chama mpangala
JF-Expert Member
- Sep 3, 2015
- 549
- 841
Mwaka 1993 MIIKKA ALEKSANTERI KARI akiwa anaipambania elimu yake ya chuo kikuu
.
Ndipo anapewa Information kuwa anapaswa kuja nchini TANZANIA haraka iwezekanavyo.
Taarifa ile ilimtaka MIIKKA kuwasiri TANZANIA akiwa na watu kadhaa Walifika TANZANIA na hapo wakapokelewa na mtu aliyejitambulisha kama Captain JOHN KOMBA.
Captain JOHN KOMBA aliwachukua kina MIIKKA moja kwa moja mpaka nyumbani.
Kisha walivyofika hapo MIIKKA akaambiwa
"kuanzia sasa utakuwa unaishi hapa"
MIIKKA akaanza kuishi hapo, lakini siku kadhaa mbele akapelekwa mpaka Tanzania one theatre, ndio hiyo band ya music mnaiita "TOT"
Kwa kuwa MIIKKA alikuwa na utaalamu wa vifaa vya music hapo akatakiwa kufanya kazi fulani zinazohusiana na music.. Akiwa hapo TOT akaweka urafiki wa siku kadhaa na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la KENNY.
KENNY ni shabiki wa music wa kofokafoka, hivyo hakupaswa kuambatana naye kwakuwa hiyo si kazi iliyomleta, ila MIIKKA aliweka urafiki wa siri.
Lakini hata hivyo MIIKKA hakujua kuwa. Kazi hiyo ikiisha anapaswa kurudi nchini kwao FINLAND mara moja.
Baada ya kazi hiyo kuisha, MIIKKA alifanya kama maagizo yalivyo mtaka..
Naam! MIIKKA alirudi nchini kwao FINLAND, ila akiwa FINLAND ndipo. Anasikia anapaswa kuambatana tena na watu kadhaa mpaka nchini ZAMBIA, huko kuna documentary fulani wanapaswa kwenda kufanya.
Safari hiyo ikaanza mara moja Ila wakiwa njiani MIIKKA akabadirisha usafiri na kuchukua usafiri ambao ulimleta mpaka nchini TANZANIA. Alipofikia TANZANIA akamtafuta KENNY,
KENNY akampokea MIIKKA, Kisha akamtambulisha kwa rafiki yake aliyeitwa TONY..
hivyo awamu hii tunaweza kusema wenyeji wa MIIKKA walikuwa ni KENNY na TONY.
MIIKKA akaanza kuonyeshwa chocho za jiji la DAR ES SALAAM lakini. hata hivyo maisha ya getogeto hayakuwa poa sana, pesa ilikata day after day.
MIIKKA akawaza nini cha kufanya, ndipo akamshitua TONY kuwa yeye anaweza ku-produce music.
Yaani kama wakipata sehemu basi wanaweza kutengeneza kipato cha kujikimu..
TONY akaamua kumpeleka. MIIKKA moja kwa moja mpaka zilipo studios za MJ RECORD,
TONY akawaambia wale majamaa aliowakuta pale MJ RECORD kuwa..
Oyaa huyu mtu ni nomaa anaweza ku-produce music mbaya, mchukueni.
Wale majamaa wakasema mpaka wafikishe ujumbe kwa bosi. wao ambaye ni MASTER J.
Hivyo TONY na MIIKKA waliombwa kuondoka, kwamba ujumbe wao ungefikishwa kwa bosi na wangejibiwa siku kadhaa mbele.
Lakini masiku yakasonga bila majibu yoyote.
TONY na MIIKKA wakaona ukimiya nao ni jibu, ndipo TONY alipoamua. Kumpeleka MIIKKA kwa bosi mwingine..
Bosi huyo ambaye alikuwa akimiliki Studios za FM RECORD baada ya kumuona MIIKKA akavutiwa naye na kumpa kazi moja kwa moja... Hapo ndipo historia ya music inapoanza kuandikwa na MIIKKA
MIIKKA akafanya kazi na watu kama
Dully Sykes- julieta
Solid Ground Family-Athumani Mlevi
Zahrani Ft Complex-Tupa Mawe.
Kisha akafanya albam nzima ya saida karoli iitwayo maria salome
lakini hata hivyo. Mwaka 2002 MIIKKA akafanya kazi na msanii MAD ICE wimbo ukaitwa Baby Gal.
Wimbo huu ulivuma mnoo
Moja ya vitu ambavyo MIIKKA alikuwa akivifanya mara zote, akiwa anatengeneza mdundo nikuacha instruments zishike nafasi na beat itembee. Umaarufu wa MIIKKA uliongezeka Na hapo akaanza kujiita MIIKKA MWAMBA..
Yaani majina yake halisi ni MIIKKA ALEKSANTERI KARI, hivyo alibadili jina lake la mwisho ambalo ni KARI liwe kwa Kiswahili na tafsiri yake ni MWAMBA, that's why akajiita MIIKKA MWAMBA.. MIIKKA akaanza kuzungumzwa na kutajwa kama producer chipukizi na hatari kwa ukanda wa East African.
Jambo lililofanya mtu mzima ZIGGY DEE avutike kutoka nchini UGANDA na kuja kufanya naye wimbo ulioitwa ENO MAIKI... Kama huujui wimbo huo wa ZIGGY DEE perhaps unapaswa kutazama vizuri line ya umri wako.
Huu ni wimbo uliamsha hisia za watu, miaka hiyo ulibamba mbaya kwenye makumbi ya starehe club🙌🏻
Na kumfanya MIKKA kuzidi kuzungumzwa kama producer anayekuja kwa kasi
Jambo hili likafanya Wasanii wengi waliokuwa wanajitafuta kwenye game, wamuibukie MIIKKA pale FM RECORD na kuomba kufanya kazi naye.
Alipendwa na wengi, sababu MIIKKA alikua mpole na muelewa lakini pia ni producer aliyempa muda mwanamuziki.
Likewise kwa D KNOB. Wakati ambao D KNOB anajitafuta, akaibukia kwa MIIKKA akamsumbua sana pale, brother najua brother najua.
Basi MIIKKA akaamua kutengeneza beat na kumpa D KNOB ili aifanyie mazoezi.
Kisha MIIKKA akapata safari, akarudi nchini kwao FINLAND. Huku nyuma D KNOB akawa na kazi ya kuandika mistari na kufuta..
Katika uandishi wake wote huo wa kufuta-futa akasahau kuweka chorus.
MIIKKA alivyorudi tu TANZANIA D KNOB akawa wa kwanza kufika studio brother tayari nimemaliza..
MIIKKA akachukua. beat ileile ya D KNOB na kumwambia aimbe ili amsikie..
D KNOB si ndio akaanza kuflow sasa, MIIKKA akashangazwa na alichokisikia na kubaki anacheka..
Unujua alicheka nini, alicheka baada ya kusikia wimbo hauna chorus.
Miaka hiyo ilikuwa ni kitu cha ajabu sana..🙌🏻. Lakini MIIKKA akamshauri D KNOB wajaribu kuweka chorus mwanzo wa nyimbo na mwisho wa nyimbo..
Na baada ya wimbo ule kuachiwa ukawa ni habari nyingine, jambo ambalo hawakulitegemea... MIIKKA akawa gumzo, jambo lililofanya studios tofauti za bongo kutamani kufanya kazi naye..
MIIKKA alikuwa na uwezo wa ajabu wa kutumia instrumental moja ndani ya beat nyingi tofauti.
Na bado instrumental ikaendelea kuleta radha tofauti. Mfano kwenye beat ya wimbo wa MAD ICE Uitwao baby gal. Mule ndani kuna instrumental fulani inafanana na malimba.... Likewise ukija kwenye wimbo wa D KNOB Uitwao Elimu mtaani. Mule ndani kuna instrumental inayofanana na malimba.... Kama hiyo haitoshi ukisikiliza wimbo wa saida karoli uitwao mapenzi kizunguzungu, Mule ndani kuna instrumental inayofanana na malimba...
Lakini ukisikiliza hizi nyimbo zote kila wimbo unakupa radha tofauti🙌🏻
Itoshe kusema MIIKKA alikuwa mwamba kweli..
Aishi sana popote alipo🙏🏼.
.
Ndipo anapewa Information kuwa anapaswa kuja nchini TANZANIA haraka iwezekanavyo.
Taarifa ile ilimtaka MIIKKA kuwasiri TANZANIA akiwa na watu kadhaa Walifika TANZANIA na hapo wakapokelewa na mtu aliyejitambulisha kama Captain JOHN KOMBA.
Captain JOHN KOMBA aliwachukua kina MIIKKA moja kwa moja mpaka nyumbani.
Kisha walivyofika hapo MIIKKA akaambiwa
"kuanzia sasa utakuwa unaishi hapa"
MIIKKA akaanza kuishi hapo, lakini siku kadhaa mbele akapelekwa mpaka Tanzania one theatre, ndio hiyo band ya music mnaiita "TOT"
Kwa kuwa MIIKKA alikuwa na utaalamu wa vifaa vya music hapo akatakiwa kufanya kazi fulani zinazohusiana na music.. Akiwa hapo TOT akaweka urafiki wa siku kadhaa na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la KENNY.
KENNY ni shabiki wa music wa kofokafoka, hivyo hakupaswa kuambatana naye kwakuwa hiyo si kazi iliyomleta, ila MIIKKA aliweka urafiki wa siri.
Lakini hata hivyo MIIKKA hakujua kuwa. Kazi hiyo ikiisha anapaswa kurudi nchini kwao FINLAND mara moja.
Baada ya kazi hiyo kuisha, MIIKKA alifanya kama maagizo yalivyo mtaka..
Naam! MIIKKA alirudi nchini kwao FINLAND, ila akiwa FINLAND ndipo. Anasikia anapaswa kuambatana tena na watu kadhaa mpaka nchini ZAMBIA, huko kuna documentary fulani wanapaswa kwenda kufanya.
Safari hiyo ikaanza mara moja Ila wakiwa njiani MIIKKA akabadirisha usafiri na kuchukua usafiri ambao ulimleta mpaka nchini TANZANIA. Alipofikia TANZANIA akamtafuta KENNY,
KENNY akampokea MIIKKA, Kisha akamtambulisha kwa rafiki yake aliyeitwa TONY..
hivyo awamu hii tunaweza kusema wenyeji wa MIIKKA walikuwa ni KENNY na TONY.
MIIKKA akaanza kuonyeshwa chocho za jiji la DAR ES SALAAM lakini. hata hivyo maisha ya getogeto hayakuwa poa sana, pesa ilikata day after day.
MIIKKA akawaza nini cha kufanya, ndipo akamshitua TONY kuwa yeye anaweza ku-produce music.
Yaani kama wakipata sehemu basi wanaweza kutengeneza kipato cha kujikimu..
TONY akaamua kumpeleka. MIIKKA moja kwa moja mpaka zilipo studios za MJ RECORD,
TONY akawaambia wale majamaa aliowakuta pale MJ RECORD kuwa..
Oyaa huyu mtu ni nomaa anaweza ku-produce music mbaya, mchukueni.
Wale majamaa wakasema mpaka wafikishe ujumbe kwa bosi. wao ambaye ni MASTER J.
Hivyo TONY na MIIKKA waliombwa kuondoka, kwamba ujumbe wao ungefikishwa kwa bosi na wangejibiwa siku kadhaa mbele.
Lakini masiku yakasonga bila majibu yoyote.
TONY na MIIKKA wakaona ukimiya nao ni jibu, ndipo TONY alipoamua. Kumpeleka MIIKKA kwa bosi mwingine..
Bosi huyo ambaye alikuwa akimiliki Studios za FM RECORD baada ya kumuona MIIKKA akavutiwa naye na kumpa kazi moja kwa moja... Hapo ndipo historia ya music inapoanza kuandikwa na MIIKKA
MIIKKA akafanya kazi na watu kama
Dully Sykes- julieta
Solid Ground Family-Athumani Mlevi
Zahrani Ft Complex-Tupa Mawe.
Kisha akafanya albam nzima ya saida karoli iitwayo maria salome
lakini hata hivyo. Mwaka 2002 MIIKKA akafanya kazi na msanii MAD ICE wimbo ukaitwa Baby Gal.
Wimbo huu ulivuma mnoo
Moja ya vitu ambavyo MIIKKA alikuwa akivifanya mara zote, akiwa anatengeneza mdundo nikuacha instruments zishike nafasi na beat itembee. Umaarufu wa MIIKKA uliongezeka Na hapo akaanza kujiita MIIKKA MWAMBA..
Yaani majina yake halisi ni MIIKKA ALEKSANTERI KARI, hivyo alibadili jina lake la mwisho ambalo ni KARI liwe kwa Kiswahili na tafsiri yake ni MWAMBA, that's why akajiita MIIKKA MWAMBA.. MIIKKA akaanza kuzungumzwa na kutajwa kama producer chipukizi na hatari kwa ukanda wa East African.
Jambo lililofanya mtu mzima ZIGGY DEE avutike kutoka nchini UGANDA na kuja kufanya naye wimbo ulioitwa ENO MAIKI... Kama huujui wimbo huo wa ZIGGY DEE perhaps unapaswa kutazama vizuri line ya umri wako.
Huu ni wimbo uliamsha hisia za watu, miaka hiyo ulibamba mbaya kwenye makumbi ya starehe club🙌🏻
Na kumfanya MIKKA kuzidi kuzungumzwa kama producer anayekuja kwa kasi
Jambo hili likafanya Wasanii wengi waliokuwa wanajitafuta kwenye game, wamuibukie MIIKKA pale FM RECORD na kuomba kufanya kazi naye.
Alipendwa na wengi, sababu MIIKKA alikua mpole na muelewa lakini pia ni producer aliyempa muda mwanamuziki.
Likewise kwa D KNOB. Wakati ambao D KNOB anajitafuta, akaibukia kwa MIIKKA akamsumbua sana pale, brother najua brother najua.
Basi MIIKKA akaamua kutengeneza beat na kumpa D KNOB ili aifanyie mazoezi.
Kisha MIIKKA akapata safari, akarudi nchini kwao FINLAND. Huku nyuma D KNOB akawa na kazi ya kuandika mistari na kufuta..
Katika uandishi wake wote huo wa kufuta-futa akasahau kuweka chorus.
MIIKKA alivyorudi tu TANZANIA D KNOB akawa wa kwanza kufika studio brother tayari nimemaliza..
MIIKKA akachukua. beat ileile ya D KNOB na kumwambia aimbe ili amsikie..
D KNOB si ndio akaanza kuflow sasa, MIIKKA akashangazwa na alichokisikia na kubaki anacheka..
Unujua alicheka nini, alicheka baada ya kusikia wimbo hauna chorus.
Miaka hiyo ilikuwa ni kitu cha ajabu sana..🙌🏻. Lakini MIIKKA akamshauri D KNOB wajaribu kuweka chorus mwanzo wa nyimbo na mwisho wa nyimbo..
Na baada ya wimbo ule kuachiwa ukawa ni habari nyingine, jambo ambalo hawakulitegemea... MIIKKA akawa gumzo, jambo lililofanya studios tofauti za bongo kutamani kufanya kazi naye..
MIIKKA alikuwa na uwezo wa ajabu wa kutumia instrumental moja ndani ya beat nyingi tofauti.
Na bado instrumental ikaendelea kuleta radha tofauti. Mfano kwenye beat ya wimbo wa MAD ICE Uitwao baby gal. Mule ndani kuna instrumental fulani inafanana na malimba.... Likewise ukija kwenye wimbo wa D KNOB Uitwao Elimu mtaani. Mule ndani kuna instrumental inayofanana na malimba.... Kama hiyo haitoshi ukisikiliza wimbo wa saida karoli uitwao mapenzi kizunguzungu, Mule ndani kuna instrumental inayofanana na malimba...
Lakini ukisikiliza hizi nyimbo zote kila wimbo unakupa radha tofauti🙌🏻
Itoshe kusema MIIKKA alikuwa mwamba kweli..
Aishi sana popote alipo🙏🏼.