moudgulf
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 142,674
- 743,909
Jamiiforums itabakia kuwa kituo muhimu cha habari, elimu na burudani. Shukrani sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni vyema kusoma thread yote kwa umakini na kuielewa kabla hujakimbilia kupost.Siashakufa huyu au
With much thanks, sisi watu wazima tunaguswa sana na thread constructive kama hizi. Hello nice.View attachment 554780
General Manuel Antonio Norriega
Manuel Antonio Noriega Moreno (Spanish pronunC.I.A.tion: [maˈnwel noˈɾjeɣa]; February 11, 1934 – May 29, 2017) alikua mwanasiasa na mwanajeshi wa nchi ya Panama pia infoma wa C.I.A. wa kipindi kirefu. Alikua mtawala wa kijeshi wa Nchio ya Panama na dikteta 1983 mpaka 1989 wamarekani walipovamia nchi hiyo kijeshi na kumuondoa madarakani.
Alizaliwa jijini Panama na kusoma katika moja ya shule za kijeshi mjini lima na baada ya hapo ya sekondari ya Americans. Baada ya hapo alijiunga na jeshi la Nchi hiyo na kuwa mmoja wa maafisa wa jeshi,alifanya kazi kwa karibu na mkuu wa intelijensia wa jeshi la nchi hiyo na kupanda vyeo ambapo baada ya Omar Torrijo ambaye ndiye aliyekua mkuu wa intelijensia wa jeshi kufanya jaribio la mapinduzi na kushinda alipewa nafasi hiyo mwaka 1968.Baada ya kifo cha torrijo mwaka 1981,Norriega alijiimarisha kiutawala mpaka akawa kiongozi wa panama ingawa sio rasmi mwaka 1983 (de facto ruler of panama). kuanzia mwaka 1950 mpaka karibu na kipindi ambacho Marekani walikuja kumvamia, Norriega alikua akifanya kazi kwa karibu sana na C.I.A. Norriega alikua moja ya vyanzo muhimu vya kuamnika vya C.I.A. kwenye masuala ya intelijensia, pia ilikua ndio sehemu muhimu ya kuanzishia, kupanga pamoja na kupitishia silaha na fedha linapokuja suala la operasheni yoyote inayohusu masuala ya kijeshi marekani ya kati na kusini.
Norriega pia alijihusisha na biashara ya madawa ya kulevyahas cocane kwa kiwango cha hali ya juu kitu ambacho wamarekani walikifahamu fika kwa miaka mingi, ila waliliruhusu suala hilo liendelee kwa sababu za umuhimu wa Norriega kwenye masuala ya kijeshi na kiusalama katika ukanda huo wa marekani ya kati na kusini.
Utawala wa Norriega katika Nchi hiyo uligubikwa na ukandamizwaji wa vyombo vya habari, uimarishwaji wa jeshi, pamoja na uteswaji na ukandamizwaji wa mahasimu wa kisiasa. Noriega aliweza kusimamia uchaguzi wowote na kupata matokeo anayotaka yeye, alijitengenezea utajiri mkubwa kupitia biashara yake ya madawa ya kulevya. Taratibu mahusiano yake na Nchi ya marekani yalianza kupungua kwa sababu ya vitendo hivyo pamoja na kuanza kuuza taarifa za kiintelijensia kwa mahasimu wa marekani. Mwaka 1988 Norriega alibainishwa kwamba ni mmoja wa watu wanaosafirisha madawa ya kulevya katika miji ya Miami Florida. Marekani waliiivamia Panama 1989 na kumuondoa madarakani na kumpeleka marekani kama mfungwa wa kivita.
alisomewa makosa nane yanayohusiana na kuuza madawa ya kulevya kupanga na kusafirisha madawa ya kulevya na utakatishaji wa fedha haramu. Mwaka 1992 alihukumia kifungo cha miaka 40 jela mbapo kilipunguzwa na kuwa miaka 30 jela.
Kifungo cha Norriega nchini marekani kilisitishwa mwaka 2007 baada ya Nchi ya Panama pamoja na Ufaransa kuomba kumuhukumu bila yeye mwenyewe kuwapo mahakamani kwa mauaji mwaka 1995 na utakatishaji wa fedha mwaka 1999. ufaransa ilikabidhiwa mtuhumiwa huyu mwaka 2010 mwezi wa nne baada ya ombi lao kukubaliwa na alifikishwa Paris 27|4|2010 na baada ya kesi yake kusikilizwa upya alihukumiwa kifungo cha miaka saba, mwezi wa saba 2010. Makubaliano ya kumhamisha gereza kutoka Ufaransa na kumpeleka Panama kutumikia kifungo cha miaka 20 yalifikiwa ikiwa ni vifungo vyote vilivyomkabili nchini marekani pamoja na ufaransa hivyo alipelekwa panama 23|09|2011. Norriega alifariki katika hospitali ya Santo Thomas katika jiji la Panama 29|05|2017 miezi miwili baada ya uperation ya ubongo.
MAISHA YA MWANZO NA FAMILIA
Noriega alizaliwa katika jiji la panama,katika familia ya kimasikini ya mestizo au mchanganyiko wa rangi ambayo inajumuisha wazawa wa marekani,waafrica na waspaniola.Mama yake anazungumziwa kuwa mpishi na dobi na baba yake alikua muhasibu na hakuishi muda mrefu na mama yake alifariki kwa maradhi ya kifua kikuu wakati Noriega akiwa mdogo.Noriega alilelewa na bibi yake katika apatimenti ya chumba kimoja katika makazi ya watu wengi holela (slum) za mji wa Terraplen.Waandishi wa habari na wa vitabu wanasema kwamba sio mtoto halali wa Ricaurte Noriega bali ni mtoto wa house boy wao ambaye uinasadikiwa alitembea na mama mwenye nyumba ,houseboy huyo alijulikana kwa jina la Moreno.
Norriega alipata elimu yake ya mwanzo Escuela República de México, na baadae katika shule ya sekondari inayoheshimika sana jijini Panama kwa kuzalisha wanamapinduzi wengi na viongozi wa kisiasa ya Instituto Nacional . Akiwa katika shule hizi alikua naelezewa kama kijana ambaye yuko makini muda wote. Pia anaelezewa kama kijana aliyependa sana kusoma na alikua anavishwa vizuri na mlezi wake.
wakati akiwa Instituto Nacional, alikutana na kaka yake luis ambaye ni nduguyake na alikua mwanaharakati katika shule hiyo ,norriega kabla ya hapo hakuwahi kukutana na ndugu wa kuzaliwa kwa upande wowote sio mama wala baba. Huyu Luis ndiye hasa alimleta Norriega kwenye siasa na kumpeleka kwenye chama cha kijamaa upande wa vijana. Kuna wakati alikua akiishi pamoja na kaka yake. Wakati akiwa katika chama hicho upande wa vijana alishiriki katika maandamano na pia kuandika baadhi ya makala ya kukosoa uwepo wa Mrekani katika Panama.Katika wakati huu ndio inasadikiwa kwamba ndipo wamerekani walimchukua katika kitengo chao cha intelijensia na alikua akitumiaka katika kuwapa taarifa wamarekani za kikundi cha wanaharakati wenzake akiwemo kaka yake. aliendelea kufanya kazi na wamerekani katika sehemu mbalimbali mpakamwaka 1980 na inasadikiwa aliwahi kulipwa kiasi cha usd 10.70 mwaka 1955 ambapo ilikua ni moja ya malipo ya awali ambayo aliendelea kulipwa kwa mda mrefu kwa kutoa taarifa hizo.
Baada ya kumaliza katika shule ya Instituto Nacional alipata scholarship kwenye chuo cha mafunzo ya kijeshi cha Chorrillos Military School kilichopo Nchini Peru mjini Lima kwa kusaidiana na Luis ambaye tayari alikua anafanya kazi katika ubalozi wa panama nchini Peru.Alikua na ndoto zilizoota mbawa za kuwa daktari ila alishindwa kupata nafasi katika chuo kikuu cha Panama. Akiwa nchini peru alitengeneza urafiki na Roberto Díaz Herrera, ambaye baadae alikuja kuwa rafiki wa karibu na muhimu sana.
Norriega baadae alioana na Felicidad Sieiro de Noriega, ambaye walikutana mwaka 1960 na walifanikiwa kupata mabinti watatu ambao ni Lorena, Sandra and Thays Noriega. Siero alikua ni mwalimu wa shule na Norriega alikua mwanajeshi. familia ya mkewe Norriega haikufurahishwa na ndoa hiyo, pamoja na hayo Norriega anaonekana hakuwa na utulivu katika ndoa yao na mara kadhaa mkewe alisikika akitaka ndoa hiyo ivunjwe ingawaje baadae alibadili mawazo na kuendelee na mumewe. wahusika hawa wanne wa familia hii ya Norriega wanaripotiwa kwamba walikuwepo wazima wa afya wakati wa kifo cha Norriega.
ITAENDELEEAAAA
Inaonekana pamoja na mambo yote hayo jamaa alikuwa mtu wa bata sana dah!Alijificha ubalozi wa vatican, wanajeshi wa marekani wakaenda kupiga mziki kwa sauti ya juu sana baada ya siku tano jamaa ikabidi atoke mwenyewe
Asante kiongozi hivi vitu tunajikumbushia tuHabar nzuri umenikumbusha 80s.. 90s.. Hongera Kwa kumbukumbu nzuri..
Sent using Jamii Forums mobile app