Messi vs Ronaldo: Nani zaidi?


Kaka acha maneno weka CV tulinganishe... Ronaldo ni sawa na Canavaro tena canavaro nae ana world cup anampita ronaldo maana uchezaji bora wa dunia anao na world cup gold medal juuuu... Ronaldo bado sana.. Na kama ulikua ujui world cup ya 2014 inabaki south america na messi anakamata glory hiyo hata kama haters hamtaki
 

Lazima messi akabwe na wengi kwakuwa passi zote za barca huwa zinaelekezwa kwake akamalizie. Labda kama messi yupo mbali ndo mtu mwingine anaweza ku attempt kufunga. Madrid kuna uchoyo Wa passi kwa kila mchezaji na ndo maana wafungaji ni wengi tu. Nadhani CR7 ni zaidi ya messi hasa ukiangalia mazingira ya uchezaji ya timu yake ukilinganisha na barca na messi.
 
Sasa mbona hueleweki wewe unatoa CV then unashindwa kuitetea? Kama issue ni kubeba WC hata Messi so far hajachukua World Cup so kutokana na vigezo vya kuchukua WC hata kina Kleberson,Arbeloa,Luca Toni ni bora kuliko Messi na Ronaldo
 

Hata Lionel messi angekuwa Real Madrid angetisha kajamaa kana super talent tukubali tukatae japo hatukapendi
 


Ok kumbe ni moja wapo kati ya vikosi bora vilivyopata kutokea hapa Duniani...kama ni moja wapo hapo sawa.
 
Last edited by a moderator:


Alesandro Nesta akiwa na miaka 36 alipata kutamka kuwa huyo Messi akinipita na kufunga goli basi ntachomolea jezi saa hiyohiyo na kisha ntavua njumu na kuwarushia washabiki na ndio utakuwa mwisho wangu katika ulimwengu wa Soka.
Na mpaka Nesta anastahafu AC Milan alisimamia kiapo chake na bwana Messi hakuweza kufunga.
Sasa hapo ndipo utagundua kuwa hao mabeki anaowakimbizaga wakiwa wanne au watano ni sawa na mabeki wa Kariakoo Lindi au Mji Mpwapwa.

grande Nesta
Forza Milan
 
Angalia data zako vizuri.....
Juventus say emotional farewell to their beloved Alessandro Del Piero | Paolo Bandini | Football | guardian.co.uk

 
Hapa ni sawa comparing Ferrari na Porsche....kwanza Ronaldo ni mchezaji ghali sana duniani akiwa ameuzwa toka man u kwa mkwanja mnyamwezi mil 131....
wote wameshachukua kiatu cha uchezaji bora wa FIFA....

Tukianza na finishing kwa kutumia maguu....Messi ni mkali wa kumalizia hasa kwa guu lake ma mavi na mara nyingi amekuwa akishambulia tokea upande wa kulia nafasi ambayo alianza kuitumia tangu pep achukue timu...mara nyingi messi umaliziaji wake hauna makosa hata chembe na hasa timu ikiwa ina shine naweza kumpa rate ya 9/10..

Lakini wakai messi ni mtumiaji mzuri wa akili analikaribia lango Ronaldo yeye ni mtumiaji wa nguvu sana na ni mmaliziaji mzuri wa guu lake la kulia na kwa matumizi yake ya nguvu amekuwa si mfungaji mmaliziaji mzuri na nampa rate ya 8/10

Umaliziaji kwa kichwa...
Messi yawezekana akawa ni mbovu kinoma noma katika umaziliaji kwa kichwa na mpoja ya magoli yake bora ambayo alibahatisha kumalizia kwa kichwa ni lile la final na man u nampa rate ya 6/10

Ronaldo ni mkali wa vichwa na haogopi kutia kichwa na hufunga kwa kichwa hata kwa umbali mrefu na ukizingatia ni mtumiaji mzuri wa nguvu..nampa 8/10(kumbuka kuna wakali wa vichwa kama patrick kluivet ambao wana rate ya 10/10 na yazidu zidane mwenye rate ya 9/10)

Kwenye free-kicks...
wote ni wakali wamipira mfu messi kama kawaida yake anatumia akili sana kwenye upigaji wa mipira mfu na ana kawaida ya kupiga kwenye nyavu ndogo mfano mzuri angalia el-classico ya juzi....nampa messi 8/10
Ronaldo ni mkali wa powerfull freekicks na amekuwa mkali tangu alipokuwa man u na hata real madrid hapa ronaldo nampa rate ya 9/10

Dribbling na kontrol
Messi ni guru wa ku dribble hapana shaka kwa hili ni mkali wa kukimbia na mpira uku akikatiza kati kati ya misiutu ya mabeki nampa 10/10
Ronaldo ni mkali lakini sio kivileeeee yeye mar nyingi anatumia ile chenga ya tangulia twende na kukimbiza na ana luzi controll sana anapokuwa yupo katika eneo la hatari nampa 9/10


Skills na teknic
Messi ni magic wa skill japo hajamfikia dinho umaarufu wa skills zake ni kwamba huwa zinaleta madhara kwenye timu pinzani nampa 10/10 unlike ronaldo ambae ni show man anapiga skills nyuma ya mstari wa nusu uwanja ambapo haendi popote ni mzuri kumuangalia lakini hana impact kwa timu kwa hizo skills zake...nampa 9/10

team play
messi amnekuwa maarufu hasa akiwa na viungo bora kabisa kwa kipindi hiki xavi na iniesta kombinenga hii huwa ni ya kuogopewa na ndio maana watu wengi wanasema messi si bora kwa sababu anacheza na watu kama hao..nampa 9/10

ronaldo kama kawaida ni selfish anjulikana hivyo na mara nyingi amekuwa hata akipigiwa boo na mashabiki bernabeu nampa 6/10

phsical
messi ni kadogo kadogo hakana nguvu kivilee na kama mnavyojua alizaliwa akiwa njiti..ni mzuri sana ukiwa nae ana kwa ana...ndio maana defenders always wanambwaga chini..nampa 7/10
Ronaldo ni fiziki anaonekana ni mtu anaenyanyua vitu vizito na kula vizuri na inamsaidia kupiga mprikwa kwa mbali nampa 9/10


kitakwimu tangu ronaldo aende real 2009

Messi

2009-10
Games: 64
Goals: 49
Assists: 11

2010-11
Games: 61
Goals: 51
Assists: 22

2011-12
Games: 68
Goals: 74
Assists: 27

Ronaldo

2009-10
Games: 39
Goals: 33
Assists: 7

2010-11
Games: 65
Goals: 56
Assists: 16

2011-12
Games: 73
Goals: 77
Assists: 16



hitimisho
messi ni mkali tena kwa kila game iwe ngumu au laini..messi hakabiki anabadilika badilika anaweza kucheza kati kama namba 8 anaweza kurudi mpaka nyuma anachukua mpira na kusambaza kwa winga na mido wa kati na anaweza pia kukimbia na mpira toka nyuma mpak akafunga..lakini ronaldo ni mkali wa mechi zake..zikija meschi muhimu haonekani....

jumla
messi 69/70
ronaldo 68/70
 
wote wanafunga
ila Messi ana' assist(pasi za mwisho) kuliko Ronaldo

kwa uchoyo na kujisikia ronaldo kamzidi messi
 
Hapa ndipo watu tunapo gongana vichwa Kama ma Bus ya Mikoa yanavyokatisha Njia Kichwa cha Habari kilikuwa Rahisi tu Messi au Ronaldo nani ni Zaidi?

Sasa Sijui kina Del piero wameingia vipi tena Kisa hana Red Card mwisho tutamuongelea na Gary Leniker bure hana Red Card vilevile.

Messi na Ronaldo ndio Ma Artist wa Mpira sasa hivi Messi yeye Hana Zile step Over ambazo C. Ronaldo anazo ila Chambua za Messi ni kiboko labda ufupi wake nao unakuwa Rahisi kupenya mtu kirahisi na ukitizama wachezaji wengi Barca hawajabadilika pengine ndio uwepesi wa kujuana na wenzake au vipi sijui?.

C Ronaldo jamaa ni mchezaji mwenye juhudi sana ila R Madrid haina watu Pengine wa kugongeana zile Pasi anazozihitaji yeye ila Bado ukitizama hayupo mbali na Messi kwahiyo Piga uwa wote wanavipaji zaidi ya wachezaji wengi ambao bado sasa hivi wanaocheza Mpira wa Miguu Duniani ila Messi kamzidi C Ronaldo sio mbali sana kwahiyo kwa Maoni yangu Messi ni zaidi.
 

Nimekugongea LIKE wewe ni mmoja wa washabiki wachache wa Man U aliyesimamia ukweli! Wengi kwa sababu Ronaldo alichezea Man U basi wana tabia ya kusema Ronaldo anajua sana kuliko Messi,wanabisha hao! Ukweli wote ni wachezaji wazuri ila Messi amezidi kidogo wajameni khaa!! ka mwili kadogo mambo makubwa mno!
 


Asante sana Yo yo...
Nimekubaliana na wewe kwa kukIri kwako kuwa Messi hata akiruhusiwa kucheza na mikono hamfikii Dinho the saint
 
mesii the magician .. talent player of his generation that's all ..
mesiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
messi: modest, flamboyant, easy on the eye, unplayable one-on-one, entertaining dribles, down to earth

ronaldo: arrogant, direct play, physical, easier to beat one-on-one, speedier but less entertaining, proud
 
Mimi kwa club za ulaya ni Real Madrid pekee ndio ikifungwa roho inaniuma na sina timu england kabisa,lkn natamka pasi na shaka kuwa Messi ni mzuri kuliko CR japo Barca nawachukia.
 
Messi anakipaji, Ronaldo ana mazoezi.! Hivyo siku zote mwenye kipaji hubaki juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…