KANYABOYA
Kanya Boya ni BOXER bondia wa ngumi za kulipwa wa Burundi
Bondia huyu Felix Kanyaboya kati ya Miaka ya 1986 / 1987 alikuja kucheza Tanzania , Alikuwa anafikia Hotel za Kariakoo.
Bondia huyu alikuwa na Mikwala mingi saana na siku ya Mechi anatoka Hotelini Kariakoo anatembea kwa Miguu akiwa kavalia kabisa Gloves , ring bout, Gum sheed, anapiga shadow box njia nzima na watu wanamshangilia mpk Railways Club Gerezani
Akipanda Ulingoni Round zake 2 tu kapigwa KO mbaya , ndipo Jina lake likavuma KANYABOYA
Anajifanya anajua ngumi, mbwembwe nyingi akipanda Ulingoni anapigwa ndio jina likakuwa KANYABOYA