snowhite
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 18,065
- 24,559
saaawa unapenda historia na unachapisha vitabu vya Sykes na nn sijui.Dira...
Nigependa kueleza kidogo kuhusu kuwa mimi nimespecialise chembelecho ''ishu'' ya familia ya Sykes na Uislam.
Tuanze na ukoo wa Sykes.
Waandishi wa historia ya Tanganyika walitishwa na vitu vitu viwili navyo ni Sykes kutawala harakati za Waafrika katika kupigania haki za Waafrika kuanzia mwaka wa 1929 hadi ulipopatikana uhuru 1961.
Mwaka wa 1929 historia hii inaanza na baba, Kleist Sykes hadi alipofariki 1949.
1950 hadi 1961 harakati hizi zinapokelewa na wanae Abdul, Ally na Abbas.
Ukoo huu ulikuwa na ushawishi mkubwa katika AA, TAA na TANU na pia katika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika chama alichoanzisha baba yao 1933 pamoja na wenzake kama Ali Jumbe Kiro na Mzee bin Sudi kwa kuwataja wachache.
Hii Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilianzishwa na viongozi wale wale ambao walikuwa wanaongoza AA katika miaka hiyo.
Hii ndiyo sababu huwezi kuuondoa Uislam katika harakati za kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hiki ndicho chanzo cha tatizo linalotaabisha wengi wenu.
Mnataka kuifuta historia hii na mumpachike Julius Nyerere awe ndiye muasisi wa TANU na kuwa kapigania uhuru wa Tanganyika peke yake akiwa hana ofisi, hana watu wala hana fedha.
Kafika Dar es Salaam kafungua ofisi kajulikana na watu na wa watu wakamuunga mkono na akawa anajaza watu katika mikutano ya TANU Mnazi Mmoja bila ya msaada wa mtu yeyote.
Mimi nimesahihisha haya kwa kuzipitia Nyaraka za Sykes na nyaraka hizi zikanipa historia yote kama ilivyokuwa.
Ikiwa kuandika haya kwako ni ''specialisation'' ya Sykes ningependa kukukumbusha kuwa umesahau kuwaongeza wale ambao ''specialisation,'' yao ni Julius Nyerere peke yake.
Nakuomba uwaongeze hawa katika orodha yako kwani hawa wamebobea kwa miaka mingi katika kazi hii iliyowaondosha wazalendo wengi katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika wakabakia na Nyerere peke yake.
Hawa hawaruhusu mzalendo yeyote atajwe katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Lakini mimi sikuspecialise kwa Sykes peke yake.
Nimewarejesha katika historia wazalendo wengi wakawa ''speciality'' zangu : Chief David Kidaha Makwaia, Dr. Vedasto Kyaruzi, Dr. Michael Lugazia, Dr. Luciano Tsere, Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Wilbard Mwanjisi, Japhet Kirilo, Dome Okochi Budohi, Denis Phombeah, Zuberi Mtemvu, Mshume Kiyate, Joseph Kimalando, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Mohamed Yusuf Badi, Sheikh Abdallah Rashid Sembe, Hamisi Kheri, Sheikh Said Chaurembo, Mshume Kiyate, Sheikh Mohamed Ramiyya, Iddi Faiz Mafungo, Iddi Tosiri, Amina Kinabo, Hawa bint Maftah, Nyange bint Chande, Mama Bint Mwalimu, Halima Selengia, Zarula bint Abdulrahman, Chiku bint Said Kisusa Abdulrahman wengi, wengi, wengi sana.
Wake kwa waume nimeandika historia zao katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Sikumwandika Abdulwahid Kleist Sykes peke yake.
Kitabu chake kipo sasa tunakwenda chapa ya tano na hapa JF tunakijadili kitabu sasa takriban miaka 10.
View attachment 2186656
View attachment 2186658
Sasa ndo ukaona ulete haya maelezo kwenye uzi huu!
ungeshukuru tu kwa kuwa acknowledged jamani!
ahahhahahhaa dah!