Mfahamu Harry Price almaarufu kama The Father of GhostBusters

Mfahamu Harry Price almaarufu kama The Father of GhostBusters

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Habari ya uzima WanaJF; pole kwa wagonjwa na walio na afya muendelee kuwa afya njema zaidi. Kama ilivyo Kawaida yangu kuleta nyuzi au makala za kuongezeana maarifa kwenye mambo mbalimbali. Hivyo leo Naomba nilete kwenu uzi huu unaomhusu mtu maarufu katika taaluma wa kuleta ufafanuzi wa masuala ya kiroho pamoja na mambo ya Giza.

NB: Sina dhamira yoyote ya kumbadilisha mtu Imani yake kwa kile nitakachokiweka humu; na endapo ilitokea hivyo Naomba niombe samahani sana mwanzoni.

IMG_2048.jpg

Tarehe 17 mwezi wa Januari Mwaka 1881, Dunia ilipata nafasi ya kushuhudia uzazi wa Harry Price. Muingereza aliyekuwa na taaluma kadha wa kadha; akiwa ni mtafiti wa masuala ya mizimu pamoja na mizuka ndani ya nyumba mbalimbali za wakazi wa Uingereza. Lakini alikuwa ni mshauri kwenye kesi mbalimbali za masuala hayo.

IMG_2049.jpg

Alipata elimu ya awali katika shule ya Waller Road Infants School Kisha alienda kwenye shule ya Haberdashers' Aske's Hatcham Boys School. Akiwa na Miaka 15 alianzisha kikundi cha Carlton Dramatic Society ambacho kilijihusisha na sanaa za maigizo. Humu Harry akiwa mtoto aliandika visa vingi ikiwemo; Kisa chake cha kushuhudia shughuli za kimangara kwenye Nyumba moja iliyoko Shropshire.

IMG_2041.jpg

Bwana Mkubwa Prive alidai kuwa alianza kuona vivuli vya watu usiku; Vivyo hivyo akiwa amelala aliweza kuona viumbe mbalimbali ambao hakuweza kuwatambua wakizunguka chumbani mwake. Vyote hivi alivishuhudia akiwa na Miaka 15 tu.

IMG_2050.jpg

Alipofikisha Miaka 20 aliona kuna haja ya kuwaumbua wale watu wapigaji, mfano; waongo pamoja na watapeli ambao hutumia picha pamoja na maelezo ya kitapeli ili kujenga hofu kwa jamii. Alitumia nguvu na muda mwingi akifanya utafiti juu ya watapeli hao. Jambo ambalo kiukweli lilizaa matunda na kuanza kupata maadui wengi tu.

IMG_2047.jpg

Ili kulinda taswira yake ilimpasa kubadilisha taarifa za maisha yake mwanzoni pamoja na za familia yake. Alidai kuwa alikuwa ni mtoto wa familia ya kitajiri kutoka Shropshire Ingawa taarifa sahihi ni kuwa New Cross kwenye familia ya Baba aliyekuwa akiuza karatasi kwa ajili ya barua.

IMG_2043.jpg

Mwaka 1925 Price alifungua maabara maalumu Kwa ajili ya kufanya utafiti wa kina kuhusu kesi zote zinazotolewa na watu kuhusu masuala ya kiimani. Lakini marafiki zake waliokuwa ni wapigaji wa pesa kupitia uongo au utapeli kwa watu katika matamasha au maonesho. Hivyo walibadilika na kuwa maadui zake mpaka kufa kwake. Huyu Bwana ilikuwa ni ngumu sana kumuamini mtu tu kwa sababu eti ametokewa na kitu au amesikia sauti ya ajabu. Mpaka afanye udadisi wa kina.

IMG_2044.jpg

Price alifanyia utafiti tuhuma zote kwa usawa na kama ilikuwa na ukweli basi alionesha kuwa Ina ukweli Ingawa tuhuma nyingi hazikuwa na ukweli na zilikuwa na malengo ya upigaji wa pesa tu na umaarufu.

Mwaka 1920 Bwana Mkubwa Harry Price alijiunga na Chama cha Utafiti wa Masuala yenye Utata (Society for Psychical Research) na alitumia ujuzi wake wa mazingaombwe kuwaumbua watu waongo na watapeli.

IMG_2046.jpg


Alikuwa mwanachama wa vyema vingi tu mfano; Magic Circle, National Laboratory of Psychical Research, American Society for Psychical Research, University of London Council for Psychical Investigation pamoja na The Ghost Club.

IMG_2052.jpg

Tarehe 29 Machi 1948 Price alipatwa na shambulio la ghafla la moyo na kufariki nyumbani kwake huko Pulborough, Magharibi mwa Sussex akiwa na Miaka 67.

Makala zake pamoja na tafiti zake zilihamishiwa kwenda kwenye chuo kikuu cha Londo kati ya mwaka 1976 na 1977 na Mjane wa Harry Price.

IMG_2040.jpg


Mpaka anafariki alikuwa amesaidia watu wengi sana na kujipatia maadui wengi ambao aliwaumbua.​

IMG_2051.jpg

Nasaha kubwa pamoja na Imani ya Bwana Harry Price ni kuwa sio kila tukio linamahusiano na upande wa Pili yaani mashetani, mapepo au roho chafu hivyo inapaswa mtu kuwa makini na ikiwezekana fanya utafiti na udadisi wa kina.

IMG_2039.jpg

Moja kati ya picha bandia iliyofanyiwa utafiti na Harry Price.
IMG_2040.jpg
Naomba niishie Hapo wanajukwaa. Mpaka Wakati Mwingine tena.
Asante sana @Mshana Jr @Lumumba @Madame B na wengine.
 
ungetoa mfano wa tukio moja alilolifanyia kazi

Mwaka 1926
Bwana Harry Price aliitwa kwenda kufanya utafiti nchini Italia Vienna ikiwa ni Mwezi wa Aprili mwaka 1926. Alisikia shuhuda kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu tukio la mtoto wa kike mmoja aliyesadikika kuwa amepanda mashetani.
Alipata kuona vithibitisho kadhaa wa kadha mfano: Kutoa sauti zisizo za kawaida, pamoja na macho kubadilika rangi na kuwa meupe na Wakati Mwingine kuwa rangi nyekundu.
Alisafiri na familia hii yote mpaka Uingereza ili kuona vithibitisho zaidi. Hii ni Moja kati ya kesi iliyompa umaarufu Kwani mwanzoni alikataa na kutoa ushahidi katika kesi za wapiga dili tu matapeli.
Mtoto huyu wa kike akipandwa na mashetani hayo aliweza kuhamisha vitu mfano viti & meza na pamoja na kutoa hata damu huku akitoa vicheko vya kutisha.
IMG_2056.jpg

IMG_2057.jpg
 
Harry Price kwa ufupi alikhwa ni mtafiti wa masuala ya kiroho hususani matukio ya mizimu, roho chafu pamoja Na matukio ya kutisha.
Huyu Bwana Mkubwa alikuwa anachallenge matukio pamoja na watu waliokuwa wanazusha matukio ili kupata umaarufu.
Huyu ndo Bwana Mkubwa wa kwanza kuanza kutumia maabara kwa ajili ya kuchunguza picha ili kuleta suluhu kwenye matukio mbalimbali ndani ya Uingereza na sehemu zingine.
Nipo [emoji120]
 
Sijaona alichofanikiwa hadi hapa sojaokota lolote
 
Back
Top Bottom