingi na uchaguzi mkuu. Kama mpaka sasa upinzani hauna vuguvugu la uchaguzi tutegemee hukumu gani toka kwa wananchi
 
Mimi bado sijajiandisha katika daftari la kupiga kura, ninapatwa na kigugumizi juu ya hilo kwa sababu ya wizi wa ccm katika zoezi zima la kura. hivyo naona hata nikijiandisha nikapigia chama kingine bado sisiemu watapita kwa wizi wao. nikiona upinzani wamekaa vizuri nitajiandisha na kuwapa kura yangu kuliko hawa mafisadi.

Wahi kujiandikisha ushindi katika uchaguzi unaamuliwa na kura zinazozidi, kura yako inaweza kumake a very big differrence, imagine mkiwa watu elfu moja kama wewe inamaana watu elfu moja wanaotaka mabadiliko hawatapiga kura. Hamasisha wewe na wenzio mnajiandikisha na msikose kupiga kura Oktoba 2010.
 
sijui wangapi ambao wameisoma hii ripoti bado wataipigia kura CCM!

Kwanza Mzee mkjj ninashukuru kwa kuwa na moyo wa kizalendo na wenye nia ya kweli na kuleta mabadiliko.

Nadhani soluhisho muhimu ni kuondokana na na dhana a uchama uchama. tuchague watu.pia bungeni ile ajenga ya wagombea binafis ilurudishwe. naamini kuna wtu wengi safi hawataki kujihusisha na vyama kama wapiga kura wengi pia hatuna vyama.

Lakini pia tukisema tuchague watu na si chama linakuja tatizo lingine Viongozi waadilifu, wazalendo wa kweli kwenye pande zote mbili za shilingi( UTAWALA na UPINZANI) ni wachache. ndio maana suala la mgombea binafsi liluridhswe kurudisha imani kwa wapiga kura.

Mtazamo wangu ni kuwa tuanahitaji Rais awe wa CCM na wabunge wengi zaidi watoke upinzani au wawe binafsi

Wananchi wanachagua au tunachagua CCM si kwasababu ni chaguo letu bali ni ile kauli ya zimwi likujualo. Wapinzani wanahitaji kufanya kazi zaidi ya wanayofanya sasa. TRUST kwa wananchi ni ndogo.

Mimi nadhani vita nzuri sio kuhangaika kuwang'oa CCM madarakani. itatuchukua muda sana kwa hali halisi. Vita nzuri ni kufunua uozo kama huu. Kuanika utendaji kazi mbovu za taasisi kama tume za maadili, Jeshi, EPA, Richmond. meremeta nk.

CCM Wao wenyewe huko jikoni kwao watanyoosheana vidole, kuchambuana na baadae kutengana.Kwa syle hii CMM original aliyoitaka mwalimu nyerere itarudi na labda tunaweza kuanza kujikongoja tena baada ya kuchechema kwa zaidi ya miaka 40 sijui ni ya uhuru au ufungwa?
 
Asante MMK kwa ripoti nzuri, ila ina mtazamo wa ki"conspiracy theory" zaidi kuliko factual labda hizo habari mlizozizuia zinaweza kutoa majibu ya maswali mengi ambayo hayana majibu ya moja kwa moja

Unfortunately conspiracy is the substance of the whole Meremeta saga; huwezi kuelewa Meremeta bila ya kuelewa njama nyuma yake. Na ndiyo, kuna mengine ambayo hatujayaweka lakini ni rahisi mtu mwingine yoyote kuyapata na kuthibitisha tunachokidai.
 
Mkuu pole na hongera kwa kazi nzito really umeonyesha uzalendo wa hali ya juu. Nimepitia ripoti hii, aaaaghrrrrrr! samahani nashindwa kuendelea lakini nadhani unahitajika mwitikio wa ziada. Tumekuwa too wordy.
 
Wananchi mkiletewa kanga, tshirt na bahasha chukueni wala msiache maana ni ,ali yenu ndo mnapewa, ila kwenye sanduku la kura wakaangeni hao ccm.
 
Mkuu nimeipitia hii ripoti kwa undani..

Imauma sana na ina tia aibu sana pale tunapojiita taifa lenye amani utlivu na utawala wa sheria.
Hivi hata kama kuongopa nako mpaka uende shule,....???

Maana takwimu zinawasuta,usajili wa hayao makampuni ndo usiseme kabisaa,...

Naomba niwaulize wajuzi wa humu JF mnijuze kidogo kuhusu hili;

Yale yote anayozungumza waziri akiwa bungeni anaandaliwa na nani ama anaandaa mwenyewe?

Na pili takwimu hizi (mfano uzalishaji wa meremeta) anaziandaa nani na zinakua chini ya waziri husika kwa kipindi hicho ama zinakuwepo wizarani kama kumbukumbu ya yeyote atakaye baada ya huyo aliye madarakani kuja azisome kama ref?

Hapa naanza kuona ni kwanini tulicheleweshewa mawasiliano,kama redio tv na hata barabara kwa makusudi ili wanachi walio wengi wasiweze kuyasikia madudu haya yanaposomwa bungeni tena kwa majisifu na unafiki mkubwa.

Huu msemo wa mwana JF usemao"Miafrica ndivyo tulivyo,...." naona una ukweli ndani yake.
 
Mi naweza hata kulia ninapoisoma. Nadhani ni laana kwenye nchi yetu. Hakuna hata mmoja mwenye uchungu na nchi hii. Na hata hao wachache wenye uchungu wananyamazishwa either kwa kutishiwa kunyang'anywa uanachama ama kuuawa kabisa.Natamani kuhamia Rwanda....
 
Duuu! kweli sasa hivi mambo yanakwenda behind the curtain, na kama tusipokuwa makini hata humu JF tutapigwa kizungumkuti maana naona hata namba ya members sasa hivi inaongezeka kwa kasi sana hasa baada ya kutoka ripoti ya Meremeta


Hizo ni mbinu za kisasa tu mkuu zisikupe preshaaa!!!!. Hata mauzo ya jezi ya Real Madrid yalipanda ghafla pale CR7 alipohamia Benabuu. Ni mbinu za kiuhamasishaji tu...
 
Hii thread najua itakuwa ndefu sana. Cha msingi tujitahidi wakuu tusiwe off topic - kuongea vitu visivyo ndani ya mada.
 
Its like Novel sikutarajia nilichokisoma,good lucky guys na Amani ya Mungu iwatangulie mfanikishe kile kilichowaleta Duniani.....Inamaanishwa tutaongozwa na genge la wahuni wa kimataifa???? ni ukweli mchungu
 
Mi naweza hata kulia ninapoisoma. Nadhani ni laana kwenye nchi yetu. Hakuna hata mmoja mwenye uchungu na nchi hii. Na hata hao wachache wenye uchungu wananyamazishwa either kwa kutishiwa kunyang'anywa uanachama ama kuuawa kabisa.Natamani kuhamia Rwanda....
Bado najivunia kuwa Mtanzania, sitamani kamwe kuwa na utaifa mwingine zaidi ya utanzania. Tanzania njema itatokana na sisi, kuyakimbia matatizo si suluhisho la matatizo yenyewe
 
Asante sana MMK kwa kazi hii nzuri sana. Nimeisoma mara mbili mbili na kuielewa vizuri. Niaibu na inatisha sana labda ndio maana wengine wanaogopa kuigusa na gungangania kuwa ni siri ya kijeshi.

Je unajua kuwa DeBeers ndio walo mgodiwa mwadui? Utendaji wao ni huo huo wa kutokufuata taratibu. Mwaka 1997 na 98 nilikuwa naenda sana Shinyanga kwa rafiki yangu na nilieleza kuwa wanachimba kwa nguvusana bila kufuata any systematic way, nasikia hata uwanja wandege walichimbia bora wasikie kuna almasi nyingi. Ile ilikuwa looting kabisa.

Tuomb Mungu atusaideie na hawa washindwe

Asante sana na Mungu akubariki katika kazi zako
 
Wananchi mkiletewa kanga, tshirt na bahasha chukueni wala msiache maana ni ,ali yenu ndo mnapewa, ila kwenye sanduku la kura wakaangeni hao ccm.

Unachosema ni cha kweli, Tatizo watanzania wengi hatuna elimu ya URAIA. Tunaogopa kuwakaanga Mafisadi wa CCM tukizani watajua kuwa hatukuwapa kura zetu. Kuna kila sababu ya kusambaza elimu ya uraia nyumba hadi hadi nyumba.
 
Mmmmmmmmmmhhhhhhhhh! Presha inapanda presha inashuka asante kwa kutukumbuka tuanaendelea kuisoma hii ni kiboko kwakweli.... Ubarikiwe sana Mkuu
 
thanks alot MMK
let us read it carefully
 
thanks alot MMK
let us read it carefully
Wana JF na MMK,
Nakushukuru sana kwa Taarifa hii nzuri pamoja na marekebisho yake. Sasa iwe Bungeni au nje ya Bunge, Serikali lazima itoe maelezo ya kina. Hakuna eneo la Serikali ambalo halihojiwi na Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 63(2)(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tushikamane hadi kieleweke na majibu sahihi yapatikane.
 
Wana JF na MMK,
Nakushukuru sana kwa Taarifa hii nzuri pamoja na marekebisho yake. Sasa iwe Bungeni au nje ya Bunge, Serikali lazima itoe maelezo ya kina. Hakuna eneo la Serikali ambalo halihojiwi na Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 63(2)(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tushikamane hadi kieleweke na majibu sahihi yapatikane.
Tumechoka sasa na kudanganywa inabidi ku-take action wenyewe. Na hili tunaliweza sana tu ni suala la muongozo nini kifanyike na itakuwa hakuna cha nani afanye ni jukumu la kila Mtanzania ambaye sio fisadi, mwizi wala mla rushwa
 
Back
Top Bottom