Baljurashi
JF-Expert Member
- Dec 30, 2017
- 1,628
- 2,720
Kuna jamii gani katika wanaAdam ambayo hakuna mauaji? Ambapo watu hawakupinduana au kuua viongozi wao kwa tamaa za madaraka au sababu zengine?... Unauliza chanzo cha mauwaji kwa waarabu? Ni jadi yao kuinukiana na kumalizana sababu ya fitna na husda tu. Ndio zao.
Kwanza WaOttoman sio Waarabu. Labda useme unawalenga Waislam. Hata kama wangekuwa Waarabu, yaliyotokea kwao (kupinduana na kuuwa watawala) yalitokea na hutokea katika jamii zote za WanaAdam. Sijui kwanini hujawa muadilifu.Hawanaga hata sababu za maana Mzee! Soma historia ya Ottoman uone ndugu alipopata ufalme alivoinukia na kuwamaliza ndugu zake wa karibu! Ni watu wa ajabu kidogo; angalau ustaarabu wa kileo ndio umewabadiilisha.
Wengine wanasemwa wametawala kwa urefu wa mpaka miaka 95.Hapana ni pharaoh Pepi II Neferkare, alianza kutawala akiwa na miaka 6.
Abdul Karim Qassim nae akauawa mwaka 1963.
Ilikua mwaka 1958 Mfalme Hussein wa Jordan aliomba msaada wa kijeshi kutoka Iraq ili kukabiliana na mgogoro wa Lebanon. Mkuu wa majeshi wa Iraq, Colonel Abd al-Karim Qasim aliandaa jeshi. Cha kushangaza alilielekeza jeshi kuingia Ikulu ya Mfalme mjini Baghdad. Mfalme Faisal aliamuru askari wake wasijibu mashambulizi bali wajisalimishe.
Jeshi lilimuamuru Mfalme Abdalah, mke wake Hiyam, mama yake Nafeesa, shangazi yake Abadiya pamoja na wafanya kazi watiifu wa Mfalme wageukie ukutani. Walipigwa risasi. Wote walipoteza maisha pale pale isipokua Mfalme aliokolewa lakini alifia njiani akielekea hospitali.
Kiongozi wa Mapinduzi haya Alikua Kaptain Abdul Sattar Saaba Al-lbousi.
View attachment 2296351
Mfalme Malik Faisal II akikabidhi shahada kwa wahitimu wa chuo kikuu cha Baghdad mwaka 1955.