Mimi kila mmoja namuangalia kwa aina yake ila ronaldo kwa kweli namkubali sana kwanza kitendo cha kutamba england na anaenda kuleta upinzani mkubwa kule spain hili si jambo dogo kabisa ambalo messi bado hajalifanya, kuhusu mechi ile ya elclassico sijavutiwa nayo kwa kuwa unaposhinda pambano la ngumi baada ya mwenzako kuteuka mguu mmoja bado nakua silidhiki na ushindi huo(11 kwa 10).
Nitamuomba messi akavunje marekodi huko kwingine hasahasa england. Nikimuangalia messi ana aina ya mchezo wake ambao utaupata spain tu au katika team inayofundishwa na mtu kama guadiola lakini ronaldo nae ana aina yake ya mchezo kwangu mimi huu mchezo unaweza kuupata sehemu nyingi ya dunia ndio maana huyu ronaldo anaweza enda leta upinzani mkubwa ligi yoyote ile atakayoenda cheza