Meya Issaya Mwita atoa tamko

Meya Issaya Mwita atoa tamko

Naomba ufafanuzi wa haya.
1. Theluthi mbili ya akidi ya wajumbe wa kumtoa Meya haikufika kikanuni , sasa ni kwa nini kikao kikaendelea?
2. Ni kwa nini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi hajatoa tamko lolote hadi sasa?
2/3 ya wajumbe inatafutwa kwa kura , na ilishindikana kupatikana kwa vile waliopiga kura ya kumkataa meya walikuwa 16 tu badala ya 17 wanaotakiwa kikanuni , kwahiyo ilikuwa lazima kura zipigwe tu ili kujaribu kuona kama wanaweza kupata wanachokitaka .

Lingine unalotakiwa kujua ni kwamba ndani ya awamu ya 5 hakuna waziri yeyote mwenye mamlaka ya kupinga yaliyopangwa na ccm hata kama yatamdhalilisha waziri binafsi , hawa mawaziri wote unaowaona kazi yao ni kujibu maswali bungeni tu , waziri wa wizara zote ni yule aliyewateua .
 
Binafsi Nilikuwa Nahesabu siku tu huyu Meya kwenda CCM sababu alikuwa karibu Nao sana mpaka siku moja akaambiwa unafanya nini huko njoo uunge mkono juhudi sijui walipishana nini mpaka Wameamua kumfanyia uhuni huu hivi akienda mahakama ya jadi Mtamlaumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mayor hajui Sheria
Kwanza aliomba mahakama arudishiwe umeya Ina maana alikuwa anajua kuwa yeye Sio meya.Sasa alisema yeye Ni meya kivipi?

Hiyo akidi ya theluthi mbili Ni ya wajumbe waliohudhuria kikao haihesabu hata wale waliosusa kikao
Akidi ilitimia ya kumwondoa
We endelea kuota tu
 
Mayor Issaya Mwita anaandika...

Na Issaya Mwita.
Mayor wa Jiji la DSM.

Marafiki zangu nawashukuru kwa maombi na dua zenu

Kuna watu wengi hawakumuelewa hakimu kwa maamuzi yake ile jana

Nilifungua kesi 6/01/2020... Siku ya Jumatatu, katika maombi yangu nilimtaka hakimu anipe mambo mawili

1. Kwanza anipe zuio la muda na kwamba mimi Isaya Mwita niendelee kuwa Mayor Mpaka pale mahakama itakaposikiliza kesi yangu ya Msingi

Na nikaieleza mahakama kwamba tayari kuna procedure mbalimbali za kuniondoa katika nafasi yangu

Maombi yangu ya pili ilikuwa ni muda wa kudumu mpaka nitakapoipata haki yangu

Kwa kuwa maombi yangu niliyapeleka kwa hati ya dharura tulipangiwa kusikiliza 8/1/2020.

Tarehe 7 jioni wajumbe wa baraza tulipata barua ya kuitwa kwenye kikao na kwamba kikao kitakuwa 9/01/2020... Alhamisi saa 4 asubuhi ...

Kwa hiyo nikaipeleka barua ile ya wito mahakamani asubuhi ya 8/01 ambayo ndiyo ilikuwa siku ya kusikiliza kesi hiyo ...

Barua ile wa wito haikupokelewa ...kwa mizengwe tuu ...na mawakili wa serikali wakiongozwa na Naibu wa mwanasheria Mkuu ndugu Malata ... wakasema barua hiyo ilipaswa kufailiwa kabla ya samansi kuwafikia

Kesi yetu ikaendelea siku hiyo ya tarehe 8 na tulitegemea kupewa status quo...lakini hakimu hakutoa siku ile ..akapanga Siku ya 9... mchana

Kumbuka kwamba wito wa kikao cha baraza ni saa 4 hiyo hiyo 9/01/2020

Ikanilazimu kuhudhuria baraza siku hiyo ...na kama mlivyosoma kwenye vyombo vya habari .... Marafiki zangu hawa wakapiga kura na kupata 16 votes ...

Ikumbukwe kwamba baraza la jiji la Dar es salaam lina wajumbe 26

Wabunge 5... kila mbunge anaiwakilisha wilaya (Halmashauri)
Mameya 6
Na madiwani 15 ...kila Halmashauri inaleta madiwani watatu watatu ... hivyo basi idadi yetu inakamilika kwa kuwa na wajumbe 26

Sasa marafiki zangu kutafuta 2/3 ya 26 unaweza kuona ni 17.3 ...

Kanuni zetu za kudumu ..Toleo la 1982 kama lilivyotangwa na gazeti la serikali ...

Kanuni 12... unaonesha kwamba ...ili kumuondoa Mayor..2/3 ya wajumbe watasaini ili kupata uhalali wa kuitisha mkutano Maalum wa kumuondoa meya ...Kigezo hicho madiwani walikikidhi

Sasa utata ulikuja pale ambapo ..marafiki zangu hawa walimtegemea yule Diwani aliye wasainia kutotokea kwenye kikao ...wakabaki wamepigwa butwaa... Mara wakafanya maamuzi ya haraka .."Tumsainie jina lake" kweli walifanya hivyo ...mimi na baadhi ya wajumbe tulichelea kuingia ... nilipoingia ndiyo nikagundua jina la Diwani yule limekuwa fojali...

Hapo ndipo kizaa zaa kipoanza

Lakini baadae tulikubaliana tukaendelea tukapiga Kura CCM wakapata 16 na sisi tumebaki na kura 2 tu

Kanuni ya 84 (1) inasema Meya ataondolewa madarakani kwa 2/3 ya wajumbe wa Halimashauri hapo ndipo walipokwama.

Wakaanza maigizo kwamba ni 2/3 ya wajumbe waliohudhuria kikao wakasahau kwamba ni 2/3 ya wajumbe ndiyo iliyoitisha kikao kile

Turudi sasa kwa Maamuzi ya Mahakama ...

Kwangu mimi sioni kama Hakimu amekosea kwani hatukupeleka barua ile kwa muda ...
Hivyo alikuwa sawa kuninyima struts quo ...

Lakini pia maamuzi hayo wangekuwa na maana sana ile siku ya 8/01/2020 au 9/01

Maamuzi ya jana hayana athari yoyote kwangu kwa kuwa tayari kile nilichotaka kukizuia kilishafanyika 9/01/2020 ... na kwamba sasa Azimio la kutaka kuniondoa limekosa uhalali wa kikanuni

Asanteni sana.
Wajumbe nane ambao hawakuhudhuria ni kina nani na ni wa chama gani? Kuna haja ya kuanza kushughulikiana kichama
 
Mayor Issaya Mwita anaandika...

Na Issaya Mwita.
Mayor wa Jiji la DSM.

Marafiki zangu nawashukuru kwa maombi na dua zenu

Kuna watu wengi hawakumuelewa hakimu kwa maamuzi yake ile jana

Nilifungua kesi 6/01/2020... Siku ya Jumatatu, katika maombi yangu nilimtaka hakimu anipe mambo mawili

1. Kwanza anipe zuio la muda na kwamba mimi Isaya Mwita niendelee kuwa Mayor Mpaka pale mahakama itakaposikiliza kesi yangu ya Msingi

Na nikaieleza mahakama kwamba tayari kuna procedure mbalimbali za kuniondoa katika nafasi yangu

Maombi yangu ya pili ilikuwa ni muda wa kudumu mpaka nitakapoipata haki yangu

Kwa kuwa maombi yangu niliyapeleka kwa hati ya dharura tulipangiwa kusikiliza 8/1/2020.

Tarehe 7 jioni wajumbe wa baraza tulipata barua ya kuitwa kwenye kikao na kwamba kikao kitakuwa 9/01/2020... Alhamisi saa 4 asubuhi ...

Kwa hiyo nikaipeleka barua ile ya wito mahakamani asubuhi ya 8/01 ambayo ndiyo ilikuwa siku ya kusikiliza kesi hiyo ...

Barua ile wa wito haikupokelewa ...kwa mizengwe tuu ...na mawakili wa serikali wakiongozwa na Naibu wa mwanasheria Mkuu ndugu Malata ... wakasema barua hiyo ilipaswa kufailiwa kabla ya samansi kuwafikia

Kesi yetu ikaendelea siku hiyo ya tarehe 8 na tulitegemea kupewa status quo...lakini hakimu hakutoa siku ile ..akapanga Siku ya 9... mchana

Kumbuka kwamba wito wa kikao cha baraza ni saa 4 hiyo hiyo 9/01/2020

Ikanilazimu kuhudhuria baraza siku hiyo ...na kama mlivyosoma kwenye vyombo vya habari .... Marafiki zangu hawa wakapiga kura na kupata 16 votes ...

Ikumbukwe kwamba baraza la jiji la Dar es salaam lina wajumbe 26

Wabunge 5... kila mbunge anaiwakilisha wilaya (Halmashauri)
Mameya 6
Na madiwani 15 ...kila Halmashauri inaleta madiwani watatu watatu ... hivyo basi idadi yetu inakamilika kwa kuwa na wajumbe 26

Sasa marafiki zangu kutafuta 2/3 ya 26 unaweza kuona ni 17.3 ...

Kanuni zetu za kudumu ..Toleo la 1982 kama lilivyotangwa na gazeti la serikali ...

Kanuni 12... unaonesha kwamba ...ili kumuondoa Mayor..2/3 ya wajumbe watasaini ili kupata uhalali wa kuitisha mkutano Maalum wa kumuondoa meya ...Kigezo hicho madiwani walikikidhi

Sasa utata ulikuja pale ambapo ..marafiki zangu hawa walimtegemea yule Diwani aliye wasainia kutotokea kwenye kikao ...wakabaki wamepigwa butwaa... Mara wakafanya maamuzi ya haraka .."Tumsainie jina lake" kweli walifanya hivyo ...mimi na baadhi ya wajumbe tulichelea kuingia ... nilipoingia ndiyo nikagundua jina la Diwani yule limekuwa fojali...

Hapo ndipo kizaa zaa kipoanza

Lakini baadae tulikubaliana tukaendelea tukapiga Kura CCM wakapata 16 na sisi tumebaki na kura 2 tu

Kanuni ya 84 (1) inasema Meya ataondolewa madarakani kwa 2/3 ya wajumbe wa Halimashauri hapo ndipo walipokwama.

Wakaanza maigizo kwamba ni 2/3 ya wajumbe waliohudhuria kikao wakasahau kwamba ni 2/3 ya wajumbe ndiyo iliyoitisha kikao kile

Turudi sasa kwa Maamuzi ya Mahakama ...

Kwangu mimi sioni kama Hakimu amekosea kwani hatukupeleka barua ile kwa muda ...
Hivyo alikuwa sawa kuninyima struts quo ...

Lakini pia maamuzi hayo wangekuwa na maana sana ile siku ya 8/01/2020 au 9/01

Maamuzi ya jana hayana athari yoyote kwangu kwa kuwa tayari kile nilichotaka kukizuia kilishafanyika 9/01/2020 ... na kwamba sasa Azimio la kutaka kuniondoa limekosa uhalali wa kikanuni

Asanteni sana.
Wazee wa kugushi hawajaanza leo wala jana. Kihiyo mnamkumbuka?
 
Watanzania tujenge tabia ya kuheshimu sheria na katiba.Utamu wa madaraka ni kuzingatia hayo mawili.Tusijenge taswila kwa vijana wetu kuwa waweza kupata madaraka kwa kuteuliwa bila ya kuchaguliwa,waweza kutoa maamuzi bila kushirikisha wadau wahusika,waweza kuvunja katiba usihojiwe nk
 
Naomba ufafanuzi wa haya.
1. Theluthi mbili ya akidi ya wajumbe wa kumtoa Meya haikufika kikanuni , sasa ni kwa nini kikao kikaendelea?
2. Ni kwa nini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi hajatoa tamko lolote hadi sasa?
Unasubiri waziri wa Ccm atoe tamko juu ya maamuzi ya ovyo ya ccm wenzake? Au hukumsikia waziri mwezi April akikemea maDc kutoingilia fedha za jimbo na waziri huyohuyo akiwa Hai mwezi January mwaka huu akasema mwamuzi wa mwisho fedha za jimbo ni Dc?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na wananchi wamejua hili. Hawamjali aliyetumwa bali aliyemtuma. Na wao kila mwanzo wa kauli zao humtukuza yule aliyewatuma ili kutafuta uhalali na mapambio ya sifa na utukufu ni mengi tu
Unasubiri waziri wa Ccm atoe tamko juu ya maamuzi ya ovyo ya ccm wenzake? Au hukumsikia waziri mwezi April akikemea maDc kutoingilia fedha za jimbo na waziri huyohuyo akiwa Hai mwezi January mwaka huu akasema mwamuzi wa mwisho fedha za jimbo ni Dc?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom