fullcup
JF-Expert Member
- Jun 21, 2016
- 809
- 2,204
Huyu jamaa stori zake hazifanani sana na akina Jombi ambao walikuwa wakitikisa Mbeya Mjini maana yeye alijikita porini. Alikuwa akifanya uwindaji haramu katika hifadhi ya Ruaha upande wa Mbarali akitokea kata Moja inaitwa Madibira.
Huyu jamaa na wasaidizi wake walikuwa wakinyoa para (zungu) wakati wakiingia hifadhi na ilikuwa ni lazima kunyoa tena iwapo zitaota kabla hawajatoka. Huyu jamaa wakati akitafutwa na askari alikuwa hapatikani kirahisi. Alikuwa na uwezo wa kujibadilisha Maumbo mbalimbali kwa kutumia madawa Kama vile kuwa mwanamke, kichuguu, nyati, Mzee na wakati mwingine jiwe.
Inasemekana aliua askari wengi sana miaka hiyo. Alikuwa anafanya shughuli za ujangili kwa kujiamini sana mpaka wajomba wakawa wanamuogopa. Mara ya mwisho alikuta ujumbe nyumbani kuwa anaombwa na Rais awasaidie askari pori kuimarisha ulinzi kutokana yeye kuyafahamu maeneo mengi ya hifadhi na maficho ya majangili kwa malipo makubwa.
Akakubali na kuanza kuwa sehemu ya askari pori na akilipwa hela ndefu. Kumbe ulikuwa mtego, inasadikika wakati wa kuchoma sindano za kujikinga na magonjwa gani sijui malaria yeye walimpiga sumu hakumaliza miaka miwili wakala wali maharage na arobaini ikawa ndio mwisho wake.
Huyu jamaa na wasaidizi wake walikuwa wakinyoa para (zungu) wakati wakiingia hifadhi na ilikuwa ni lazima kunyoa tena iwapo zitaota kabla hawajatoka. Huyu jamaa wakati akitafutwa na askari alikuwa hapatikani kirahisi. Alikuwa na uwezo wa kujibadilisha Maumbo mbalimbali kwa kutumia madawa Kama vile kuwa mwanamke, kichuguu, nyati, Mzee na wakati mwingine jiwe.
Inasemekana aliua askari wengi sana miaka hiyo. Alikuwa anafanya shughuli za ujangili kwa kujiamini sana mpaka wajomba wakawa wanamuogopa. Mara ya mwisho alikuta ujumbe nyumbani kuwa anaombwa na Rais awasaidie askari pori kuimarisha ulinzi kutokana yeye kuyafahamu maeneo mengi ya hifadhi na maficho ya majangili kwa malipo makubwa.
Akakubali na kuanza kuwa sehemu ya askari pori na akilipwa hela ndefu. Kumbe ulikuwa mtego, inasadikika wakati wa kuchoma sindano za kujikinga na magonjwa gani sijui malaria yeye walimpiga sumu hakumaliza miaka miwili wakala wali maharage na arobaini ikawa ndio mwisho wake.