Mfahamu Mteja anayefaa kupotezwa

Mfahamu Mteja anayefaa kupotezwa

tzhosts

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2016
Posts
403
Reaction score
510
Katika ulimwengu wa biashara,kuna aina mbili za wateja

Kuna wateja ambao ni LOYAL na wateja ambao ni ROYAL mteja ambaye hayuko katika kundi moja katia ya hili basi sio mteja.

Mteja ROYAL ni mteja yoyote yule ambaye ananunua kwako kwa mara ya kwanza au mara kwa mara-Ndio maana kuna msemo mteja ni mfalme.Mteja wa pili ni yule ambaye ananunua kwako mara kwa mara yaani ni loyal kwako.

Sasa hawa wateja wawili ndio wa muhimu sana kwenye biashara yako na ukiwapoteza hao basi utawapoteza wateja wengi zaidi.

Hata hivo kuna wateja wengine ambao bado sijawapa jina ila wanakua na tabia ya kuja dukani kwako na kukuelekeza namna ya kufanya biashara yako kwa maslahi yao.Mfano(Mteja anakwambia mbona kwa fulani tunauziwa bei hii?)Kama anauziwa bei hio si aende akanunue huko?Aina hii ya mteja ikiwezekana usimuuzie kabisa huduma au bidhaa yako.Ukimuonea huruma sana Mwambie Nenda kanunue Pale kwa bei ya chini uje uniuzie mimi.Akija na mzigo wake mwambie peleka kwako ukatumie wote.

Kwa nini nasema huyu ni mteja wa kupotezwa na kupotezewa?Ni kwa sababu yeye anataka kukufundisha wewe jinsi ya kufanya biashara yako bila kujali maslahi yako.Unapofanya biashara,una malengo na unaelewa ni nini unataka kupata,Mtu anapokupangia BEI anakosa adabu.Kupangiwa bei ni tofauti na kuomba discount-Mteja anaeomba discount sio sawa na anayekupangia bei.

Kila heri
 
?Aina hii ya mteja ikiwezekana usimuuzie kabisa huduma au bidhaa yako.Ukimuonea huruma sana Mwambie Nenda kanunue Pale kwa bei ya chini uje uniuzie mimi.Akija na mzigo wake mwambie peleka kwako ukatumie wote.
Safi sana.
 
Katika ulimwengu wa biashara,kuna aina mbili za wateja

Kuna wateja ambao ni LOYAL na wateja ambao ni ROYAL mteja ambaye hayuko katika kundi moja katia ya hili basi sio mteja.

Mteja ROYAL ni mteja yoyote yule ambaye ananunua kwako kwa mara ya kwanza au mara kwa mara-Ndio maana kuna msemo mteja ni mfalme.Mteja wa pili ni yule ambaye ananunua kwako mara kwa mara yaani ni loyal kwako.

Sasa hawa wateja wawili ndio wa muhimu sana kwenye biashara yako na ukiwapoteza hao basi utawapoteza wateja wengi zaidi.

Hata hivo kuna wateja wengine ambao bado sijawapa jina ila wanakua na tabia ya kuja dukani kwako na kukuelekeza namna ya kufanya biashara yako kwa maslahi yao.Mfano(Mteja anakwambia mbona kwa fulani tunauziwa bei hii?)Kama anauziwa bei hio si aende akanunue huko?Aina hii ya mteja ikiwezekana usimuuzie kabisa huduma au bidhaa yako.Ukimuonea huruma sana Mwambie Nenda kanunue Pale kwa bei ya chini uje uniuzie mimi.Akija na mzigo wake mwambie peleka kwako ukatumie wote.

Kwa nini nasema huyu ni mteja wa kupotezwa na kupotezewa?Ni kwa sababu yeye anataka kukufundisha wewe jinsi ya kufanya biashara yako bila kujali maslahi yako.Unapofanya biashara,una malengo na unaelewa ni nini unataka kupata,Mtu anapokupangia BEI anakosa adabu.Kupangiwa bei ni tofauti na kuomba discount-Mteja anaeomba discount sio sawa na anayekupangia bei.

Kila heri
Duh nakuunga mkono kabisa! Hawa wanaopanga bei wanazingua sana.
 
Biashara inahitaji uvumilivu,ukiwa na hasira unaweza kupoteza wateja wengi; mteja anayekupangia bei jaribu kumuelewesha kwanini bei ya bidhaa au huduma yako ni tofauti na sehemu nyingine, unaweza kutumia pointi za ubora n.k. Cha muhimu jitahidi kumu-win mteja yeyote anayekuja kwako
 
Biashara inahitaji uvumilivu,ukiwa na hasira unaweza kupoteza wateja wengi; mteja anayekupangia bei jaribu kumuelewesha kwanini bei ya bidhaa au huduma yako ni tofauti na sehemu nyingine, unaweza kutumia pointi za ubora n.k. Cha muhimu jitahidi kumu-win mteja yeyote anayekuja kwako
Mkuu,
Kuna wateja wa kueleweshwa na wakija unawaelewesha ila kuna wapanga BEI.Huwa wanaanza na "MBONA" fulani anatuuzia bei flani?Akianza hivo ndugu yangu huyu ni chuma ulete.Mteja wa kueleweshwa atakuuliza kwa nini?huku analipa hatakutajia bei ya mshindani wako mpaka aone kuna ulazima.
 
Mkuu,
Kuna wateja wa kueleweshwa na wakija unawaelewesha ila kuna wapanga BEI.Huwa wanaanza na "MBONA" fulani anatuuzia bei flani?Akianza hivo ndugu yangu huyu ni chuma ulete.Mteja wa kueleweshwa atakuuliza kwa nini?huku analipa hatakutajia bei ya mshindani wako mpaka aone kuna ulazima.
Ni kweli wanaudhi,ila wanamna hiyo unaweza kumjibu, inategememea na anapochukulia mzigo,yawezekana huko alipochukulia hatozwi kodi n.k ndio maana bei yake iko chini
 
Ni kweli wanaudhi,ila wanamna hiyo unaweza kumjibu, inategememea na anapochukulia mzigo,yawezekana huko alipochukulia hatozwi kodi n.k ndio maana bei yake iko chini
Mkuu umewahi kutana na mteja wa aina hii?Huwa wanakuwa na tabia ya kutaka kukufanya wewe ama ujisikie vibaya,ujione mwizi,uone aibu.Huwa sio hao unaoelezea wewe wa kuambiwa kuwa kuna sehemu sijui hawalioi kodi.
 
Mkuu biashara kwako itakuwa ngumu ukiwa namna hiyo, mteja hata aje kwa gia gani lazima ujue namna bora ya kum win.

Akijifanya mjuaji na wewe ukashupaza shingo baishara haita songa mbele. Hakikisha unamu win tu.
Usiweke kisirani na mteja.
 
Mkuu biashara kwako itakuwa ngumu ukiwa namna hiyo, mteja hata aje kwa gia gani lazima ujue namna bora ya kum win.

Akijifanya mjuaji na wewe ukashupaza shingo baishara haita songa mbele. Hakikisha unamu win tu.
Usiweke kisirani na mteja.
Mimi isemi uwe na kisirani,Nasema hivi kwamba kuna aina ya wateja ambaohawaheshimu biashara ya mtu.Wanfikiri maslahi yao tu.Na mbaya zaidi wanakufanya wewe huijui biashara yako.Hao sio wateja wa kutumia nguvu kumshawishi
 
Mimi isemi uwe na kisirani,Nasema hivi kwamba kuna aina ya wateja ambaohawaheshimu biashara ya mtu.Wanfikiri maslahi yao tu.Na mbaya zaidi wanakufanya wewe huijui biashara yako.Hao sio wateja wa kutumia nguvu kumshawishi
Nilikuelewa vizuri tu, ujue kuna wateja ambao wana taarifa ambazo sio sahihi juu ya bidhaa fulani, so, akija na 'kukupangia bei' wewe ndo muda wako wa kumuelimisha na kumpa taarifa sahihi huenda akaja kuwa mteja wako wa kudumu hadi ukashangaa.

Na ujitahidi usimjibu yale majibu meusi, maana huenda kuna wateja wengine wakakusikia unavyomjibu huyo mteja mwenzao na ikawa ni mwanzo wa kukuhama.

Vinginevyo biashara itakuwa ngumu sana kwako mkuu.
 
Wabongo bwana!! Mtu anajifanya hana shida ya wateja wakati ndio wanaomuweka mjini.
Mkuu; Biashara ina Utaratibu wake (Maadili ya kuzingatia) mfano akija mtu ktk eneo la Biashara yako, jiridhishe kwanza je ni Mteja kweli au amekuja hapo kwako kuwa ni kijiweni? Pili chukua tahadhari isijekuwa ni Mwizi au mtu anaetafuta Udhaifu wako ktk biashara yako.Aina hii ya Wateja/Watu - utakuta anachukua muda mrefu sana kupata Bidhaa/Huduma na hata kama ameshahudumiwa bado ataendelea kuwepo hapo na vijihadithi viiingi(Umbea) yaani anaweka kiwingu hapo ktk Biashara yako.
Wewe ukishatambua kwamba mtu huyo yuko nusunusu Mteja sio Mteja ni heri ukampotezea mazima kwani iko siku atasababisha shida hapo kwako mfano Ugomvi, kufukuza wateja kwa Tabia yake/maneno yake n.k. Kwa kifupi HUYO Hakuweki Mjini bali anakufukuza. Mteja gani anafanya kijiwe kwenye Biashara yako kazi ni kuazima simu yako au za wengine atume msg au anaomba anunuliwe soda au anatoa habari za fulani iko hv na hv n.k.?
Naunga mkono hoja ya SUKAH na Ushauri aliotoa.
 
Wabongo bwana!! Mtu anajifanya hana shida ya wateja wakati ndio wanaomuweka mjini.
Mpaka najiuliza wenzetu wanafanya biashara za aina gani mbona kama hawabembelezi wateja kabisa?

Mteja kukupangia bei tu au kusema mbona kwa fulani wanauza hivi ndio yamtoke hayo yote! Labda kama mteja amekwapua bidhaa na kukimbia nayo hivi hivi mteja kwangu ni mfalme daima. Nipo kwa hili game kwa miaka takribani 10 sasa kumjibu mteja jambo ambalo halijakaa sawa hapana kwa kweli.
 
Mpaka najiuliza wenzetu wanafanya biashara za aina gani mbona kama hawabembelezi wateja kabisa?

Mteja kukupangia bei tu au kusema mbona kwa fulani wanauza hivi ndio yamtoke hayo yote! Labda kama mteja amekwapua bidhaa na kukimbia nayo hivi hivi mteja kwangu ni mfalme daima. Nipo kwa hili game kwa miaka takribani 10 sasa kumjibu mteja jambo ambalo halijakaa sawa hapana kwa kweli.
Wenzetu wana loyal na royal wateja, hawahitaji wengine.
 
Mpaka najiuliza wenzetu wanafanya biashara za aina gani mbona kama hawabembelezi wateja kabisa?

Mteja kukupangia bei tu au kusema mbona kwa fulani wanauza hivi ndio yamtoke hayo yote! Labda kama mteja amekwapua bidhaa na kukimbia nayo hivi hivi mteja kwangu ni mfalme daima. Nipo kwa hili game kwa miaka takribani 10 sasa kumjibu mteja jambo ambalo halijakaa sawa hapana kwa kweli.
Pamoja na kuwa mteja mfalme asivuke mipaka. Kuna wateja kama alivyosema mtoa mada wanataka hadi wakupangie jinsi gani uendeshe biashara yako, unaweza kumpa sababu zote hizo kwanini unauza bei hii au unauza brand hii na sio ile yeye akang'ang'ania msimamo wake kuwa fulani anauza hivi wewe bei zako kubwa (yaani mpigaji) ndio majibu kama hayo yanakuja, kuwa kifupi siwezi kubeat bei ya huyo kiroho safi kachukue kwa huyo na mara nyingi wateja hao huwa wanaishia kununua kwako kwasababu unakuta hata huko anakosema wanauza bei ndogo si kweli anakutikisa tu au wanauza vitu vya kiwango cha chini na anajua.
 
Kauli ya MTEJA NI MFALME inatumika vibaya sana sana sana.

Huwa sihudumii mteja mwenye mashaka na bidhaa/huduma yangu

hata wafanyakazi wangu nimeshawambia,mteja mwenye madharau (asihudumiwe)

Anakuja mwenyewe kwa miguu yake unamkaribisha kama mfalme,anakwambia nipe

kitu flani ORIGINAL unamtolea product original, kwenye BEI anakutajia bei ya Product feki

unamwambia kwa upole na ustarabu HAPANA hiki hakiuzwi bei hii ORIGINAL hamna inayouzwa

chini ya kiasi flani,Anakupandia juuu kama kalamba pilipili na madharau juu OOOh wapiiii hiii bei ni hiii

hiii nanunuaga pale original kwa bei hiii,Huwa mteja wa namna hiyo siongei nae TENA nachukua ile

bidhaa niliyomuonyesha nairudsha nilipoitoa,kisha nakaa chini namuangalia.. Mteja wa namna hiii

Hata aseme nimpe ile ile product kwa bei mara 3 ya niliyomtajia Mwanzo, SIMUUZIIIIII TENA yani akanunue anaponunuaga.

Nimemaliza! ipo hivyo kwangu na kila mtu anaefanya kazi na mimi namfundisha namna yakuwahudumia wateja wanamna hiyo.
 
Fanya kila unachojiskia ila usidharau huduma ninayotoa

usidharau wafanyakazi wangu, kuna wateja kisa namba yangu ya simu ipo kweupe

anaipiga unapokea anaanza kukulalamikia kuhusu mfanyakazi,Huwa nawambiaga

Malizaneni wenyewe kama mmeshindwana ONDOKA ila mimi siwezi ku comment chochote

kwenye hiyo case yenu maana sikuwepo wakati mnaanza hadi mlipofikia,ktk vitu sipendi ni

aina hiyo ya wateja wanaodharau wafanyakazi wangu,yani unanipgia simu ili iweje? nimgombeze

huyo mfanyakazi au nimfukuze kazi au nimfanyaje? Uliemkuta ofisini ndio BOSS ni mtu mzima ana akili timamu hawezi kukuvunjia heshima kama hujamvunjia heshima, Wateja wanaojiona wna mamlaka kila mahali Swapendi asee...
 
Pesa ya mteja ni ya thamani sana lakini pia Bidhaa ya muuzaji ni ya thamani sana.

Wateja wengi hufikiri pesa yao ina thamani kuliko bidhaa wanayoinunua na katka

wateja huwa napenda nikutane nao ni hawa wanaodhani pesa yao ina thamani kuliko huduma/bidhaa yangu.

Maana Wanapataga somo la Juzi Jana na Leo na hawarudiagi tena na uhakika si kwangu tu ila naamini hata huko watapoenda.
 
Back
Top Bottom